Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rr uku. 26-27
  • 2B Ezekieli—Maisha na Wakati Wake

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 2B Ezekieli—Maisha na Wakati Wake
  • Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MANABII WA WAKATI WAKE
  • Yerusalemu Inaharibiwa
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
rr uku. 26-27

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 2B

Ezekieli​—Maisha na Wakati Wake

Maandishi

Ezekieli maana yake “Mungu Anatia Nguvu.” Hata kama maunabii yenye anazungumuzia iko na maonyo, ujumbe wote wenye kuwa ndani unapatana na maana ya jina lake na unatia nguvu imani ya wale wenye wanataka kumutolea Mungu ibada safi.

Ezekieli

MANABII WA WAKATI WAKE

  • Yeremia

    YEREMIA,

    wa familia moja ya kikuhani, alitumikia zaidi sana Yerusalemu (647–580 M.K.Y)

  • Hulda

    HULDA

    alitumika wakati kitabu cha Sheria kilivumbuliwa mu hekalu, mwaka wa 642 hivi M.K.Y.

  • Danieli

    DANIELI,

    wa familia ya kifalme ya Yuda, alipelekwa Babiloni mu mwaka wa 617 M.K.Y.

  • Habakuki

    HABAKUKI

    inawezekana alitumikia Yuda ku mwanzo wa utawala wa Yehoyakimu

  • Obadia

    OBADIA

    alitoa unabii juu ya Edomu, inawezekana wakati wa uharibifu wa Yerusalemu

WALITOA UNABII WAKATI GANI? (TAREHE ZOTE M.K.Y.)

Muchoro wa matukio wenye kuonyesha wakati Yeremia, Hulda, Danieli, Habakuki, Ezekieli, na Obadia walitoa unabii

MATUKIO MAKUBWA YA MAISHA YA EZEKIELI (TAREHE ZOTE M.K.Y.)

  1. 643 hivi: Anazaliwa

  2. 617: Anapelekwa mu utekwa Babiloni

  3. 613: Anaanza kutoa unabii; anaona maono ya Yehova

  4. 612: Anaona maono kuhusu uasi-imani ku hekalu

  5. 611: Anaanza kutangaza makosa ya wakaaji wa Yerusalemu

  6. 609: Bibi yake anakufa na maadui wanaanza kuzunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita kwa mara ya mwisho

  7. 607: Anapokea habari yenye kuhakikisha kwamba Yerusalemu imeharibiwa

  8. 593: Anaona maono ya hekalu

  9. 591: Anatabiri kwamba Nebukadneza atavamia Misri; anamaliza kuandika kitabu chake

WAFALME WA YUDA NA WA BABILONI

  1. 659-629: Yosia anaendelesha ibada safi lakini anakufa wakati iko anapigana na Farao Neko

  2. 628: Yehoahazi anatawala mubaya mu miezi tatu na anakamatwa na Farao Neko

  3. 628-618: Yehoyakimu ni mufalme mubaya na Farao Neko anamufanya kuwa mutawala mudogo

  4. 625: Nebukadneza anashinda jeshi la Misri

  5. 620: Nebukadneza anavamia Yuda kwa mara ya kwanza na anamufanya Yehoyakimu kuwa mutawala mudogo mu Yerusalemu

  6. 618: Yehoyakimu anaasi Nebukadneza lakini inawezekana anakufa wakati Wababiloni wanavamia Inchi ya Ahadi kwa mara ya pili

  7. 617: Yehoyakini, mwenye anajulikana pia kwa jina la Yekonia, ni mufalme mubaya mwenye anatawala mu miezi tatu na kisha anajitia mu mikono ya Nebukadneza

  8. 617-607: Sedekia, mufalme muovu, muoga, anafanywa kuwa mutawala mudogo na Nebukadneza

  9. 609: Sedekia anaasi Nebukadneza, mwenye anafikia kuvamia Yuda kwa mara ya tatu

  10. 607: Nebukadneza anaharibu Yerusalemu, anakamata Sedekia, anamufanya kuwa kipofu, na anamupeleka Babiloni

Rudia ku sura ya 2, fungu la 28, 29

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine