Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 87 uku. 204-uku. 205 fu. 3
  • Chakula cha Mangaribi cha Mwisho cha Yesu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Chakula cha Mangaribi cha Mwisho cha Yesu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Chakula cha Mangaribi cha Bwana
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • ‘Mufanye Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Pasaka ya Mwisho ya Yesu Inakaribia
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Chakula cha Bwana​—Ukumbusho Unaomuletea Mungu Heshima
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 87 uku. 204-uku. 205 fu. 3
Yesu anaanzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana na mitume wake waaminifu kumi na moja

87

Chakula cha Mangaribi cha Mwisho cha Yesu

Kila mwaka, tarehe 14 ya mwezi wa Nisani, Wayahudi walikuwa wanafanya Pasaka. Pasaka ilikuwa inawakumbusha namna Yehova aliwatoshaka katika utumwa wa Misri na kuwaleta katika Inchi ya Ahadi. Mu mwaka wa 33, Yesu na mitume wake walifanyia Pasaka Yerusalemu, mu chumba kimoja cha juu. Wakati walimaliza kula, Yesu alisema: “Mumoja wenu atanisaliti.” Mitume walishituka na kumuuliza: ‘Ni nani?’ Yesu aliwajibu: ‘Ni ule mwenye nitapatia mukate.’ Kisha, akamupatia Yuda Iskariote mukate. Palepale Yuda akasimama na kuenda.

Kisha, Yesu akasali, akagawanya mukate vipande-vipande, na kupatia mitume wenye walikuwa pale. Akawaambia: ‘Mukule mukate huu. Unafananisha mwili wangu, wenye nitatoa kwa ajili yenu.’ Kisha, akasali kwa ajili ya divai, akaichukua na kupatia mitume wake. Akawaambia: ‘Mukunywe hii divai. Inafananisha damu yangu, yenye nitatoa ili zambi zisamehewe. Ninawatolea ahadi kwamba mutakuwa wafalme pamoja na mimi mbinguni. Mukuwe munafanya hivi kila mwaka ili kunikumbuka.’ Njo maana wanafunzi wa Yesu wanakusanyikaka mangaribi ya Nisani 14 kila mwaka. Ule mukutano njo unaitwa Chakula cha Mangaribi cha Bwana.

Kisha kula ile chakula, mitume walianza kubishana juu ya kujua ni nani njo alikuwa mukubwa kati yao. Lakini Yesu aliwaambia: ‘Ule mwenye anajiona kuwa mudogo zaidi kati yenu, njo mukubwa zaidi.’

Kisha akaongeza: ‘Ninyi muko marafiki wangu. Ninawaambia kila kitu chenye Baba yangu anapenda niwaambie. Sasa hivi nitaenda kwa Baba yangu mwenye iko mbinguni, lakini ninyi mutabakia. Watu watajua kama muko wanafunzi wangu wakati wataona namna munapendana. Munapaswa kupendana sawa vile niliwapenda.’

Ku mwisho, Yesu alimuomba Yehova awalinde wanafunzi wake wote. Alimuomba Yehova asaidie wanafunzi wake wafanye kazi kwa amani. Alisali jina la Yehova litakaswe. Kisha, Yesu na mitume wake waliimba nyimbo za kumusifu Yehova na kisha wakaenda inje. Wakati wa kumukamata Yesu ulikuwa umekaribia.

“Musiogope, kundi ndogo, kwa maana Baba yenu amekubali kuwapatia ninyi Ufalme.”​—Luka 12:32

Maulizo: Yesu alipatia mitume wake ahadi gani? Yesu alifundisha mitume mambo gani ya maana wakati alikula chakula cha mwisho pamoja nao?

Matayo 26:20-30; Luka 22:14-26; Yohana 13:1, 2, 26, 30, 34, 35; 15:12-19; 17:3-26

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine