Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 42 uku. 102-uku. 103 fu. 3
  • Yonatani Alikuwa Hodari na Mushikamanifu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yonatani Alikuwa Hodari na Mushikamanifu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ubakie Muaminifu kwa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Muendelee Kuonyesha Upendo Wenye Upole
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Penda Watu Ambao Mungu Anapenda
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 42 uku. 102-uku. 103 fu. 3
Yonatani na mubeba-silaha wake

42

Yonatani Alikuwa Hodari na Mushikamanifu

Yonatani, mutoto wa kwanza wa Sauli, alikuwa mupiganaji-vita mwenye kuwa hodari. Daudi alisema kama Yonatani alikuwa anakimbia sana kupita tai na alikuwa na nguvu kupita simba. Siku moja, Yonatani aliona maaskari Wafilisti 20 ku mulima. Akaambia mubeba-silaha wake: ‘Tutapigana nao kama tu Yehova anatupatia alama. Kama Wafilisti wanatuambia tuende kwenye wako, ile itakuwa alama ya kuonyesha kama tunapaswa kupigana nao.’ Wafilisti wakasema hivi kwa sauti: ‘Mukuje tupigane!’ Palepale, Yonatani na mubeba-silaha wake wakapanda ku ile mulima na wakashinda wale maaskari.

Yonatani anamupatia Daudi vitu fulani

Juu Yonatani njo alikuwa mutoto mukubwa wa Sauli, yeye njo alipaswa kuwa mufalme kisha baba yake. Lakini Yonatani alijua kama Yehova alikuwa amechagua Daudi akuwe mufalme wa Israeli kisha baba yake. Yonatani hakusikilia Daudi wivu. Yonatani na Daudi wakakuwa marafiki wa sana. Walifanya mapatano kama kila mumoja atalinda na kupigania mwenzake. Yonatani alipatia Daudi koti yake, upanga wake, upinde wake, na mukaba wake kuwa alama ya urafiki wao.

Wakati Daudi alikuwa anamukimbia Sauli, Yonatani alienda kuonana na Daudi na akamuambia: ‘Usiogope, ukuwe hodari. Yehova amekuchagua ukuwe mufalme. Na hata baba yangu anajua vile.’ Je, ungependa kuwa na rafiki muzuri sawa Yonatani?

Mara mingi Yonatani alitia maisha yake mu hatari juu asaidie rafiki yake. Alijua kama Mufalme Sauli alitaka kuua Daudi, kwa hiyo aliambia baba yake: ‘Daudi hana kosa, kama unamuua utakuwa umefanya zambi.’ Sauli alikasirikia sana Yonatani. Kisha miaka fulani, Sauli na Yonatani wakakufa ku vita.

Kisha Yonatani kufa, Daudi alitafuta Mefibosheti, mutoto wa Yonatani. Wakati Daudi alimupata, alimuambia: ‘Juu baba yako alikuwaka rafiki yangu sana, nitakutunza maisha yako yote. Utaishi mu nyumba yangu ya kifalme na utakuwa unakula ku meza yangu.’ Daudi hakusahau hata kidogo rafiki yake Yonatani.

“Mupendane kama vile niliwapenda ninyi. Hakuna mwenye iko na upendo mukubwa kuliko huu, kwamba mutu atoe uzima wake kwa ajili ya marafiki wake.”—Yohana 15:12, 13

Maulizo: Namna gani Yonatani alionyesha kama alikuwa hodari? Namna gani Yonatani alionyesha kama alikuwa mushikamanifu?

1 Samweli 14:1-23; 18:1-4; 19:1-6; 20:32-42; 23:16-18; 31:1-7; 2 Samweli 1:23; 9:1-13

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine