Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 4 uku. 16-uku. 17 fu. 2
  • Aliua Mudogo Wake Juu ya Kasirani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Aliua Mudogo Wake Juu ya Kasirani
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”
    Tuige Imani Yao
  • “Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Mungu Alikubali” Zawadi Zao
    Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 4 uku. 16-uku. 17 fu. 2
Kaini anakasirika wakati Abeli anamutolea Yehova zabihu

4

Aliua Mudogo Yake kwa Sababu ya Kasirani

Kisha kutoka mu bustani, Adamu na Eva walizaa watoto wengi. Mutoto wao wa kwanza aliitwa Kaini, alikuwa mulimaji, na mutoto wao wa pili aliitwa Abeli, alikuwa muchungaji.

Siku moja Kaini na Abeli walimutolea Yehova zabihu. Unajua zabihu ni nini? Ni zawadi ya pekee yenye mutu anatolea Mungu. Yehova alifurahia zabihu ya Abeli, lakini hakufurahia zabihu ya Kaini. Kaini alikasirika sana. Yehova alimuambia Kaini kama, kasirani ingemusukuma afanye jambo la mubaya. Lakini, Kaini hakusikiliza.

Kuliko kusikiliza, Kaini alimuambia Abeli hivi: ‘Tuende kwenye shamba.’ Wakati walikuwa wao wawili tu mu shamba, Kaini alipiga ndugu yake na kumuua. Yehova alifanya nini? Yehova alipatia Kaini malipizi kwa kumufukuza aende mbali na familia yake. Yehova hakukubali Kaini arudie kwao.

Kaini anamukaribia Abeli mu shamba

Ile inatufundisha nini? Tunaweza kukasirika kwa sababu mambo haikuwe vile tulipenda. Tukiona kama tunaanza kukasirika ao mutu mwingine anatushauria juu ya tabia yetu ya kukasirika, tunapaswa kubadilika bila kukawia na kujikaza kutulia.

Kwa sababu Abeli alimupenda Yehova na alifanya mambo ya muzuri, Yehova angali anamukumbuka. Mungu atafufua Abeli wakati atafanya hii dunia ikuwe paradiso.

“Fanya kwanza amani na ndugu yako, na kisha urudie na utoe zawadi yako.”​—Matayo 5:24

Maulizo: Taja majina ya watoto wawili wa kwanza wa Adamu na Eva, na kazi yenye walikuwa wanafanya. Juu ya nini Kaini aliua ndugu yake?

Mwanzo 4:1-12; Waebrania 11:4; 1 Yohana 3:11, 12

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine