Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od sura 4 uku. 24-29
  • Kutaniko Inapangwa na Kuongozwa Namna Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kutaniko Inapangwa na Kuongozwa Namna Gani?
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUTANIKO INAPANGWA KITEOKRASI
  • LEO PIA MAKUTANIKO INAFUATA MUFANO WA MITUME
  • KAZI YENYE MATENGENEZO FULANI YA MASHAHIDI INAFANYAKA
  • NAMNA MAMBO INAPANGWA MU BIRO ZA TAWI
  • Waangalizi wa Kuchunga Kundi
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Tengenezo Linalotumikia “Mungu wa Amani”
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od sura 4 uku. 24-29

SURA YA 4

Kutaniko Inapangwa na Kuongozwa Namna Gani?

MUTUME Paulo alitaya kweli moya ya maana juu ya Mungu mu barua yake ya kwanza yenye aliandikia Wakorinto. Aliandika hivi: “Mungu haiko Mungu wa muvurugo lakini ni wa amani.” Kisha, wakati alizungumuzia mikutano ya kutaniko, alisema: “Mambo yote yatendeke kwa adabu na kwa utaratibu.”​—1 Ko. 14:33, 40.

2 Ku mwanzo-mwanzo tu ya ile barua, mutume Paulo alishauria kutaniko ya Korinto juu ya migawanyiko yenye ilikuwa ndani. Paulo aliomba ndugu na dada wa mu ile kutaniko ‘waseme kwa upatano’ na ‘waunganishwe kabisa katika akili ileile na njia ileile ya kufikiri.’ (1 Ko. 1:10, 11) Kisha aliwashauria juu ya hali yenye ilikuwa inaharibisha umoja wa kutaniko. Paulo alitumia mufano ya mwili ya mutu juu ya kuwasaidia waone kama umoja na upatano ni mambo ya lazima sana mu kutaniko. Aliomba wote mu kutaniko watendeane kwa upendo, hata kama hawako na madaraka ileile. (1 Ko. 12:12-26) Juu kukuwe upatano kati ya ndugu na dada mu kutaniko, inaomba kutaniko ipangwe muzuri.

3 Lakini kutaniko ya Kikristo ilipaswa kupangwa namna gani? Ni nani mwenye angeipanga? Ingefuata mufano gani? Ni nani wangepewa madaraka? Kama tunaacha Biblia ituongoze, tutapata majibu yenye kuwa wazi ya ile maulizo.​—1 Ko. 4:6.

KUTANIKO INAPANGWA KITEOKRASI

4 Kutaniko ya Kikristo ilianzishwa siku ya Pentekoste 33 K.K.Y. Tunajua mambo gani kuhusu kutaniko ya wakati wa mitume? Tunajua kama ilipangwa na kuongozwa kiteokrasi, ni kusema, ilikuwa chini ya utawala (Kigiriki, the·osʹ) wa Mungu (kraʹtos). Ile maneno mbili inapatikana mu 1 Petro 5:10, 11. Mu Biblia muko habari moya yenye inaonyesha mambo yenye ilitokea mu Yerusalemu, kumepita miaka 2 000 hivi. Ile habari inaonyesha wazi kama Mungu njo alianzisha kutaniko ya watiwa-mafuta. (Mdo. 2:1-47) Ile kutaniko ilikuwa jengo ao nyumba yake. (1 Ko. 3:9; Efe. 2:19) Leo pia, kutaniko ya Kikristo inapangwa na kutumika sawa vile kutaniko ya wakati wa mitume.

Leo pia, kutaniko ya Kikristo inapangwa na kutumika sawa vile kutaniko ya wakati wa mitume

5 Kutaniko ya kwanza ilianza na wanafunzi 120 hivi. Ili kutimiza unabii wenye uko mu Yoeli 2:28, 29, Mungu alimwangia kwanza wale wanafunzi roho yake takatifu. (Mdo. 2:16-18) Lakini ileile siku, watu wengine 3 000 hivi walibatizwa mu maji na kuingizwa mu kutaniko ya Wakristo wenye walizaliwa kwa roho. Waliitika neno yenye ilihusu Kristo na “wakaendelea kujitoa wenyewe kwa fundisho la mitume.” Kisha pale, “Yehova akaendelea kuwaongezea kila siku watu wenye walikuwa wanaokolewa.”​—Mdo. 2:41, 42, 47.

6 Kutaniko ya Yerusalemu iliendelea kuongezeka sana, mupaka kuhani mukubwa wa Wayahudi akaanza kulalamika kwa kusema kama wanafunzi wamejaza Yerusalemu na mafundisho yao. Kati ya wanafunzi wapya mu Yerusalemu, mulikuwa pia makuhani wengi Wayahudi wenye walifikia kuwa mu ile kutaniko.​—Mdo. 5:27, 28; 6:7.

7 Yesu alisema hivi: “Mutakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Ile maneno ilitimia. Kisha Stefano kuuawa, mateso mingi ilitokea mu Yerusalemu. Ile ilifanya wanafunzi wenye walikuwa naishi mule wasambazwe mu Yudea na Samaria yote. Lakini, kila fasi kwenye walienda, waliendelea kutangaza habari njema na kufanya wanafunzi wengi. Hata watu fulani wa Samaria walifanywa kuwa wanafunzi. (Mdo. 8:1-13) Kisha pale, watu wenye hawatahiriwe, ni kusema, watu wenye hawakukuwaka Wayahudi, walihubiriwa habari njema na wakaikubali. (Mdo. 10:1-48) Ile kazi yote ya kuhubiri, ilisaidia kupata wanafunzi wengi na kuanzisha makutaniko ya mupya inje ya Yerusalemu.​—Mdo. 11:19-21; 14:21-23.

8 Ni mipango gani yenye ilifanywa ili kuhakikisha kama kila kutaniko ya mupya inapangwa na kuongozwa kiteokrasi, ni kusema, vile Mungu anapenda? Kupitia utendaji wa roho ya Mungu, wachungaji walichaguliwa ili kutunza kundi. Mu safari yao ya kwanza ya umisionere, mutume Paulo na Barnaba waliweka wazee mu makutaniko yenye walitembelea. (Mdo. 14:23) Luka, mwenye ni mumoja wa waandikaji wa Biblia, anaeleza juu ya mukutano wenye mutume Paulo alifanya pamoya na wazee wa kutaniko ya Efeso. Mutume Paulo aliwaambia hivi: “Mujiangalie ninyi wenyewe na kundi lote, lenye roho takatifu imewaweka ninyi kuwa waangalizi kati yake, ili kuchunga kutaniko la Mungu, lenye alinunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe.” (Mdo. 20:17, 28) Walistahili kuwa wazee, juu walitimiza mambo yenye Biblia inaomba ili kuwa muzee wa kutaniko. (1 Ti. 3:1-7) Mutume Paulo aliambia Tito, mufanyakazi mwenzake, aweke wazee mu makutaniko ya Krete.​—Tito 1:5.

9 Vile makutaniko iliendelea kuongezeka, ni vile mitume na wanaume wazee mu Yerusalemu waliendelea kuwa waangalizi wenye kuongoza kutaniko ya Kikristo ya mu dunia yote ya wakati wa mitume. Ni wao njo walifanyiza baraza yenye kuongoza ya ile wakati.

10 Wakati mutume Paulo aliandikia Wakristo wa kutaniko ya Efeso, alisema kama juu kutaniko ya Kikristo iendelee kuwa na umoja na iendelee kutii mamlaka ya Yesu, ni lazima kufuata muongozo wa roho ya Mungu. Mutume Paulo aliwatia moyo waendelee kuonyesha unyenyekevu na waendelee kuwa na “umoja wa roho” kwa kuishi kwa amani pamoya na ndugu na dada wote wa kutaniko. (Efe. 4:1-6) Kisha alitaya maneno ya Zaburi 68:18, na kuonyesha kama maneno yenye kuwa ndani inahusu mupango wa Yehova wa kuwa na wanaume wenye wanastahili kiroho ili kuwa mitume, manabii, waeneza-injili, wachungaji, na walimu wa kutumikia kutaniko. Wale wanaume ni zawadi kutoka kwa Yehova. Kwa hiyo, wangesaidia kutaniko yote iendelee kukomala kiroho juu imupendeze.​—Efe. 4:7-16.

LEO PIA MAKUTANIKO INAFUATA MUFANO WA MITUME

11 Leo, makutaniko yote ya Mashahidi wa Yehova inaongozwa namna makutaniko ilikuwa naongozwa mu siku za mitume. Ile makutaniko yote inafanyiza kutaniko moya yenye umoja mu dunia yote, na Wakristo watiwa-mafuta njo musingi wa ile kutaniko. (Zek. 8:23) Yesu njo anafanya ile iwezekane. Anaendelea kutimiza kwa uaminifu ahadi yenye aliambiaka wanafunzi wake watiwa-mafuta, yenye inasema kama ataendelea kuwa nao “sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” Leo, watu wenye wako najiunga na kutaniko yenye iko naongezeka, wanaitikia habari njema ya Mungu, wanajitoa kwa Yehova kwa moyo wote, kisha wanabatizwa na kuwa wanafunzi wa Yesu. (Mt. 28:19, 20; Mk. 1:14; Mdo. 2:41) Wanatambua kama Yesu Kristo, “muchungaji mwema,” njo Kichwa ya kundi yote yenye inafanyizwa na Wakristo watiwa-mafuta na “kondoo wengine.” (Yoh. 10:14, 16; Efe. 1:22, 23) Ile “kundi moja” inaendelea kuwa na umoja kwa kutambua kwa uaminifu cheo ya Kristo na pia kwa kutii njia yenye anatumia ili kuongoza tengenezo, ni kusema, “mutumwa muaminifu na mwenye busara,” mwenye aliweka. Tuendelee basi kutumainia mutumwa muaminifu na mwenye busara.​—Mt. 24:45.

KAZI YENYE MATENGENEZO FULANI YA MASHAHIDI INAFANYAKA

12 Ili kutoa chakula ya kiroho kwa wakati yenye kufaa na kufanya habari njema ya Ufalme ihubiriwe mbele mwisho ifike, tengenezo ya Yehova ilishakaanzisha matengenezo fulani. Ile matengenezo ni yenye kukubaliwa na sheria mu inchi mbalimbali, na yote inatumika mu umoja. Inasaidia ikuwe mwepesi kufanya kazi ya kuhubiri habari njema mu dunia yote.

NAMNA MAMBO INAPANGWA MU BIRO ZA TAWI

13 Wakati biro ya tawi inaanzishwa mu inchi fulani, Halmashauri ya Tawi yenye kuwa na wazee watatu ao zaidi inafanywa ili kuongoza kazi mu ile inchi na pia mu inchi zingine zenye ile tawi inasimamia. Muzee moya kati yao, anawekwa kuwa muratibu wa Halmashauri ya Tawi.

14 Makutaniko yenye kila tawi inaongoza, inagawanywa mu mizunguko. Ile mizunguko inaweza kuwa na ukubwa tofauti-tofauti; ile inategemea luga ao hali ya eneo, ao hesabu ya makutaniko yenye iko mu eneo yenye inaongozwa na tawi. Mwangalizi wa muzunguko anawekwa ili atumikie makutaniko mu kila muzunguko. Juu mwangalizi wa muzunguko ajue namna ya kutimiza kazi yake, biro ya tawi inamutoleaka muongozo.

15 Ndugu na dada mu makutaniko, wanafuata mipango yenye kufanywa mu tengenezo, yenye inatolewa kwa faida ya wote. Wanakubali wazee wenye tengenezo inaweka ili wasimamie kazi ku tawi, mu mizunguko, na mu makutaniko. Wanajua kama ni mutumwa muaminifu na mwenye busara tu njo anapaswa kuwatolea chakula ya kiroho kwa wakati wenye kufaa. Mu siku zetu pia, mutumwa muaminifu anakubali kabisa ukichwa wa Kristo, anashikamana na kanuni za Biblia, na kutii muongozo wa roho takatifu. Na siye pia, wakati tunatumika mu umoja, tunapata matokeo ya muzuri sawa ile yenye Wakristo wa wakati wa mitume walipataka. Biblia inasema hivi juu yao: “Kwa kweli, makutaniko yakaendelea kuwa nguvu katika imani na hesabu ya waamini iliendelea kuongezeka siku kwa siku.”​—Mdo. 16:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine