Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od sura 1 uku. 6-11
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SEHEMU YA MBINGUNI YA TENGENEZO YA YEHOVA
  • TENGENEZO YA YEHOVA IKO NAENDA
  • ‘Tuhakikishe Mambo Yaliyo ya Maana Zaidi’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Nilianza Kuona Maono ya Mungu”
    Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
  • Unaendelea Kusonga Mbele Pamoja na Tengenezo la Yehova?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Yehova Iko Anaongoza Tengenezo Lake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od sura 1 uku. 6-11

SURA YA 1

Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova

MU DUNIA muko matengenezo mingi. Muko matengenezo ya dini, ya politike, ya biashara, na ya kutolea watu misaada. Kila tengenezo iko na kusudi ao mipango yake, mawazo yake, na namna yake ya kufanya mambo. Lakini kuko tengenezo moya yenye iko tofauti kabisa na ile matengenezo yote. Neno ya Mungu inaonyesha waziwazi kama, ile tengenezo ni ya Mashahidi wa Yehova.

2 Inafurahisha juu ulishakuwa mu tengenezo ya Yehova. Tayari unajua mapenzi ya Mungu ni nini, na ulishaanza kuifanya. (Zb. 143:10; Ro. 12:2) Uko mutumishi wa Mungu mwenye kuwa na bidii, na uko nafanya kazi pamoya na ndugu na dada wa mu dunia yote wenye kuwa na upendo. (2 Ko. 6:4; 1 Pe. 2:17; 5:9) Ile inafanya ukuwe na furaha sana na upate baraka mingi, sawa vile Neno ya Mungu inasema. (Mez. 10:22; Mk. 10:30) Kwa kufanya mapenzi ya Yehova kwa uaminifu leo, unajitayarisha kwa ajili ya wakati yenye kuya ya muzuri sana na yenye kudumu.​—1 Ti. 6:18, 19; 1 Yo. 2:17.

3 Muumbaji wetu Mukubwa iko na tengenezo moya tu mu dunia yote, yenye inaongozwa kiteokrasi. Ile inamaanisha kama Yehova, mwenye ni Kichwa juu ya vitu vyote njo iko naingoza. Tunamutumainia kabisa. Yeye ni Muamuzi wetu, Mupaji-sheria wetu, na Mufalme wetu. (Isa. 33:22) Juu yeye ni Mungu wa utaratibu, alishakamata mipango juu ‘tufanye kazi pamoya naye’ ili kutimiza kusudi yake.​—2 Ko. 6:1, 2.

4 Vile tunakaribia sana mwisho wa hii ulimwengu, Kristo Yesu, Mufalme mwenye aliwekwa, njo mwenye anaendelea kutuongoza ili tuendelee kufanya mapenzi ya Yehova muzuri. (Isa. 55:4; Ufu. 6:2; 11:15) Yesu alitabiri kama wafuasi wake watafanya kazi kubwa kuliko ile yenye alifanya mu utumishi wake hapa ku dunia. (Yoh. 14:12) Ile ingewezekana, juu kisha wakati murefu kupita, wafuasi wa Yesu wangekuwa wengi na wangehubiri mupaka maeneo ya mbali zaidi. Wangetangaza habari njema ya Ufalme mupaka kwenye miisho ya dunia.​—Mt. 24:14; 28:19, 20; Mdo. 1:8.

5 Tayari ile unabii iko natimia. Lakini, Yesu alionyesha waziwazi kama, kazi ya kutangaza habari njema itamalizika mu wakati yenye Yehova aliweka. Mambo mingi yenye kuwa mu Neno ya Mungu inaonyesha kama, siku kubwa ya Yehova na yenye kuogopesha sana iko karibu.​—Yoe. 2:31; Sef. 1:14-18; 2:2, 3; 1 Pe. 4:7.

Tunapaswa kujikaza sana kufanya mambo yenye Mungu anatuomba. Ili tuweze kufanya vile, tunapaswa kujua muzuri namna tengenezo ya Mungu iko natumika

6 Mu hii wakati ya mwisho, tayari tunajua mapenzi ya Mungu ni nini. Kwa hiyo, tunapaswa kujikaza sana kufanya mambo yenye Mungu anatuomba. Ili tuweze kufanya vile, tunapaswa kujua muzuri namna tengenezo ya Mungu iko natumika na kuiunga mukono kabisa. Tengenezo ya Mungu iko natumika kwa kufuata kanuni za Maandiko, kutia ndani amri, sheria, maagizo, miongozo, na mafundisho yenye kuwa mu Neno ya Mungu, yenye iliongozwa na roho yake.​—Zb. 19:7-9.

7 Wakati watu wa Yehova wanafuata ile miongozo yenye kutegemea Biblia, wanaishi na kutumika pamoya kwa amani na umoja. (Zb. 133:1; Isa. 60:17; Ro. 14:19) Nini njo iko nasaidia umoja ya ndugu na dada mu dunia yote ikuwe nguvu zaidi? Ni upendo. Ule upendo njo uko natuchochea, na tuko nauvala. (Yoh. 13:34, 35; Kol. 3:14) Kwa kufuata ile njia yenye inamupendeza Yehova Mungu, tunatembea hatua kwa hatua na sehemu ya mbinguni ya tengenezo yake.

SEHEMU YA MBINGUNI YA TENGENEZO YA YEHOVA

8 Mu maono, nabii Isaya, Ezekieli, na Danieli waliona sehemu ya mbinguni ya tengenezo ya Yehova. (Isa., sura. 6; Eze., sura. 1; Da. 7:9, 10) Mutume Yohana pia, aliona namna mambo inapangwa mbinguni, na aliandika kwa kifupi ile mambo mu kitabu ya Ufunuo. Mu maono, aliona Yehova ku kiti ya Ufalme yenye utukufu pamoya na malaika wenye walikuwa wanatangaza hivi: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yehova Mungu, Mweza-Yote, mwenye alikuwa na mwenye iko na mwenye anakuja.” (Ufu. 4:8) Yohana aliona pia “mwana-kondoo . . . akiwa amesimama katikati ya kile kiti cha ufalme,” ni kusema, Mwana Kondoo wa Mungu, Yesu Kristo.​—Ufu. 5:6, 13, 14; Yoh. 1:29.

9 Mu ile maono, Yehova anaikala ku kiti ya Ufalme. Ile inaonyesha kama yeye njo Kichwa ya ile tengenezo. Andiko ya 1 Mambo ya Nyakati 29:11, 12 inasema hivi juu ya Yehova, na juu ya cheo yake ya juu zaidi: “Ee Yehova, ukubwa ni wako na nguvu na uzuri na sifa na utukufu, kwa maana kila kitu mbinguni na duniani ni chako. Ufalme ni wako, Ee Yehova. Wewe Ndiwe mwenye kujiinua mwenyewe ukiwa kichwa juu ya vyote. Utajiri na utukufu vinatoka kwako, na unatawala juu ya kila kitu, na katika mukono wako kuko nguvu na uwezo, na mukono wako unaweza kufanya mutu kuwa mukubwa na kupatia wote nguvu.”

10 Juu Yesu Kristo ni mufanyakazi pamoya na Yehova, iko na cheo ya juu kule mbinguni na alishapewa mamlaka makubwa. Kwa kweli, Mungu ‘aliweka vitu vyote chini ya miguu yake na kumufanya kuwa kichwa juu ya vitu vyote kuhusiana na kutaniko.’ (Efe. 1:22) Mutume Paulo alisema hivi juu ya Yesu: “Mungu alimuinua kwenye cheo cha juu zaidi na kumupatia kwa fazili jina lenye kuwa juu zaidi ya kila jina lingine, ili katika jina la Yesu kila goti lipigwe​—la wale wenye kuwa mbinguni na la wale wenye kuwa duniani na la wale wenye kuwa chini ya udongo—​na kila ulimi ukubali waziwazi kama Yesu Kristo ni Bwana kwa utukufu wa Mungu Baba.” (Flp. 2:9-11) Kwa hiyo, tunaweza kutumainia kabisa uongozi wenye haki wa Yesu Kristo.

11 Mu maono, nabii Daniel aliona Muzee wa Siku ku kiti Yake ya Ufalme mbinguni, na malaika “maelfu elfu [wenye] waliendelea kumutumikia, na elfu kumi mara elfu kumi walisimama mbele yake.” (Da. 7:10) Biblia inaita ile jeshi ya malaika “roho kwa ajili ya utumishi mutakatifu, wenye walitumwa ili kutumikia wale wenye watariti wokovu.” (Ebr. 1:14) Wale malaika wote wamepangwa katika ‘viti vya ufalme, utawala, serikali, na mamlaka.’​—Kol. 1:16.

12 Wakati tunafikiri sana juu ya zile sehemu za mbinguni za tengenezo ya Yehova, tunaweza kuelewa namna Isaya alijisikia wakati ‘alimuona Yehova akiwa amekaa kwenye kiti cha ufalme chenye kuwa juu na chenye kuinuliwa,’ na “maserafi walikuwa wamesimama juu yake.” Isaya alisema hivi: “Ole wangu! Kwa maana ni kama nimekufa, kwa maana mimi ni mutu mwenye hana midomo safi, na ninaishi kati ya watu wenye hawana midomo safi; kwa maana macho yangu yamemuona Mufalme, Yehova wa majeshi mwenyewe!” Kusema kweli, Isaya aliogopa na kujishusha wakati alielewa ukubwa wa tengenezo ya Yehova. Mambo yenye aliona ilimugusa sana, njo maana wakati Yehova alitafuta mutu wa kutuma ili kufanya kazi ya pekee, ya kutangaza hukumu zake, Isaya alisema hivi: “Mimi huyu! Unitume mimi!”​—Isa. 6:1-5, 8.

13 Wakati watu wa Mungu wanatambua na kupenda tengenezo ya Yehova, ile inawasukuma wakuwe tayari kutumwa sawa vile Isaya. Vile tengenezo ya Yehova iko naenda, ni vile pia tuko najikaza kutembea pamoya nayo. Tuko nafanya yetu yote ili kuonyesha kama tunaitumainia.

TENGENEZO YA YEHOVA IKO NAENDA

14 Sawa vile sura ya 1 ya unabii wa Ezekieli inaonyesha, Yehova njo iko naongoza gari kubwa sana ya mbinguni. Ile gari kubwa sana inafananisha sehemu ya tengenezo ya Yehova yenye haionekane. Yehova iko juu ya ile gari, ni kusema, iko naiongoza muzuri na kuitumia kulingana na kusudi yake.​—Zb. 103:20.

15 Kila gurudumu iko na gurudumu ingine ndani yake na magurudumu yote iko na ukubwa uleule. Njo maana Biblia inasema kama, ile magurudumu ‘inaenda upande wowote wa zile pande ine.’ (Eze. 1:17) Magurudumu inaweza kugeukia ngambo ingine palepale bila kukawia. Lakini, ile haimaanishe kama ile gari iko najiongoza yenyewe. Yehova haache tengenezo yake iende fasi yoyote kwenye inapenda. Ezekieli 1:20 inasema hivi: “Yalikuwa yanasonga mahali kwenye roho ilitaka yaende.” Kwa hiyo, kupitia roho yake takatifu, Yehova njo anaongozaka tengenezo yake fasi yote kwenye anapenda iende. Lakini tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Niko natembea hatua kwa hatua pamoya na ile tengenezo?’

16 Kutembea hatua kwa hatua pamoya na tengenezo ya Yehova haiko tu kuenda ku mikutano na kuhubiri, lakini kuko mambo ingine ya kufanya. Kwanza, inaomba kufanya maendeleo na kukomala kiroho. Tunapaswa ‘kuhakikisha mambo ya maana zaidi’ na kuendelea kula chakula ya kiroho yenye tuko napata kwa ukawaida. (Flp. 1:10; 4:8, 9; Yoh. 17:3) Ni muzuri pia kukumbuka kama, tengenezo iko naongozwa muzuri, na wale wenye kuwa ndani wanapaswa kutumika kwa umoja. Kwa hiyo, tunapaswa kuelewa kama ni jambo ya maana tutumie muzuri mali ya kiroho na ya kimwili yenye Yehova iko natupatia ili kutimiza kazi yake. Kwa kuendelea kutembea hatua kwa hatua na gari ya mbinguni ya Yehova, tunaishi kulingana na ujumbe wenye tuko nahubiri.

17 Kwa musaada wa tengenezo ya Yehova Mungu, tunaendelea kufanya mapenzi yake. Tusisahau kama mwenye kuongoza ile gari ya mbinguni ni Yehova. Kwa hiyo, kuendelea kutembea hatua kwa hatua na ile gari inaonyesha kama tunaheshimia na kutumainia Yehova, Mwamba wetu. (Zb. 18:31) Mu Biblia muko hii ahadi: “Yehova atapatia watu wake nguvu. Yehova atabariki watu wake kwa amani.” (Zb. 29:11) Kuwa mu sehemu ya tengenezo ya Yehova leo, inafanya tukuwe na nguvu na amani yenye Yehova anapatia wale wenye kuwa ndani. Bila shaka, Yehova atatubariki sana kama tunaendelea kufanya mapenzi yake sasa na milele.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine