WIMBO 113
Tuko Wenye Amani
Maandishi
1. Tumusifu Yehova
mwenye amani.
Atamaliza vita
na maumivu.
Mukubwa wa amani
ni Yesu Kristo;
Atafanya kukuwe
amani sana.
2. Maneno ya makali
tulishaacha.
Mikuki na mipanga
tulishatupa.
Tunafanya amani
na watu wote.
Na tuhurumiane
kila wakati.
3. Amani tuko nayo
inashangaza;
Ni baraka ya Mungu,
tuko hakika.
Tutii maagizo
na tupendane,
Njo tupate amani
kutoka juu.
(Ona pia Zb. 46:9; Isa. 2:4; Yak. 3:17, 18.)