Utangulizi wa Sehemu ya 7
Sehemu hii inazungumuzia historia ya maisha ya Mufalme Sauli na Mufalme Daudi. Inazungumuzia mambo yenye ilifanyika mu kipindi cha miaka 80 hivi. Ku mwanzo, Sauli alikuwa munyenyekevu na alimuogopa Mungu. Lakini kisha wakati fulani alibadilika na kukataa kufuata muongozo wa Yehova. Yehova alimukataa, na kisha wakati fulani akaambia Samweli atie Daudi mafuta juu akuwe mufalme wa pili wa Israeli. Juu ya wivu, Sauli alitafuta mara mingi kuua Daudi. Lakini, Daudi hakulipiza kisasi. Yonatani, mutoto ya Sauli, alijua kama Yehova alikuwa amechagua Daudi. Kwa hiyo, alichagua kuwa mushikamanifu kwa Daudi. Hata kama Daudi alifanya zambi fulani nzito, aliitika Yehova amurekebishe. Kama uko muzazi, usaidie mutoto wako ajue kama ni jambo ya maana sana kuwa muaminifu kwa Yehova na kutii wale wenye amechagua juu watuongoze.