80
Yesu Anachagua Mitume 12
Kisha kuhubiri kwa karibu mwaka moja na nusu, Yesu alipaswa kufanya uamuzi wa maana sana. Angechagua nani ili watumike naye? Angezoeza nani ili waongoze kutaniko la Kikristo? Ili kukamata ile maamuzi, Yesu alipenda Yehova amuongoze. Kwa hiyo, alienda ku mulima ili akuwe peke yake, na alisali usiku wote. Wakati ilikuwa asubui, aliita wanafunzi wake fulani na kuchagua kati yao mitume 12. Unakumbuka majina yao? Kulikuwa Petro, Andrea, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartolomayo, Tomasi, Matayo, Yakobo (mwana wa Alfayo), Tadayo, Simoni, na Yuda Iskariote.
Andrea, Petro, Filipo, Yakobo
Wale mitume 12 njo walikuwa wanatembea pamoja na Yesu. Kisha kuwazoeza, aliwatuma waende kuhubiri peke yao. Yehova aliwapatia uwezo wa kufukuza pepo wachafu na kuponyesha wagonjwa.
Yohana, Matayo, Bartolomayo, Tomasi
Yesu aliita wale Mitume 12 marafiki wake, na aliwatumainia. Wafarisayo walikuwa wanaona kama mitume walikuwa watu wenye hawana elimu na wa kawaida tu. Lakini Yesu alizoeza wale mitume ili wafanye kazi ya kuhubiri. Wangekuwa pamoja na Yesu wakati wa maana sana mu maisha yake. Kwa mufano walikuwa naye mbele akufe na kisha yeye kufufuliwa. Sawa vile Yesu, wengi kati ya wale mitume 12 walikuwa watu wa Galilaya. Wamoja kati yao walikuwa wameoa.
Yakobo mwana wa Alfayo, Yuda Iskariote, Tadayo, Simoni
Mitume hawakukuwa wakamilifu, walikuwa wanafanya makosa. Wakati fulani, walisema bila kuwaza na walikamata maamuzi ya mubaya. Wakati mwingine, walikosa uvumilivu. Hata walibishana juu ya kujua ni nani alikuwa wa maana sana kati yao. Lakini walikuwa watu wazuri na walimupenda Yehova. Wao njo walikuwa washiriki wa kwanza wa kutaniko la Kikristo na walisaidia sana kutaniko kisha Yesu kurudia mbinguni.
“Nimewaita ninyi marafiki, kwa sababu nimewajulisha mambo yote yenye nilisikia kutoka kwa Baba yangu.”—Yohana 15:15