WIMBO 139
Wazia Uko mu Dunia Mupya
1. Uwazie kila siku
Uko na miye mu Paradiso;
Hauchoke na maisha.
Muko amani na furaha;
Na Ufalme wa Yehova
Unatawala fasi yote;
Na hakuna tena watu wabaya.
Tutamuimbia Mungu kwa furaha:
(REFREE)
“Yehova, Mungu, aksanti sana.
Sasa mambo inabadilika.
Tunakuimbia ili kukusifu,
Kukuheshimia na kukushukuru.”
2. Pima tena kuwazia
Tuko sasa mu dunia mupya,
Na hamuna maumivu,
Hamuna woga wala kifo.
Sasa waza, unaona
Ndugu yako anafufuka.
Ahadi za Mungu zinatimia!
Tutakumbatiana na tutaimba:
(REFREE)
“Yehova, Mungu, aksanti sana.
Sasa mambo inabadilika.
Tunakuimbia ili kukusifu,
Kukuheshimia na kukushukuru.”
(Ona pia Zb. 37:10, 11; Isa. 65:17; Yoh. 5:28; 2 Pe. 3:13.)