Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 76 uku. 180-uku. 181 fu. 2
  • Yesu Anasafisha Hekalu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anasafisha Hekalu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Anaonyesha Bidii kwa Ajili ya Ibada ya Kweli
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Anasafisha Tena Hekalu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Je, Wajua?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 76 uku. 180-uku. 181 fu. 2
Yesu anatumia fimbo ya kamba ili kufukuza wanyama inje ya hekalu na anapindua meza za wenye wako wanabadilisha feza

76

Yesu Anasafisha Hekalu

Yesu alienda Yerusalemu katika Mwezi wa 4 hivi mu mwaka wa 30. Watu mingi walikuwa wamekuja Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka. Walikuwa wanatoa zabihu za wanyama ku hekalu, kama vile walizoea kufanya. Wamoja walikuja na wanyama wao, lakini wengine waliuza wanyama pale Yerusalemu.

Wakati Yesu alifika ku hekalu, aliona wafanyabiashara wako wanauzisha wanyama ndani ya hekalu. Walikuwa wanafanya biashara mu nyumba ya Yehova ya ibada! Yesu alifanya nini? Alitengeneza mujeledi wa kamba (fimbo ya kamba) na alifukuza kondoo na ngombe zenye zilikuwa mu hekalu. Alipindua meza za watu wenye walikuwa wanabadilisha feza na akamwanga chini feza zao za vichele. Yesu aliambia wale wenye walikuwa wanauzisha njiwa: ‘Mutoshe hivi vitu hapa! Muache kufanya nyumba ya Baba yangu kuwa nafasi ya biashara!’

Watu wenye walikuwa ku hekalu walishangaa kuona mambo yenye Yesu alifanya. Wanafunzi wake walikumbuka unabii fulani juu ya Masiya wenye unasema hivi: ‘Nitakuwa na bidii sana kwa ajili ya nyumba ya Yehova.’

Kisha wakati fulani, mu mwaka wa 33, Yesu alisafisha hekalu mara ya pili. Hakuruhusu mutu yeyote azarau nyumba ya Baba yake.

“Hamuwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.”​—Luka 16:13

Maulizo: Yesu alifanya nini wakati aliona watu wako wanauzisha wanyama ku hekalu? Juu ya nini Yesu alifanya vile?

Matayo 21:12, 13; Marko 11:15-17; Luka 19:45, 46; Yohana 2:13-17; Zaburi 69:9

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine