WIMBO 28
Rafiki ya Yehova Ni Nani?
Maandishi
1. Ni nani rafiki
yako eh Yehova?
Nani anakujua weye?
Nani unapenda?
Mwenye anasoma
Neno yako sana,
Mushikamanifu, na mwenye
haki na imani.
2. Nani anaweza
kukukaribia?
Nani unajua kwa jina
na kufurahia?
Mwenye kukusifu
na kukusikia,
Muaminifu tena mwenye
anasema kweli.
3. Tunaufungua
moyo wetu kwako,
Unatuhangaikiaka
na unatupenda.
Tunapenda sana
kukukaribia.
Hatuna rafiki mwingine
kama weye Baba.
(Ona pia Zb. 139:1; 1 Pe. 5:6, 7.)