Utangulizi wa Sehemu ya 3
Biblia inazungumuzia watu kidogo sana wenye walimutumikia Yehova kisha Garika. Kwa mufano Abrahamu, mwenye alijulikana kuwa rafiki ya Yehova. Juu ya nini Yehova alimuita rafiki yake? Kama uko muzazi, fundisha mutoto wako kama Yehova anamupenda kabisa na anataka kumusaidia. Kama Abrahamu na wanaume wengine waaminifu, sawa vile Loti na Yakobo, tunaweza kumuomba Yehova kwa uhuru wote ili atusaidie. Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatimiza mambo yote yenye anasema atafanya.