Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 33 uku. 82-uku. 83 fu. 2
  • Rutu na Naomi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Rutu na Naomi
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Mahali Wewe Unapoenda, Nitaenda’
    Tuige Imani Yao
  • ‘Mahali Wewe Unapokuenda, Nitakuenda’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • ‘Mwanamuke Mwema Sana’
    Tuige Imani Yao
  • ‘Mwanamuke Bora Sana’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 33 uku. 82-uku. 83 fu. 2
Naomi anaambia Rutu arudie kwao

33

Rutu na Naomi

Wakati kulikuwa njaa mu inchi ya Israeli, mwanamuke Mwisraeli mwenye kuitwa Naomi alihamia Moabu na bwana yake na watoto wake wanaume wawili. Kisha, bwana ya Naomi akakufa. Mutoto wake mumoja alioa Rutu, na mwingine alioa Orpa, wanamuke Wamoabu. Lakini, kisha wakati fulani watoto wa Naomi walikufa.

Wakati Naomi alipata habari kama njaa ilikuwa imeisha mu inchi ya Israeli, aliamua kurudia. Rutu na Orpa walienda pamoja naye, lakini, wakati walikuwa mu njia, Naomi aliwaambia hivi: ‘Mulikuwa bibi wazuri kwa watoto wangu na mulikuwa wakwe wazuri kwangu. Ninapenda muolewe tena. Murudie Moabu.’ Wakamuambia: ‘Tunakupenda sana! Hatupendi kukuacha.’ Naomi akaendelea kuwabembeleza warudie. Kisha, Orpa akarudia, lakini Rutu akabakia. Naomi akamuambia: ‘Orpa anarudia kwa watu wake na kwa miungu yake. Rudia naye, na uende ku nyumba ya mama yako.’ Lakini, Rutu akamuambia: ‘Sitakuacha. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako Mungu wangu.’ Unawaza Naomi alijisikia namna gani wakati Rutu alimuambia vile?

Rutu na Naomi walifika Israeli mwanzo wa mavuno ya mbegu ya shayiri (orge). Siku moja, Rutu alienda kuokota mbegu ya shayiri mu shamba la mwanaume mwenye kuitwa Boazi, mwenye alikuwa mutoto wa Rahabu. Boazi alipata habari kama Rutu alikuwa Mumoabu mwenye alikataa kabisa kuachana na Naomi. Aliambia wafanyakazi wake waache mbegu fulani mu shamba juu Rutu aziokote.

Rutu anakusanya mbegu mu shamba ya Boazi

Mangaribi, Naomi aliuliza Rutu: ‘Leo ulifanya kazi mu shamba la nani?’ Rutu akamujibia: ‘Mu shambala Boazi.’ Naomi akamuambia: ‘Boazi ni mutu wa jamaa ya bwana yangu. Uendelee kufanya kazi mu shamba lake pamoja na wanamuke wengine. Pale hakuna mutu mwenye atakusumbua.’

Naomi pamoja na Boazi, Rutu, na Obedi

Rutu aliendelea kufanya kazi mu shamba la Boazi mupaka wakati kazi ya kuvuna iliisha. Boazi alitambua kama Rutu ni mwanamuke muzuri na mwenye bidii. Ile wakati, kama mwanaume anakufa bila kuzaa watoto, mutu wa jamaa yake alipaswa kuoa bibi yake. Basi, Boazi alioa Rutu. Wakazaa mutoto mwenye aliitwa Obedi, mwenye alifikia kuwa tate (nkambo) wa Mufalme Daudi. Marafiki wa Naomi walifurahi sana. Walimuambia: ‘Kwanza, Yehova alikupatia Rutu mwenye anakupenda sana, na sasa uko na mujukuu. Yehova asifiwe.’

“Kuko rafiki mwenye anashikamana sana na mutu kuliko ndugu.”​—Mezali 18:24

Maulizo: Rutu alifanya nini yenye ilionyesha kama alipenda Naomi? Namna gani Yehova alihangaikia Rutu na Naomi?

Rutu 1:1–4:22; Matayo 1:5

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine