Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 8 uku. 26-uku. 27 fu. 1
  • Abrahamu na Sara Walimutii Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Abrahamu na Sara Walimutii Mungu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Abrahamu Alikuwa Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yehova Alimuita “Rafiki Yangu”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Uko Unangojea “Muji Wenye Uko na Misingi ya Kweli”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Abrahamu—Mwanamume Mwenye Upendo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 8 uku. 26-uku. 27 fu. 1
Abrahamu na Sara wanafunga mizigo yao ili kutoka Uru

8

Abrahamu na Sara Walimutii Mungu

Muji wa Uru ulikuwa karibu na muji wa Babeli. Watu wa Uru waliabudu miungu mingi kuliko kumuabudu Yehova. Lakini kulikuwa mwanaume mumoja mwenye aliishi mu muji wa Uru, mwenye alimuabudu Yehova tu. Aliitwa Abrahamu.

Yehova alimuambia Abrahamu hivi: ‘Utoke mu inchi yako na uache watu wa jamaa yako, uende mu inchi yenye nitakuonyesha.’ Kisha Mungu alimupatia hii ahadi: ‘Nitakufanya ukuwe taifa kubwa, nitafanyia watu mambo ya muzuri mu dunia yote kwa sababu yako.’

Abrahamu hakujua kwenye Yehova alimuambia aende, lakini alimutumainia. Kwa hiyo Abrahamu, bibi yake Sara, baba yake Tera, na Loti, mutoto wa kaka yake, walitii, wakafunga mizigo na kuanza safari ya murefu.

Abrahamu alikuwa na miaka 75, wakati yeye na familia yake walifika mu inchi yenye Yehova alipenda kuwaonyesha. Ile inchi iliitwa Kanaani. Kule, Mungu alisema na Abrahamu na akamuambia hivi: ‘Nitapatia watoto wako hii inchi.’ Lakini Abrahamu na Sara walikuwa wazee na hawakukuwa na watoto. Basi, Yehova angetimiza ile maneno namna gani?

Abrahamu na familia yake wanaenda Kanaani

“Kwa imani, Abrahamu . . . alitii kwa kutoka na kuenda mahali kwenye angepokea kuwa uriti; alitoka, hata kama hakujua mahali alikuwa anaenda.”​—Waebrania 11:8

Maulizo: Yehova aliambia Abrahamu afanye nini? Yehova alisema atafanyia Abrahamu nini?

Mwanzo 11:29–12:9; Matendo 7:2-4; Wagalatia 3:6; Waebrania 11:8

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine