Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 51 uku. 124-uku. 125 fu. 2
  • Mupiganaji-vita na Mutoto Mudogo Mwanamuke

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mupiganaji-vita na Mutoto Mudogo Mwanamuke
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Alionyesha Kiburi na Kisha Akatii
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Gehazi Alipata Matatizo kwa Sababu ya Tamaa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 51 uku. 124-uku. 125 fu. 2
Naamani anatembelea Elisha juu apone

51

Mupiganaji-vita na Mutoto Mudogo Mwanamuke

Mutoto mumoja mwanamuke Mwisraeli alikuwa anaishi Siria, mbali na kwao. Maaskari wa Siria njo walimukamataka na kuenda naye. Sasa alikuwa anatumikia bibi ya Naamani, mukubwa wa jeshi. Ule mutoto alikuwa anamuabudu Yehova, hata kama watu wenye aliishi nao hawakukuwa wanamuabudu Yehova.

Naamani alikuwa na ukoma (ugonjwa mubaya sana wa ngozi), na alikuwa anasikia maumivu saa yote. Ule mutoto mwanamuke alipenda sana kumusaidia. Aliambia bibi ya Naamani hivi: ‘Ninajua mutu mwenye anaweza kuponyesha bwana yako. Ni nabii wa Yehova. Jina lake Elisha na anaishi katika inchi ya Israeli.’

Bibi ya Naamani alielezea bwana yake mambo yenye ule mutoto alimuambia. Naamani alikuwa tayari kufanya kila kitu juu apone. Kwa hiyo alienda mu inchi ya Israeli juu aonane na Elisha. Aliwaza kama Elisha atamupokea sawa mutu wa maana sana. Lakini kuliko kuzungumuza naye uso kwa uso, Elisha alituma mutumishi wake amupokee na amuambie hivi: ‘Uende unawe mara saba katika Muto Yordani. Kisha, utapona.’

Naamani alihuzunika sana. Alisema: ‘Niliwaza ule nabii ataniponyesha kwa kumuomba Mungu wake na kupitisha-pitisha mikono yake kwenye ngozi yangu. Lakini, ananiambia niende ninawe katika huu muto wa Israeli. Kule Siria kuko mito ya muzuri sana kupita ule muto wa Israeli. Juu ya nini nisiende kunawia kule?’ Naamani alikasirika sana, na akatoka ku nyumba ya Elisha.

Naamani ananawa mu Muto Yordani na anapona

Watumishi wa Naamani walizungumuza naye. Walimuambia: ‘Hauko tayari kufanya kila kitu ili upone? Mambo yenye nabii anasema ufanye haiko nguvu. Juu ya nini unakataa?’ Naamani aliwasikiliza. Akaenda ku Muto Yordani na kujitumbukiza ndani mara saba. Kisha kujitumbukiza mara ya saba, Naamani akatoka mu maji, na ukoma wake ulikuwa umeisha kabisa. Alifurahi sana, akarudia kwa Elisha juu amushukuru. Akaambia Elisha: ‘Sasa ninajua kama Yehova njo Mungu wa kweli.’ Unawaza ule mutoto mwanamuke Mwisraeli alijisikia namna gani wakati Naamani alirudia na alishapona?

“Kutoka katika kinywa cha watoto wadogo na watoto wenye kunyonya umetokeza sifa.”​—Matayo 21:16

Maulizo: Unawaza ilikuwa mwepesi kwa ule mutoto mudogo Mwisraeli kuzungumuza na bibi ya Naamani? Unawaza nini njo ilimusaidia ule mutoto mudogo Mwisraeli akuwe na uhodari?

2 Wafalme 5:1-19; Luka 4:27

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine