Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od sura 2 uku. 12-16
  • Tambua Daraka Yenye Mungu Alimupatia Kristo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tambua Daraka Yenye Mungu Alimupatia Kristo
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • DARAKA YA KRISTO
  • KUTAMBUA DARAKA YA KRISTO MAANA YAKE NINI?
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od sura 2 uku. 12-16

SURA YA 2

Tambua Daraka Yenye Mungu Alimupatia Kristo

“KATIKA mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia,” na kila kitu yenye alikuwa amefanya kilikuwa “kizuri sana.” (Mwa. 1:1, 31) Wakati Yehova aliumba wanadamu, aliwapatia tumaini ya muzuri sana juu ya wakati yenye kuya. Lakini, uasi yenye ilitokea mu Edeni ilifanya wanadamu wasikuwe tena na furaha kwa wakati fulani. Hata vile, ile haikufanya Yehova abadilishe kusudi yenye alikuwa nayo tangu mwanzo juu ya dunia na juu ya wanadamu. Mungu alisema kama, atakomboa wazao wa Adamu wenye kumutii; ibada safi itarudishwa, na kama ataharibu ule muovu pamoya na kazi zake za mubaya. (Mwa. 3:15) Aliamua kufanya vile juu mambo ikuwe tena ‘muzuri sana.’ Alipanga kutumia Mwana wake, Yesu Kristo juu ya kufanya ile yote. (1 Yo. 3:8) Kwa hiyo, ni lazima kabisa tutambue daraka yenye Mungu alimupatia Kristo.​—Mdo. 4:12; Flp. 2:9, 11.

DARAKA YA KRISTO

2 Wakati tunafikiria daraka yenye Mungu alimupatia Kristo, tunatambua kama ile inatia ndani mambo mingi. Yesu ni Mukombozi wa wanadamu, ni Kuhani Mukubwa, ni Kichwa ya kutaniko ya Kikristo, na sasa ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Kufikiri sana juu ya ile madaraka yote, inafanya tumushukuru zaidi sana Mungu, na inatusaidia tumupende sana Yesu Kristo. Tuone vile Biblia inazungumuzia madaraka mbalimbali yenye Yesu Kristo iko nayo.

Yehova atamutumia Yesu ili kutimiza kusudi yake juu ya wanadamu

3 Wakati wa utumishi wa Kristo hapa ku dunia, ilionekana wazi kama, ni kupitia yeye njo wanadamu wenye kutii watapatanishwa na Mungu. (Yoh. 14:6) Juu ni Mukombozi wa wanadamu, Yesu alitoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi. (Mt. 20:28) Yesu alikuwa mufano muzuri kwa kuwa na mwenendo wenye kumupendeza Mungu. Lakini zaidi ya ile, Yehova atamutumia Yesu ili kutimiza kusudi yake juu ya wanadamu. Ni kupitia yeye tu njo tunaweza kukubaliwa na Mungu. (Mdo. 5:31; 2 Ko. 5:18, 19) Kupitia kifo yake ya kujizabihu na ufufuo wake, Yesu alifungulia wanadamu wenye kutii njia ya kupata baraka za milele chini ya utawala wa mbinguni wa Ufalme wa Mungu.

4 Yesu ni Kuhani Mukubwa. Kwa hiyo, anaweza “kusikilia uzaifu wetu huruma” na anaweza kufunika zambi za wafuasi wake wenye kuwa hapa ku dunia wenye walijitoa kwa Mungu. Mutume Paulo alisema hivi: “Hatuna kuhani mukubwa mwenye hawezi kusikilia uzaifu wetu huruma, lakini tuko naye mwenye amejaribiwa katika mambo yote kama vile sisi, lakini bila kufanya zambi.” Kisha, Paulo alitia moyo wale wenye kuwa na imani katika Yesu Kristo wafaidike kabisa na ile mupango yenye inawasaidia wajipatanishe na Mungu. Alisema hivi: “Basi, tukaribie kiti cha ufalme cha fazili zenye hazistahiliwe tukiwa na uhuru wa kusema, kusudi tupokee rehema na tupate fazili zenye hazistahiliwe ili zitusaidie wakati wenye kufaa.”​—Ebr. 4:14-16; 1 Yo. 2:2.

5 Pia, Yesu ni Kichwa ya kutaniko ya Kikristo. Wafuasi wake wa kwanza hawakukuwa na kiongozi mwanadamu. Ni vile pia kwetu leo. Iko natoa muongozo kupitia roho takatifu na kupitia wachungaji wadogo wenye kustahili. Wale wachungaji watatoa hesabu kwake na kwa Baba yake wa mbinguni, kuhusu namna wako nachunga kundi ya Mungu. (Ebr. 13:17; 1 Pe. 5:2, 3) Katika unabii yenye kuwa mu Biblia, Yehova alisema hivi kumuhusu Yesu: “Angalia! Nilimufanya kuwa shahidi kwa mataifa, kiongozi na kamanda kwa mataifa.” (Isa. 55:4) Yesu alionyesha kama ile unabii ilitimia wakati aliambia wanafunzi wake hivi: “Wala musiitwe viongozi, kwa maana Kiongozi wenu ni mumoja, Kristo.”​—Mt. 23:10.

6 Ili kuonyesha kama anapenda na kama iko tayari kutusaidia, Yesu anatutolea hii mualiko: “Mukuje kwangu, ninyi wote wenye kuteseka na wenye kulemewa na mizigo, na mimi nitawapumuzisha. Mubebe nira yangu na mujifunze kupitia mimi, kwa maana mimi ni mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo, na mutapata pumuziko kwa ajili yenu. Kwa maana nira yangu haiko yenye kuumiza, na muzigo wangu ni mwepesi.” (Mt. 11:28-30) Kwa kuongoza kutaniko ya Kikristo kwa upole na mu njia yenye inatuletea pumuziko, Yesu Kristo anaonyesha waziwazi kama yeye ni “muchungaji mwema” kwa sababu anamuiga Baba yake wa Mbinguni, Yehova Mungu.​—Yoh. 10:11; Isa. 40:11.

7 Mu barua ya kwanza, yenye mutume Paulo aliandikia Wakorinto, alionyesha daraka ingine ya Yesu Kristo. Alisema hivi: “Anapaswa kutawala akiwa mufalme mupaka wakati Mungu atakuwa ameweka maadui wote chini ya miguu yake. Lakini wakati vitu vyote vitakuwa vimewekwa chini ya mamlaka yake, halafu Mwana mwenyewe atajiweka chini ya mamlaka ya Ule mwenye aliweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, ili Mungu akuwe vitu vyote kwa kila mutu.” (1 Ko. 15:25, 28) Yesu njo muzaliwa wa kwanza wa uumbaji wa Mungu, na mbele akuye hapa ku dunia, alikuwa “fundi wa kazi” wa Mungu. (Mez. 8:22-31) Wakati Mungu alimutuma Yesu hapa ku dunia, Yesu alikuwa anafanya mapenzi ya Mungu kila siku. Alivumilia mateso makubwa zaidi, alikufa na iko muaminifu kwa Baba yake. (Yoh. 4:34; 15:10) Juu alibakia muaminifu mupaka kifo, Mungu alimufufua ili aishi mbinguni na akamupatia haki ya kuwa Mufalme wa Ufalme wa mbinguni. (Mdo. 2:32-36) Vile ni Mufalme, Mungu alimupatia daraka ya kuongoza makumi ya maelfu ya viumbe wa roho wenye nguvu ili kutosha utawala wa wanadamu na mambo yote ya mubaya yenye kuwa mu dunia. (Mez. 2:21, 22; 2 Te. 1:6-9; Ufu. 19:11-21; 20:1-3) Kisha ile mambo yote, ni Ufalme wa Mungu tu wenye kuongozwa na Yesu Kristo njo utatawala dunia yote.​—Ufu. 11:15.

KUTAMBUA DARAKA YA KRISTO MAANA YAKE NINI?

8 Yesu Kristo, Mufano wetu, ni mukamilifu. Alipewa daraka ya kutuhangaikia. Juu Yesu anatuonyesha upendo na kutuhangaikia, tunapaswa kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova na kutembea hatua kwa hatua na tengenezo ya Yehova yenye iko naenda mbele.

9 Wafuasi wa kwanza wa Yesu walitambua kabisa daraka yenye Mungu alimupatia Kristo. Walifanya vile kwa kutumika pamoya kwa umoja chini ya uongozi wa Kristo, na kufuata kwa unyenyekevu muongozo yenye alitoa kupitia roho takatifu. (Mdo. 15:12-21) Mutume Paulo alizungumuzia umoja ya Wakristo watiwa-mafuta wa kutaniko, wakati aliandika hivi: “Tukisema kweli, kupitia upendo tuendelee kukomaa katika mambo yote ndani ya ule mwenye ni kichwa, Kristo. Kutoka kwake mwili wote unaunganishwa pamoya kwa upatano na kufanywa ushirikiane kupitia kila kiungo chenye kinatoa kile chenye kinahitajika. Wakati kila kiungo kinafanya kazi muzuri, hilo linafanya mwili ukomae wakati unajijenga wenyewe katika upendo.”​—Efe. 4:15, 16.

10 Wakati ndugu na dada wanatumika kwa umoja na kwa upatano chini ya uongozi wa Kristo, ile inafanya kukuwe ongezeko na upendo, wenye ni “kifungo kikamilifu cha umoja.”​—Yoh. 10:16; Kol. 3:14; 1 Ko. 12:14-26.

11 Mambo yenye kutokea mu dunia leo, yenye inatimiza unabii mbalimbali wenye kuwa mu Biblia, inaonyesha waziwazi kama Yesu Kristo alipewa mamlaka ya Ufalme tangu mwaka wa 1914. Kwa sasa, iko anatawala katikati ya maadui wake. (Zb. 2:1-12; 110:1, 2) Ile inamaanisha nini kwa wale wenye kuishi ku dunia leo? Hivi karibuni, Yesu ataonyesha kabisa kama ni Mufalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, wakati ataleta hukumu ya Yehova Mungu juu ya maadui wake. (Ufu. 11:15; 12:10; 19:16) Kisha, ahadi ya Yehova ya kukomboa wanadamu yenye alitoa ku mwanzo wa uasi itatimia kwa wale wenye kuwa ku mukono wa kuume wa Kristo. (Mt. 25:34) Kutambua daraka yenye Mungu alimupatia Kristo kunatuletea furaha sana! Mu hizi siku za mwisho, tuendelee basi kutumika kwa umoja mu kazi ya kuhubiri yenye iko nafanyika mu dunia yote chini ya uongozi wa Kristo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine