Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 92 uku. 214-uku. 215 fu. 1
  • Yesu Anawatokea Wavuvi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anawatokea Wavuvi
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Pembeni ya Bahari ya Galilaya
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Alishinda Woga na Mashaka
    Tuige Imani Yao
  • Maisha ya Watu Wakati wa Zamani—Muvuvi wa samaki
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Wanafunzi Ine Watakuwa Wavuvi wa Watu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 92 uku. 214-uku. 215 fu. 1
Yesu anazungumuza na wanafunzi wake wakati samaki wako ku moto

92

Yesu Anawatokea Wavuvi

Wakati fulani kisha Yesu kutokea mitume, Petro aliamua kuenda kuvua ao kuloa samaki mu Bahari ya Galilaya. Tomasi, Yakobo, Yohana, na wanafunzi wengine walimufuata. Walivua samaki usiku wote, lakini hawakupata kitu.

Siku yenye ilifuata, asubui sana, wakaona mwanaume mumoja amesimama pembeni ya bahari. Akawauliza: ‘Mulipata samaki?’ Wakamuambia, “Hapana!” Akasema, ‘Mutupe wavu (filet) ngambo ya kuume ya mashua.’ Wakati walifanya vile, wavu ukajaa samaki mupaka wakashindwa kuukokota. Palepale Yohana akatambua kama ule mwanaume ni Yesu na akasema: “Ni Bwana!” Mara moja, Petro akajitupa mu maji na akaogelea mupaka pembeni ya bahari. Wanafunzi wengine wakamufuata na mashua.

Wakati walifika pembeni ya bahari, wakaona mukate na samaki ku moto. Yesu akawaambia walete samaki fulani kati ya samaki wenye walivua. Kisha akawaambia: “Mukuje mukule.”

Petro anafika karibu na Yesu pembeni ya bahari na wanafunzi wengine wanamufuata na mashua

Kisha kula, Yesu akamuuliza Petro: ‘Unanipenda kupita kazi ya kuvua samaki?’ Petro akasema, “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda.” Yesu akamuambia, ‘Basi lisha wana-kondoo wangu.’ Yesu akamuuliza tena: ‘Petro, unanipenda?’ Petro akasema, ‘Bwana, unajua kama ninakupenda.’ Yesu akamuambia, “Chunga kondoo wangu wadogo.” Yesu akamuuliza tena mara ya tatu. Petro akahuzunika sana. Akasema, “Bwana, unajua mambo yote; unajua kama ninakupenda.” Yesu akamuambia, “Lisha kondoo wangu wadogo.” Kisha akamuambia Petro: “Endelea kunifuata.”

“[Yesu] akawaambia: ‘Munifuate, na mimi nitawafanya ninyi kuwa wavuvi wa watu.’ Mara moja wakaacha nyavu zao na kumufuata.”​—Matayo 4:19, 20

Maulizo: Yesu alifanyia wavuvi muujiza gani? Unawaza ni juu ya nini Yesu alimuuliza Petro mara tatu ikiwa anamupenda?

Yohana 21:1-19, 25; Matendo 1:1-3

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine