SEHEMU YA PILI
“Ni Patakatifu Pangu Ndipo Mulichafua”—Ibada Safi Inapotoshwa
WAZO KUBWA: Wakaaji wa Yuda na Yerusalemu wanapotoka kiroho na mu mwenendo
Yehova alipenda na kuhangaikia Waisraeli kwa sababu walikuwa ‘mali yake yenye alipendezwa nayo sana.’ (Kut. 19:5, maelezo ya chini) Lakini kile wao walimulipa ni kuabudu miungu ya uongo mu hekalu lenye lilijulikana kuwa la Yehova! Walimuhuzunisha sana Yehova na kumuzaraulisha. Juu ya nini Waisraeli walipotoka sana vile? Unabii wa Ezekieli kuhusu kuharibiwa kwa Yerusalemu unaweza kutufundisha nini? Uhusiano wenye Waisraeli walifanya na mataifa yenye ilikuwa inawazunguka unaweza kutupatia somo gani?