Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 95 uku. 222-uku. 223 fu. 1
  • Hakuna Kitu Kingeweza Kuwazuia Kuhubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Hakuna Kitu Kingeweza Kuwazuia Kuhubiri
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Tunapaswa Kumutii Mungu Kuwa Mutawala”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • “Watu Wenye Hawana Elimu na Watu wa Kawaida”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Bwana Wake Alimufundisha Kusamehe
    Tuige Imani Yao
  • Yesu Anakulisha Maelfu ya Watu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 95 uku. 222-uku. 223 fu. 1
Petro na Yohana wanahubiri kwa uhodari hata kama makuhani na Wasadukayo wanawapinga

95

Hakuna Kitu Kingeweza Kuwazuia Kuhubiri

Mwanaume mumoja mwenye hakukuwa anatembea alikuwa anazoea kuomba-omba karibu na mulango mukubwa wa hekalu. Alikuwa anakaa pale kila siku. Siku moja, mangaribi, aliona Petro na Yohana wanaingia mu hekalu. Akawaambia: ‘Tafazali, munipatie kitu fulani.’ Petro akamuambia: ‘Niko na kitu kizuri sana cha kukupatia chenye kinapita feza. Katika jina la Yesu, simama na utembee!’ Kisha Petro akamusimamisha, na ule mwanaume akaanza kutembea! Watu wengi walifurahi sana kuona ule muujiza na wengi wakakuwa waamini.

Lakini makuhani na Wasadukayo walikasirika. Walikamata mitume, wakawapeleka ku tribinali, na kuwauliza: ‘Nani njo aliwapatia nguvu ya kuponyesha ule mutu?’ Petro akasema: ‘Yesu, mwenye muliua, njo alitupatia ile nguvu.’ Viongozi wa dini wakalalamika: ‘Muache kuzungumuza juu ya Yesu!’ Lakini mitume wakawaambia: ‘Tunapaswa kusema juu yake. Hatutaacha.’

Kisha tu Petro na Yohana kuachiliwa, walienda kuelezea wanafunzi wengine mambo yenye ilitokea. Wote pamoja, wakasali: ‘Tafazali Yehova, utupatie uhodari ili tuendelee kufanya kazi yako.’ Yehova akawapatia roho yake takatifu, na wakaendelea kuhubiri na kuponyesha. Watu mingi sana wakakuwa waamini. Wasadukayo wakasikia wivu sana mupaka wakafikia kukamata mitume na kuwafunga. Lakini usiku, Yehova akatuma malaika afungue milango ya gereza na akaambia mitume: ‘Murudie kwenye hekalu, na mufundishe watu.’

Asubui ya siku yenye ilifuata, walinzi wakaambia Sanhedrini (tribinali ya viongozi wa dini ya Wayahudi): ‘Gereza ingali inafungwa, lakini wanaume wenye mulikamata hawako ndani! Wako wanafundisha watu mu hekalu!’ Mitume wakakamatwa tena na kupelekwa mbele ya Sanhedrini. Kuhani mukubwa akawaambia: ‘Tuliwakataza kusema juu ya Yesu!’ Lakini Petro akajibu: ‘Tunapaswa kumutii Mungu kuliko wanadamu.’

Viongozi wa dini walikasirika sana na walitaka kuua mitume. Lakini Mufarisayo mumoja mwenye aliitwa Gamalieli akasimama na kusema: ‘Mufanye angalisho! Pengine Mungu iko pamoja na watu hawa. Munapenda kabisa kupigana na Mungu?’ Wakasikiliza shauri lake. Kisha kupiga mitume fimbo, wakawakataza tena kuhubiri, na kisha wakawaacha waende. Lakini ile haikufanya mitume wavunjike moyo. Waliendelea kuhubiri habari njema bila woga, mu hekalu na nyumba kwa nyumba.

“Tunapaswa kumutii Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.”​—Matendo 5:29

Maulizo: Juu ya nini wanafunzi hawakuacha kuhubiri? Yehova aliwasaidia namna gani?

Matendo 3:1–4:31; 5:12-42

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine