67
Kuta za Yerusalemu
Turudie nyuma miaka fulani. Nehemia, alikuwa Mwisraeli mwenye alikuwa anaishi katika muji wa Shushani, wenye ulikuwa mu eneo la Uajemi. Alikuwa mutumishi wa Mufalme Artashasta. Ndugu yake alitoka Yuda na kumuletea hii habari ya mubaya: ‘Wayahudi wenye walirudia Yerusalemu hawako katika usalama. Milango mikubwa na kuta za muji, zenye Wababiloni waliharibu, hazijajengwa.’ Nehemia alihuzunika sana. Alitaka kuenda Yerusalemu ili awasaidie. Kwa hiyo, alisali kwa Yehova ili mufalme amupatie ruhusa ya kuenda.
Kisha, mufalme aliona kama Nehemia hakukuwa na furaha. Akamuambia: ‘Sijakuonaka hivi. Nini njo iko inakusumbua?’ Nehemia akamuambia: ‘Juu ya nini nisihuzunike? Muji wetu, Yerusalemu, umebakia mabomoko.’ Mufalme akamuuliza: ‘Unapenda nikufanyie nini?’ Palepale, Nehemia akasali kimya-kimya. Kisha akamuambia: ‘Tafazali, uniruhusu niende kujenga upya kuta za Yerusalemu.’ Mufalme akaruhusu Nehemia aende, na akafanya mipango ili Nehemia afanye ile safari ya murefu mu usalama. Pia, akafanya Nehemia kuwa gavana wa Yuda. Na akamupatia miti yenye atatengeneza nayo milango mikubwa ya muji.
Wakati Nehemia alifika Yerusalemu, alichunguza kuta za muji. Kisha akakusanya makuhani na viongozi na kuwaambia: ‘Kuta zimeharibika sana. Tunapaswa kuanza kazi.’ Watu wakaitika, na wakaanza kujenga upya kuta za muji.
Lakini maadui fulani wa Waisraeli waliwacheka. Walikuwa wanasema: ‘Hata mbweha anaweza kubomoa ukuta wenye muko munajenga.’ Wafanyakazi hawakuacha ile maneno iwazuie kuendelea kujenga. Basi, ukuta ukaendelea kuwa murefu na kuwa nguvu sana.
Kwa hiyo, maadui walipanga kuja kupitia njia mbalimbali ili kushambulia Yerusalemu kwa kushitukia. Wakati Wayahudi walisikia juu ya mupango wa wale maadui, waliogopa. Lakini Nehemia aliwaambia: ‘Musiogope. Yehova iko pamoja na sisi.’ Kisha, akaweka walinzi ili walinde wafanyakazi, na maadui wao hawakuweza kuwashambulia.
Mu siku 52 tu, walimaliza kujenga kuta na milango mikubwa. Halafu Nehemia akakusanya Walawi wote Yerusalemu ili kutolea Yehova kuta zenye walijenga. Akawapanga mu vikundi mbili vya waimbaji. Wakapanda ku ukuta kwa kutumia vipandio vya Mulango Mukubwa wa Chemchemi, na wakaenda wamoja upande huu na wengine upande mwingine. Wakazunguka muji na wako wanamuimbia Yehova kwa tarumbeta, vinanda, na vinubi. Ezra alienda na kikundi kimoja, na Nehemia alienda na kikundi kingine. Kisha walikutana ku hekalu. Watu wote, ni kusema, wanaume, wanamuke, na watoto, walimutolea Yehova zabihu na wakafanya karamu. Sauti zao za furaha zilifika mbali sana.
“Hakuna silaha yenye itafanywa juu yako yenye itafanikiwa.”—Isaya 54:17