ULIZO LA 7
Nifanye Nini Wakinikaza Kufanya Kitendo cha Ndoa?
UNGEFANYA NINI?
Wazia jambo hili: Heather amekuwa anaonana na Mike kwa miezi mbili tu, lakini anajisikia kuwa anamujua tangu zamani. Kila mara wanaandikiana ujumbe, wanazungumuza sana kupitia telefone, na wakati fulani mumoja anaweza kujua mwenzake anataka kusema nini mbele amalize kusema! Lakini sasa, Mike hapendi mambo yaishie pale.
Kwa muda wa miezi mbili yenye imepita, Mike na Heather hawakufanya jambo lingine isipokuwa tu kukamatana mikono na kupatiana busu (baiser). Heather hapendi kufanya zaidi ya hayo. Lakini hapendi pia kumupoteza Mike. Ni Mike tu ndiye anamufanya ajisikie kuwa mwenye sura ya muzuri sana, na wa maana sana. Anajiambia, ‘Tena, mimi na Mike tunapendana . . .’
Kama ungekuwa katika hali ya Heather na kuwa na miaka ya kuanza urafiki wa kimapenzi, ungefanya nini?
WAZA KIDOGO!
Kitendo cha ndoa ni zawadi yenye Mungu anapatia tu wale wenye wameoana. Kufanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa, ni kuharibisha zawadi hiyo. Ni kama kukamata nguo ya muzuri yenye wamekupatia na kuitumia ili kupanguza uchafu
Kama unakataa kuheshimu sheria ya uvutano (pésanteur), kwa mufano unaamua kuruka kama ndege wakati uko kwenye muti murefu, utapata matokeo ya mubaya. Ni vile pia kama unakataa kuheshimu sheria ya mwenendo safi, kama sheria hii yenye kusema, ‘Mujiepushe na uasherati.’—1 Wathesalonike 4:3.
Kuna matokeo gani ya kukosa kuheshimu amri hiyo? Biblia inasema hivi: ‘Yeye aliye na mazoea ya kufanya uasherati anautendea zambi mwili wake mwenyewe.’ (1 Wakorintho 6:18) Jambo hilo ni la kweli?
Wachunguzi wametambua kwamba vijana wengi wenye walifanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa, mara nyingi wanapata matokeo fulani kati ya matokeo yenye kufuata.
HUZUNI. Vijana wengi wenye walifanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa walihuzunika kisha kufanya hivyo.
KUKOSA KUTUMAINIANA. Kisha tu kufanya uasherati, kila mumoja anaanza kujiuliza, ‘Ni nani mwengine amekwisha kufanya naye uasherati?’
KUONA MAMBO KWA NJIA TOFAUTI. Vijana wengi wanawake wanafurahia mutu mwenye atawalinda, kuliko mutu mwenye atawatumia ili kupata faida yake. Na vijana wengi wanaume hawavutiwe sana na mwanamuke mwenye aliitika kulala nao.
Jambo la maana: Kama unafanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa, unajishushia heshima kwa kuzarau kitu cha maana sana. (Waroma 1:24) Mwili wako ni wa maana sana, haupaswe kucheza nao ovyoovyo!
Uonyeshe kama uko na nguvu ya ‘kujiepusha na uasherati.’ (1 Wathesalonike 4:3) Kisha, wakati utafunga ndoa, unaweza sasa kufanya kitendo cha ndoa. Na utafurahia kabisa kufanya kitendo hicho, bila kuogopa, bila huzuni, na wasiwasi yenye kuwa kati ya mambo yenye watu wanapata kwa sababu ya kufanya kitendo cha ndoa mbele ya kuoa ao kuolewa.—Methali 7:22, 23; 1 Wakorintho 7:3.
UNAWAZA NAMNA GANI?
Mutu mwenye anakupenda kabisa, anaweza kukuletea huzuni ao kukutendea mubaya kimwili?
Mutu mwenye anakupenda kabisa, anaweza kutia urafiki wako pamoja na Mungu katika hatari?—Waebrania 13:4.