WIMBO 43
Sala ya Shukrani
Maandishi
1. Yehova Mungu ninasali kwako
Ili kukushukuru kwa yote.
Nitakutumikia sikuzote;
Unanihangaikia sana.
Ninafanyaka zambi kila siku;
Baba naomba unisamehe,
Unajua kama niko mavumbi.
Aksanti sana kwa ukombozi.
2. Nakushukuru kwa upendo wako.
Aksanti kwa kuniita kwako.
Nisaidie nikutumikie.
Nifundishe kuwa mwaminifu.
Aksanti Yah! kwa roho takatifu,
Pia kwa nguvu ya kuhubiri.
Ninapenda kuwa munyenyekevu,
Na kusema aksanti milele.