Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od sura 12 uku. 123-129
  • Kutegemeza Kazi ya Ufalme mu Eneo Yenu na mu Dunia Yote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kutegemeza Kazi ya Ufalme mu Eneo Yenu na mu Dunia Yote
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUTEGEMEZA FAIDA ZA UFALME MU DUNIA YOTE
  • KUTEGEMEZA MAHITAJI YA KUTANIKO YENU
  • NAMNA MICHANGO INATUMIWAKA
  • GARAMA ZA MUKUSANYIKO WA MUZUNGUKO
  • KUHANGAIKIA MASKINI
  • KUGAWANYA VICHAPO
  • Feza za Kuendesha Kazi za Ufalme Zinatoka Wapi?
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Waangalizi wa Kuchunga Kundi
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Namna ya Kupanua Utumishi Wako
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Sababu Gani Umutolee Ule Mwenye Kuwa na Kila Kitu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od sura 12 uku. 123-129

SURA YA 12

Kutegemeza Kazi ya Ufalme mu Eneo Yenu na mu Dunia Yote

ILI KUTIMIZA unabii wa Yesu kuhusu siku za mwisho, Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi ya kuhubiri habari njema “mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8; Mt. 24:14) Juu waweze kufanya vile, wanatoa kwa kujipendea wakati na nguvu yao ili kuendelesha faida za Ufalme. Juu wanajua kama Yehova hakose kutimizia wafanyakazi wenzake mambo yenye wako nayo lazima, wanaendelea kutia Ufalme wake pa nafasi ya kwanza mu maisha yao. (Mt. 6:25-34; 1 Ko. 3:5-9) Matokeo yenye wanapata mu hii kazi, inaonyesha wazi kama Yehova anawakubali na anawabariki.

KUTEGEMEZA FAIDA ZA UFALME MU DUNIA YOTE

2 Wakati watu wanaona njia zenye tunatumia ili kuhubiri na vile tunatoleaka watu Biblia na vichapo vya kusaidia kujifunza Biblia bila kuomba makuta, wamoya wanajiulizaka hivi: “Hii inawezekana namna gani?” Ni kweli, inaomba makuta ili kuchapisha na kutolea watu Biblia na vichapo vingine vyenye kusaidia kujifunza Biblia. Inaomba pia makuta ili kujenga na kutunza Beteli, ni kusema, fasi kwenye kunaishi watumishi wenye wanasaidia mu kazi ya kuchapisha, wenye wanasimamia kazi ya kuhubiri, na wengine wote wenye wanafanya kazi mbalimbali ku Beteli ili kuendelesha habari njema. Tena waangalizi wa mizunguko, wamisionere, mapainia wa pekee, na watumishi wengine wa wakati wote wanapewa makuta kidogo yenye inawasadia kuendelea na kazi yao. Ni wazi kama, kazi ya kuhubiri habari njema leo, ikuwe mu eneo yetu ao mu dunia yote, inaomba makuta mingi sana. Sasa, ile makuta yote inatokaka wapi?

3 Watu wengi wanapendezwa na kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kufundisha watu Biblia mu dunia yote; kwa hiyo, wanafurahiaka kutoa michango yao juu ya kutegemeza ile kazi. Lakini, ni Mashahidi kwanza njo wanatoaka michango ya kujipendea kwa ajili ya ile kazi. Wamoya wanatuma kwa kujipendea, michango yao ku biro ya tawi ya mu inchi yao. Sawa vile watumishi wa zamani wa Mungu, Mashahidi wa Yehova pia wanaonyesha roho ya ukarimu kwa kutoa michango ili kujenga mahali pa ibada kwa ajili ya Yehova. (Kut. 35:20-29; 1 Ny. 29:9) Wengine wanapatiaka tengenezo vitu vyao vya lazima. Lakini, michango ingine ya kidogo-kidogo, inatolewaka na mutu mumoya-mumoya, makutaniko na mizunguko. Wakati ile michango yote inakusanywa, makuta ya kuendelesha kazi ya Ufalme inapatikana.

Mashahidi wa Yehova wanaona kama ni pendeleo kutumia makuta na vitu vingine vyenye wako navyo ili kuendelesha kazi ya kuhubiri

4 Mashahidi wa Yehova wanaona kama ni pendeleo kutumia makuta na vitu vingine vyenye wako navyo ili kuendelesha kazi ya kuhubiri. Yesu na mitume wake walikuwa na kisanduku ya kuweka amo makuta, na ni ile ilikuwa nawasaidia wakati walikuwa na lazima ya kitu fulani. (Yoh. 13:29) Biblia inazungumuzia wanamuke wenye walitumia vitu vyao ili kusaidia Yesu na mitume wake. (Mk. 15:40, 41; Lu. 8:3) Paulo alikubali kwa furaha musaada wenye ulitolewa kwa upendo na ndugu wenye walipenda kazi ya kuhubiri habari njema iendelee na wenye walipenda kuifanya. (Flp. 4:14-16; 1 Te. 2:9) Mashahidi wa Yehova wanaendelea kufuata ile mufano kwa kuwa wenye bidii na wakarimu. Ile yote, inafanya iwezekane fasi yote kupatia watu wenye mioyo ya muzuri “maji ya uzima bure.”​—Ufu. 22:17.

KUTEGEMEZA MAHITAJI YA KUTANIKO YENU

5 Michango ya kujipendea inatumiwa pia ili kulipia garama za kutaniko. Hakuna kuomba sadaka, kukusanya makuta kutoka kwa watu, na hakuna mutu mwenye analazimishwa kutoa kiasi fulani ya makuta. Lakini, kunakuwaka visanduku vya michango fasi kwenye tunafanyiaka mikutano, juu ya kusaidia kila mutu mwenye anapenda “afanye kama vile alikusudia katika moyo wake.”​—2 Ko. 9:7.

6 Makuta yenye inatiwa mu vile visanduku, inatumiwa kwanza mu mambo yenye inahusu Jumba ya Ufalme na inatumiwa ili kuitunza. Baraza ya wazee inaweza amua kutuma kiasi fulani ya makuta ku biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya mu inchi yao, ili kutegemeza kazi ya kuhubiri mu dunia yote. Juu ya kufanya vile, kutaniko inapaswa kufanya azimio. Kufanya vile, inasaidia makutaniko mingi ikuwe inatoa kila mara michango kwa ajili ya kazi ya kuhubiri mu dunia yote. Kila mutu mu kutaniko akielewa kama kutaniko haiwezi kosa kuwa na mahitaji, ile itasaidia kuepuka kuwa nafanya saa yote matangazo juu ya kutoa michango.

NAMNA MICHANGO INATUMIWAKA

7 Kisha kila mukutano, ndugu wawili wanafunguaka visanduku vya michango, wanahesabia makuta yenye ilitiwa ndani na kuandika ile hesabu. (2 Fa. 12:9, 10; 2 Ko. 8:20) Baraza ya wazee inafanya mipango ya kuchunga muzuri ile makuta, mupaka siku itatumwa ku biro ya tawi ao kutumiwa na kutaniko. Kila mwezi, ndugu mwenye anasimamia konte ya kutaniko, anafanya ripoti ili kujulisha kutaniko hali ya konte. Na kisha kila miezi tatu, muratibu wa baraza ya wazee anafanya mipango ili kuchunguza konte ya kutaniko.

GARAMA ZA MUKUSANYIKO WA MUZUNGUKO

8 Garama zenye zinafanywa ku mikusanyiko ya muzunguko, na garama zingine za muzunguko, zinalipwa na ndugu na dada wa ile muzunguko. Njo maana, visanduku vya michango vinawekwaka fasi ya kufanyia ile mikusanyiko, juu ya kusaidia wenye wanapenda kutoa michango kwa ajili ya muzunguko. Pia, makutaniko inaweza kutoa michango wakati yoyote juu ya kusaidia kulipia garama zingine za muzunguko.

9 Kila muzunguko inapaswa kujilipia garama zake zote, na makuta yote yenye ilipita inapaswa kutumwa kwa ajili ya kazi ya mu dunia yote. Kama kisha mukusanyiko, michango haienee ili kulipia garama zenye zilifanywa ao ili kulipia garama za mukusanyiko wenye utakuya, sawa vile makuta ya kulipia fasi ya kufanyia mukusanyiko, mwangalizi anaweza kukamata mipango ili makutaniko iandikiwe juu ya kufanya michango. Kila baraza ya wazee itazungumuza pamoya na kuamua kiasi ya makuta yenye kutaniko yao itatuma mu konte ya muzunguko. Kisha pale, watafanya azimio na kutaniko juu ya ile makuta.

10 Wakati kunatokea mambo yenye inahusu makuta yenye inaomba kushugulikiwa na wazee wote wa muzunguko, wazee watafanya mukutano juu ya ile jambo siku ya mukusanyiko wa muzunguko. Zaidi ya maamuzi yenye wazee washakakamata kuhusu garama za pekee za mukusanyiko, wazee wote wanapaswa kufanya maazimio na kukubaliana juu ya maamuzi ingine yote yenye inahusu kutumia makuta ya muzunguko. Mu ile maazimio inaomba kuonyesha kiasi ya makuta ya kutumia, na kila mara wakati inaomba kutumia makuta ya muzunguko inaomba wazee waone ile maazimio juu wakubaliane.

11 Mipango inafanywa juu konte ya muzunguko ikuwe inachunguzwa kwa ukawaida.

KUHANGAIKIA MASKINI

12 Sababu ingine yenye ilifanya Yesu na mitume wake wakuwe na kisanduku fulani ya makuta, ilikuwa juu ya kusaidia maskini. (Mk. 14:3-5; Yoh. 13:29) Ili kuonyesha kama Wakristo wangeendelea kuwa na daraka ya kusaidia maskini, Yesu alisema hivi: “Maskini muko nao sikuzote.” (Mk. 14:7) Namna gani Mashahidi wa Yehova wanatimiza ile daraka leo?

13 Wakati fulani, Wakristo waaminifu mu kutaniko wanaweza kuwa na lazima ya musaada juu wamezeeka, ni vilema ao juu ya magumu ingine yenye wanaweza kupata. Kwa hiyo, watu wa familia, watu wa jamaa na ndugu wengine wenye wanajua ile hali wanaweza kupenda kusaidia. Ile inapatana na hii maneno ya mutume Yohana: “Kama mutu yeyote iko na vitu vya ulimwengu huu na anaona ndugu yake katika uhitaji lakini anakataa kumuonyesha huruma, namna gani upendo wa Mungu unakaa ndani yake? Watoto wadogo, tunapaswa kupendana, hapana kwa neno ao kwa ulimi, lakini kwa tendo na kweli.” (1 Yo. 3:17, 18; 2 Te. 3:6-12) Ibada ya kweli inatuomba pia kuhangaikia Wakristo waaminifu wenye kuwa na lazima ya musaada wa kimwili.​—Yak. 1:27; 2:14-17.

14 Mu barua yake ya kwanza kwa Timoteo, mutume Paulo alionyesha namna ya kusaidia wale wenye kuwa na lazima ya musaada wa kimwili. Unaweza kusoma shauri yenye alitoa mu 1 Timoteo 5:3-21. Kila Mukristo iko na daraka ya kutimiza mahitaji ya watu wa familia yake. Wakristo wenye kuzeeka ao wenye kuwa vilema, wanapaswa kusaidiwa na watoto wao, watoto wa watoto wao, na watu wengine wa jamaa. Wakati fulani, serikali ao mashirika fulani ya kutolea watu misaada inaweza kuwa na mipango ya kusaidia watu wa vile; kwa hiyo, watu wa jamaa ao ndugu wengine wanaweza kuwasaidia ili wafaidike na ile misaada. Hali fulani inaweza kutokea yenye inaomba kutaniko yote ifikirie musaada fulani wa kimwili wa kupatia ndugu na dada wenye wametumikia Yehova kwa uaminifu mu miaka mingi. Kama hawana watu wa familia ao watu wa jamaa wa kuwasaidia, ao pengine hawapate musaada wenye kufaa kutoka ku mashirika ya serikali ya kutoa misaada, baraza ya wazee inaweza kupendekeza kutaniko itoe musaada fulani. Wakristo wanaona kama ni pendeleo kutumia vitu vyao vya kimwili ili kusaidia wale wenye kuwa na lazima ya musaada.

15 Mateso, vita, matetemeko ya inchi, magonjwa, njala, na misiba ingine yenye kutokea mu hii wakati ya hatari, inafanya ndugu na dada zetu wengi wakuwe na lazima ya musaada. (Mt. 24:7-9) Inawezekana, makutaniko ya fasi kwenye kunatokea mambo ya vile haina uwezo wa kusaidia ndugu zao; kwa hiyo, Baraza Yenye Kuongoza inafanya mipango ili ndugu wa fasi ingine ao wa mu inchi ingine wawatolee musaada. Ile inafanana na yenye Wakristo wa eneo ya Asia Ndogo walifanyaka; wakati ndugu zao wa Yudea walikuwa mu kipindi ya njala, waliwatolea chakula. (1 Ko. 16:1-4; 2 Ko. 9:1-5) Wakati tunafuata ile mufano, tunaonyesha kama tunapenda ndugu zetu na tunaonyesha kabisa kama tuko wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo.​—Yoh. 13:35.

KUGAWANYA VICHAPO

16 Biblia na vichapo vyetu vinasaidia sana ili kueneza ujumbe wa Ufalme. Kwa kawaida, baraza ya wazee inachagua mutumishi wa huduma wa kushugulikia vichapo mu kutaniko. Ndugu wenye wanapewa ile kazi, wanaichukua kwa uzito. Wanachunga muzuri dosye zenye zinahusu mambo ya vichapo juu kutaniko isikuwe nakosa vichapo vya kutumia.

17 Juu tuko Wakristo wenye walijitoa kwa Mungu, tunajua kama wakati wetu, uwezo wetu wa akili na wa kimwili, kipaji na mali yetu, na hata uzima wetu ni zawadi zenye Mungu ametupatia. Na ametupatia azo juu zitusaidie kufanya kazi yake. (Lu. 17:10; 1 Ko. 4:7) Wakati tunatumia muzuri vitu vyote vyenye tuko navyo, tunaonyesha kama tunamupenda sana Yehova. Tunapenda kumuheshimia Yehova na vitu vyetu vya samani, juu tunajua kama anapendezwa na kila zawadi yenye tunamutolea ili kuonyesha kama tulijitoa kwake kwa nafsi yetu yote. (Mez. 3:9; Mk. 14:3-9; Lu. 21:1-4; Kol. 3:23, 24) Yesu alisema: “Mulipokea bure, mutoe bure.” (Mt. 10:8) Kwa hiyo, kama tunajitoa kabisa mu kazi ya Yehova na kutoa mali yetu, tutapata furaha kubwa.​—Mdo. 20:35.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine