Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 46 uku. 112-uku. 113 fu. 1
  • Mambo Yenye Ilifanyika Kwenye Mulima Karmeli

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo Yenye Ilifanyika Kwenye Mulima Karmeli
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Alitetea Ibada Safi
    Tuige Imani Yao
  • Alikesha, na pia Alingojea
    Tuige Imani Yao
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Je, Kuna Wakati Unapojihisi Mpweke na Mwenye Woga?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 46 uku. 112-uku. 113 fu. 1
Yehova anatuma moto na inachoma zabihu ya Eliya

46

Mambo Yenye Ilifanyika Kwenye Mulima Karmeli

Ufalme wa Israeli wa makabila kumi ulitawaliwa na wafalme wengi wabaya. Ahabu alikuwa mumoja kati ya wafalme wabaya sana. Alioa mwanamuke muovu mwenye aliabudu Baali. Jina lake lilikuwa Yezebeli. Ahabu na Yezebeli walieneza ibada ya Baali mu inchi yote na waliua manabii wa Yehova. Yehova alifanya nini? Alituma nabii Eliya aambie Ahabu jambo fulani.

Eliya aliambia Mufalme Ahabu kama juu iko anafanya mambo ya mubaya, mvua haitanyesha katika Israeli. Kwa zaidi ya miaka tatu, chakula haikukomaa na watu waliteseka na njaa. Kisha, Yehova alituma tena Eliya kwa Ahabu. Ahabu alimuambia: ‘Wewe njo umetuletea taabu! Ni sababu yako njo maana tunateseka.’ Eliya akajibu: ‘Haiko mimi njo nilifanya mvua isinyeshe. Ni wewe njo uko na makosa juu uko unaabudu Baali. Tutafanya jambo fulani juu tuone kama nani njo Mungu wa kweli. Ambia watu wote na manabii wote wa Baali wakusanyike kwenye Mulima Karmeli.’

Watu wakakusanyika ku ule mulima. Eliya akasema: ‘Muchague. Kama Yehova njo Mungu wa kweli, mumufuate. Kama Baali njo Mungu wa kweli, basi mumufuate. Tufanye hivi: Manabii 450 wa Baali watayarishe toleo na waite mungu wao, na mimi nitatayarisha toleo na kumuita Yehova. Mwenye atajibu kwa kutuma moto njo Mungu wa kweli.’ Watu wakakubali.

Manabii wa Baali wakatayarisha toleo lao. Kuanzia asubui mupaka mangaribi walikuwa wanaita mungu wao: ‘Ee Baali, utujibie!’ Juu Baali hakuwajibia, Eliya alianza kumucheka. Alisema: ‘Mumuite na sauti yenu yote. Pengine alishalala, na inaomba mutu amuamushe.’ Manabii wa Baali waliendelea kumuita mupaka mangaribi. Lakini Baali hakuwajibia.

Eliya akatia toleo lake ku mazabahu na kulimwangia maji. Kisha akasali: ‘Ee Yehova, tafazali unijibie ili watu hawa wajue kama wewe njo Mungu wa kweli.’ Mara moja Yehova akashusha moto kutoka mbinguni na ikachoma ile toleo. Watu wakasema hivi kwa sauti: ‘Yehova njo Mungu wa kweli!’ Kisha, Eliya akasema: ‘Musiache manabii wa Baali wakimbie!’ Ile siku, manabii 450 wa Baali waliuawa.

Wakati wingu la kidogo lilionekana juu ya bahari, Eliya akaambia Ahabu: ‘Mvua kubwa itanyesha. Panda katika gari yako, na uende kwako.’ Anga ikakuwa mweusi, kukakuwa giza, upepo, na mvua kubwa ikaanza kunyesha. Ku mwisho, ukame ukaisha. Ahabu akaendesha gari lake mbio sana. Lakini Yehova akasaidia Eliya. Eliya akakimbia mbio kupita lile gari! Lakini je, magumu yote ya Eliya ilikuwa imeisha? Tuone basi.

“Wajue kwamba wewe, mwenye jina lako ni Yehova, Wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”—Zaburi 83:18

Maulizo: Ni mambo gani yenye ilifanyika ku mulima Karmeli? Namna gani Yehova alijibia sala ya Eliya?

1 Wafalme 16:29-33; 17:1; 18:1, 2, 17-46; Yakobo 5:16-18

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine