Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 89 uku. 208-uku. 209 fu. 1
  • Petro Anamukana Yesu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Petro Anamukana Yesu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Petro Anamukana Yesu Kwenye Nyumba ya Kayafa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Anapelekwa kwa Anasi, Kisha Kwa Kayafa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Lazaro Anafufuliwa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Bwana Wake Alimufundisha Kusamehe
    Tuige Imani Yao
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 89 uku. 208-uku. 209 fu. 1
Petro anamukana Yesu mu kiwanja cha nyumba ya Kayafa

89

Petro Anamukana Yesu

Wakati Yesu alikuwa na mitume wake mu chumba cha juu, aliwaambia: ‘Ninyi wote mutaniacha usiku wa leo.’ Petro akasema: ‘Hapana mimi! Hata kama wengine wote wanakuacha, mimi sitakuacha.’ Lakini Yesu akamuambia: ‘Mbele jogoo awike, utanikana mara tatu.’

Wakati maaskari walimukamata Yesu na kumupeleka kwa Kayafa, karibu mitume wote walikuwa wamekimbia. Lakini, mitume wawili walienda pamoja na wale watu wengi wenye walimukamata Yesu. Mumoja wao alikuwa Petro. Aliingia mu kiwanja cha nyumba ya Kayafa na kuanza kuota moto. Moto uliangazia sura yake na mutumishi fulani mwanamuke akamuona na kumuambia: ‘Ninakujua! Ulikuwa pamoja na Yesu!’

Petro akamujibu: ‘Hapana, mimi sikukuwa naye. Sijue unataka kusema nini.’ Kisha, Petro akatoka na kuenda kwenye mulango mukubwa. Lakini, mutumishi mwingine mwanamuke akamuona na kuambia watu: ‘Huyu mutu alikuwa pamoja na Yesu!’ Petro akajibu: ‘Simujue hata Yesu!’ Kisha, mwanaume mwingine akasema: ‘Na wewe uko mwanafunzi wake! Namna yako ya kusema inaonyesha kama uko Mugalilaya, sawa vile Yesu.’ Lakini Petro akaapa na kusema: ‘Simujue ule mutu!’

Ile wakati, jogoo akawika. Petro akaona Yesu anageuka na kumuangalia. Halafu Petro akakumbuka maneno yenye Yesu alimuambiaka. Akaenda inje na kulia kwa uchungu.

Ile wakati, Sanhedrini (tribinali kubwa ya Wayahudi) ilikuwa imekusanyika kwa Kayafa ili kumuhukumu Yesu. Walikuwa wameamua kama watamuua Yesu, lakini walikuwa wanatafuta sababu ya kumuua. Lakini, hawakupata kosa hata moja. Ku mwisho, Kayafa akamuuliza Yesu: ‘Uko Mwana wa Mungu?’ Yesu akajibu: ‘Ndiyo.’ Kayafa akasema: ‘Hatuna tena lazima ya ushuhuda mwingine. Munaona, amemutukana Mungu!’ Tribinali yote ikasema: ‘Anastahili kufa.’ Wakamupiga makofi, wakamutemea mate, wakafunika macho yake, wakamupiga na kumuambia: ‘Kama uko nabii, tuambie nani njo anakupiga!’

Wakati ilikuwa asubui, wakamupeleka Yesu mu chumba cha Sanhedrini na wakamuuliza tena: ‘Uko Mwana wa Mungu?’ Yesu akawajibu: ‘Ninyi wenyewe mumesema kama niko Mwana wa Mungu.’ Kwa hiyo, wakamuhukumu kwa kusema kama kosa lake ni kumutukana Mungu na wakamupeleka kwa Pontio Pilato, Gavana wa Roma. Kisha kulitokea nini? Tutaona ile mu sura ya kufuata.

“Saa . . . imekuja, wakati kila mumoja wenu atatawanyika na kuenda kwenye nyumba yake mwenyewe na mutaniacha peke yangu. Lakini siko peke yangu, kwa sababu Baba iko pamoja na mimi.”​—Yohana 16:32

Maulizo: Ni nini ilitokea mu kiwanja cha nyumba ya Kayafa? Juu ya nini tribinali iliamua kama Yesu anastahili kufa?

Matayo 26:31-35, 57–27:2; Marko 14:27-31, 53–15:1; Luka 22:55-71; Yohana 13:36-38; 18:15-18, 25-28

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine