WIMBO 130
Tusameheane
Maandishi
1. Mungu alituma
Yesu atukomboe
Katika zambi na kifo,
ili tukuwe huru.
Kama tunatubu kweli,
na kusali kwa Mungu,
Kupitia Yesu Kristo,
atatuhurumia.
2. Kama tunapenda
Mungu atusamehe,
Ni lazima tumuige,
kwa kusameheana.
Tupendane kila siku,
na kuvumiliana.
Na tukiheshimiana,
tutakaribiana.
3. Tunapaswa kuwa
tayari kusamehe,
Na kuepuka ugomvi,
chuki, na kasirani.
Tukikuwa na upendo,
Mungu atatupenda,
Na tutasameheana
bila kulazimishwa.
(Ona pia Mt. 6:12; Efe. 4:32; Kol. 3:13.)