WIMBO 102
‘Musaidie Wale Wenye Kuwa Wazaifu’
Maandishi
1. Hakuna mutu mwenye
hakoseake.
Hata vile Yehova
anatupenda.
Iko na rehema,
basi tumuige;
Na siye tupendane
kwa moyo wote.
2. Maneno ya faraja
na yenye nguvu
Ni ya lazima sana
kwa wazaifu.
Ni watu wa Mungu,
atawakumbuka.
Tuwahangaikie
tusiwaache.
3. Tena tusifokee
ndugu na dada.
Tuwaonyeshe kama
tunawapenda.
Tuwasaidie
na kuwafariji,
Ili imani yao
ikuwe nguvu.
(Ona pia Isa. 35:3, 4; 2 Ko. 11:29; Gal. 6:2.)