Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 69 uku. 164-uku. 165 fu. 2
  • Gabrieli Anatembelea Maria

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Gabrieli Anatembelea Maria
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Anapewa Heshima Mbele ya Kuzaliwa Kwake
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Tazama! Mimi Ni “Kijakazi wa Yehova!”
    Tuige Imani Yao
  • Maria Iko na Mimba Lakini Hajaolewa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Alifikiri na Kuamua Katika Moyo Wake
    Tuige Imani Yao
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 69 uku. 164-uku. 165 fu. 2
Malaika Gabrieli anamutokea Maria

69

Gabrieli Anatembelea Maria

Malaika anamutokea Yosefu mu ndoto

Katika jamaa ya Elizabeti, mulikuwa kijana mwanamuke mwenye aliitwa Maria. Maria alikuwa anaishi katika muji wa Nazareti, kule Galilaya. Alikuwa muchumba wa seremala mwenye aliitwa Yosefu. Wakati Elizabeti alikuwa na mimba ya miezi sita, malaika Gabrieli alimutokea Maria na akamuambia hivi: ‘Jambo, Maria. Yehova amekupendelea sana.’ Maria hakuelewa Gabrieli alipenda kusema nini. Kisha Gabrieli akamuambia: ‘Utapata mimba na utazaa mutoto. Utamuita Yesu. Atakuwa Mufalme na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.’

Maria akamuambia: ‘Lakini mimi sijalalaka na mwanaume. Namna gani nitazaa mutoto?’ Gabrieli akamuambia: ‘Kwa Yehova hakuna jambo lenye haliwezekane. Roho takatifu itakuja juu yako, na utazaa mutoto mwanaume. Elizabeti, mutu wa jamaa yako, naye amekuwa na mimba.’ Kisha Maria akasema: ‘Niko mutumwa wa Yehova. Ikuwe vile unasema.’

Yosefu anaoa Maria mwenye iko na mimba

Kisha, Maria akaenda kuona Elizabeti. Elizabeti alikuwa anaishi katika muji fulani wenye ulikuwa ku milima. Wakati Maria alimusalimia, mara moja Elizabeti akasikia mutoto mwenye alikuwa mu tumbo lake anaruka. Akajazwa roho takatifu na akasema: ‘Maria, Yehova amekubariki. Nimepata pendeleo kubwa sana kwa sababu mama ya Masiya amefika katika nyumba yangu.’ Maria akajibu: ‘Ninamusifu Yehova kwa moyo wangu wote.’ Maria akabakia miezi tatu kwa Elizabeti, kisha akarudia Nazareti, kwenye alikuwa anaishi.

Wakati Yosefu alipata habari kama Maria alikuwa na mimba, alipenda waachane. Lakini malaika akamutokea mu ndoto na kumuambia: ‘Usiogope kumuoa. Hakufanya kosa hata kidogo.’ Basi, Yosefu akaoa Maria na akamupeleka mu nyumba yake.

“Yehova anafanya kila kitu chenye anapenda kufanya katika mbingu na juu ya dunia.”​—Zaburi 135:6

Maulizo: Gabrieli aliambia Maria nini kuhusu mutoto mwenye angezaa? Elizabeti na Maria walijisikia namna gani kuhusu mambo yenye iliwafikia?

Matayo 1:18-25; Luka 1:26-56; Isaya 7:14; 9:7; Danieli 2:44; Wagalatia 4:4

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine