Utangulizi wa Sehemu ya 10
Yehova ni mukubwa kupita wafalme wote. Hakuna kitu chenye kimekwisha kumushinda, na hakuna kitu chenye kitamushindaka. Kwa mufano, wakati walitupa Yeremia mu shimo, Yehova alimuokoa ili asikufe. Aliokoa Shadraki, Meshaki, na Abednego kutoka katika tanuru ya moto na aliokoa Danieli ili simba wasimukule. Yehova alilinda Esta ili aokoe taifa lote. Hataacha mambo ya mubaya iendelee milele. Unabii wenye unazungumuzia sanamu kubwa na wenye unazungumuzia muti mukubwa unaonyesha kabisa kama karibuni Ufalme wa Yehova utatosha mambo yote ya mubaya na utatawala dunia.