Utangulizi wa Sehemu ya 6
Wakati Waisraeli walifika mu Inchi ya Ahadi, tabenakulo ikakuwa nafasi kubwa ya ibada ya kweli. Makuhani walifundisha watu Sheria, na waamuzi waliongoza taifa. Hii sehemu inaonyesha namna maamuzi na matendo ya mutu inaweza kuchochea sana wengine wafanye mambo ya muzuri ao ya mubaya. Kila Mwisraeli alipaswa kuwa muaminifu kwa Yehova na kwa watu wengine. Inaonyesha namna Debora, Naomi, Yoshua, Hana, binti ya Yefta, na Samweli walikuwa mifano ya muzuri kwa wengine. Inaonyesha tena kama hata watu fulani wenye hawakukuwa Waisraeli, kama vile Rahabu, Rutu, Yaeli, na Wagibeoni walichagua kuwa upande wa Waisraeli kwa sababu walitambua kama Mungu alikuwa pamoja nao.