Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ypq ulizo 7 uku. 21-23
  • Nifanye Nini Wakinikaza Kufanya Kitendo cha Ndoa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Nifanye Nini Wakinikaza Kufanya Kitendo cha Ndoa?
  • Majibu ya Maulizo 10 Yenye Vijana Wanajiulizaka
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ngono ya Kinywa, Nayo Ni Ngono?
    Vijana Wanauliza
  • Wafundishe Watoto Wako Maadili Mema
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Majibu ya Maulizo 10 Yenye Vijana Wanajiulizaka
ypq ulizo 7 uku. 21-23
Kijana mwanamuke anakataa kabisa wakati kijana mwanaume anamuomba wafanye kitendo cha ndoa

ULIZO LA 7

Nifanye Nini Wakinikaza Kufanya Kitendo cha Ndoa?

SABABU GANI ULIZO HILO NI LA MAANA?

Maamuzi yenye unakamata kuhusu kitendo cha ndoa yatakuwa na matokeo makubwa juu yako wakati wenye kuja..

UNGEFANYA NINI?

Wazia jambo hili: Heather amekuwa anaonana na Mike kwa miezi mbili tu, lakini anajisikia kuwa anamujua tangu zamani. Kila mara wanaandikiana ujumbe, wanazungumuza sana kupitia telefone, na wakati fulani mumoja anaweza kujua mwenzake anataka kusema nini mbele amalize kusema! Lakini sasa, Mike hapendi mambo yaishie pale.

Kwa muda wa miezi mbili yenye imepita, Mike na Heather hawakufanya jambo lingine isipokuwa tu kukamatana mikono na kupatiana busu (baiser). Heather hapendi kufanya zaidi ya hayo. Lakini hapendi pia kumupoteza Mike. Ni Mike tu ndiye anamufanya ajisikie kuwa mwenye sura ya muzuri sana, na wa maana sana. Anajiambia, ‘Tena, mimi na Mike tunapendana . . .’

Kama ungekuwa katika hali ya Heather na kuwa na miaka ya kuanza urafiki wa kimapenzi, ungefanya nini?

WAZA KIDOGO!

Nguo ya muzuri inatumiwa ili kupanguza uchafu

Kitendo cha ndoa ni zawadi yenye Mungu anapatia tu wale wenye wameoana. Kufanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa, ni kuharibisha zawadi hiyo. Ni kama kukamata nguo ya muzuri yenye wamekupatia na kuitumia ili kupanguza uchafu

Kama unakataa kuheshimu sheria ya uvutano (pésanteur), kwa mufano unaamua kuruka kama ndege wakati uko kwenye muti murefu, utapata matokeo ya mubaya. Ni vile pia kama unakataa kuheshimu sheria ya mwenendo safi, kama sheria hii yenye kusema, ‘Mujiepushe na uasherati.’—1 Wathesalonike 4:3.

Kuna matokeo gani ya kukosa kuheshimu amri hiyo? Biblia inasema hivi: ‘Yeye aliye na mazoea ya kufanya uasherati anautendea zambi mwili wake mwenyewe.’ (1 Wakorintho 6:18) Jambo hilo ni la kweli?

Wachunguzi wametambua kwamba vijana wengi wenye walifanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa, mara nyingi wanapata matokeo fulani kati ya matokeo yenye kufuata.

  • HUZUNI. Vijana wengi wenye walifanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa walihuzunika kisha kufanya hivyo.

  • KUKOSA KUTUMAINIANA. Kisha tu kufanya uasherati, kila mumoja anaanza kujiuliza, ‘Ni nani mwengine amekwisha kufanya naye uasherati?’

  • KUONA MAMBO KWA NJIA TOFAUTI. Vijana wengi wanawake wanafurahia mutu mwenye atawalinda, kuliko mutu mwenye atawatumia ili kupata faida yake. Na vijana wengi wanaume hawavutiwe sana na mwanamuke mwenye aliitika kulala nao.

  • Jambo la maana: Kama unafanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa, unajishushia heshima kwa kuzarau kitu cha maana sana. (Waroma 1:24) Mwili wako ni wa maana sana, haupaswe kucheza nao ovyoovyo!

Uonyeshe kama uko na nguvu ya ‘kujiepusha na uasherati.’ (1 Wathesalonike 4:3) Kisha, wakati utafunga ndoa, unaweza sasa kufanya kitendo cha ndoa. Na utafurahia kabisa kufanya kitendo hicho, bila kuogopa, bila huzuni, na wasiwasi yenye kuwa kati ya mambo yenye watu wanapata kwa sababu ya kufanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa.—Methali 7:22, 23; 1 Wakorintho 7:3.

UNAWAZA NAMNA GANI?

  • Mutu mwenye anakupenda kabisa, anaweza kukuletea huzuni ao kukutendea mubaya kimwili?

  • Mutu mwenye anakupenda kabisa, anaweza kutia urafiki wako pamoja na Mungu katika hatari?—Waebrania 13:4.

KWA VIJANA WANAWAKE TU

Kijana mwanamuke anakaa na kufikiri

Vijana wengi wanaume wanasema kama hawawezi kuoa mwanamuke mwenye wamekwisha kufanya naye kitendo cha ndoa. Sababu gani? Kwa sababu wanafurahia mwanamuke mwenye kuwa bikira!

Jambo hilo linakushangaza ao pengine kukukasirisha? Kumbuka jambo hili: Mara nyingi filme na televizyo vinatapa sana kufanya uasherati kati ya vijana. Vinaonyesha pia kwamba ni tendo la muzuri la kujifurahisha na kwamba ni alama ya upendo wa kweli.

Lakini usidanganyike! Watu wenye wanakuchochea ufanye nao kitendo cha ndoa mbele ya kuolewa, wanatafuta tu faida yao wenyewe.—1 Wakorintho 13:4, 5.

KWA VIJANA WANAUME TU

Kijana mwanaume anakaa na kufikiri

Kama unafanya urafiki wa kimapenzi, ujiulize, ‘Ninamupenda kabisa rafiki yangu mwanamuke?’ Kama jibu lako ni ndiyo, namna gani unaweza kuonyesha kwa njia yenye kufaa kama unamupenda? Kwa kufanya nguvu ili kuheshimu sheria za Mungu, kwa kuwa na hekima ya kuepuka hali zenye kuleta majaribu, na kwa kuwa na upendo wenye kutafuta faida ya watu wengine.

Kama uko na sifa hizo, rafiki yako mwanamuke atajisikia kama mwanamuke Mushulami mwenye alikuwa na mwenendo safi. Alisema hivi: ‘Mupenzi wangu ni wangu nami ni wake.’ (Wimbo wa Sulemani 2:16) Kwa kifupi, atakupenda hata zaidi!

SHAURI

Kama mutu fulani anakuchochea mufanye naye kitendo cha ndoa kwa kusema, “Kama unanipenda, hauwezi kukataa tulale pamoja,” na wewe umuambie waziwazi, “Kama unanipenda, hauwezi kuniomba jambo hilo!”

Wakati unataka kufanya jambo fulani pamoja na mwanaume ao mwanamuke, shauri la muzuri ni hili: Kama ni jambo lenye haupendi wazazi wako waone, unapaswa kuepuka kulifanya.

MAMBO NINAPANGA KUFANYA

  • Utafanya nini wakati mutu fulani anakuomba mufanye naye uasherati?

  • Ni hali gani zinaweza kufanya ikuwe nguvu kwako kukataa?

  • Namna gani unaweza kuepuka hali hizo?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine