WIMBO 124
Tukuwe Washikamanifu
Maandishi
1. Tumutii Mungu wetu,
tushikamane naye.
Mashauri yake yote
ni ya lazima sana.
Basi tumusikilize
na kumutegemea;
Kwa sababu tunajua,
ni mushikamanifu.
2. Tuwapende ndugu zetu,
tushikamane nao.
Na wakati wa magumu
tuwaunge mukono.
Hata nini itokee
tusiwaachilie.
Kwa maneno na matendo
hatutawasahau.
3. Tufuate maagizo,
tushikamane nayo;
Inatoka kwa wazee
wenye wanatupenda.
Basi tuwaheshimie
ili tukuwe nguvu.
Na Yehova Mungu wetu
atatupenda sana.
(Ona pia Zb. 149:1; 1 Ti. 2:8; Ebr. 13:17.)