KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 2B
Ezekieli—Maisha na Wakati Wake
Ezekieli maana yake “Mungu Anatia Nguvu.” Hata kama maunabii yenye anazungumuzia iko na maonyo, ujumbe wote wenye kuwa ndani unapatana na maana ya jina lake na unatia nguvu imani ya wale wenye wanataka kumutolea Mungu ibada safi.
MANABII WA WAKATI WAKE
YEREMIA,
wa familia moja ya kikuhani, alitumikia zaidi sana Yerusalemu (647–580 M.K.Y)
HULDA
alitumika wakati kitabu cha Sheria kilivumbuliwa mu hekalu, mwaka wa 642 hivi M.K.Y.
DANIELI,
wa familia ya kifalme ya Yuda, alipelekwa Babiloni mu mwaka wa 617 M.K.Y.
HABAKUKI
inawezekana alitumikia Yuda ku mwanzo wa utawala wa Yehoyakimu
OBADIA
alitoa unabii juu ya Edomu, inawezekana wakati wa uharibifu wa Yerusalemu
WALITOA UNABII WAKATI GANI? (TAREHE ZOTE M.K.Y.)
MATUKIO MAKUBWA YA MAISHA YA EZEKIELI (TAREHE ZOTE M.K.Y.)
643 hivi: Anazaliwa
617: Anapelekwa mu utekwa Babiloni
613: Anaanza kutoa unabii; anaona maono ya Yehova
612: Anaona maono kuhusu uasi-imani ku hekalu
611: Anaanza kutangaza makosa ya wakaaji wa Yerusalemu
609: Bibi yake anakufa na maadui wanaanza kuzunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita kwa mara ya mwisho
607: Anapokea habari yenye kuhakikisha kwamba Yerusalemu imeharibiwa
593: Anaona maono ya hekalu
591: Anatabiri kwamba Nebukadneza atavamia Misri; anamaliza kuandika kitabu chake
WAFALME WA YUDA NA WA BABILONI
659-629: Yosia anaendelesha ibada safi lakini anakufa wakati iko anapigana na Farao Neko
628: Yehoahazi anatawala mubaya mu miezi tatu na anakamatwa na Farao Neko
628-618: Yehoyakimu ni mufalme mubaya na Farao Neko anamufanya kuwa mutawala mudogo
625: Nebukadneza anashinda jeshi la Misri
620: Nebukadneza anavamia Yuda kwa mara ya kwanza na anamufanya Yehoyakimu kuwa mutawala mudogo mu Yerusalemu
618: Yehoyakimu anaasi Nebukadneza lakini inawezekana anakufa wakati Wababiloni wanavamia Inchi ya Ahadi kwa mara ya pili
617: Yehoyakini, mwenye anajulikana pia kwa jina la Yekonia, ni mufalme mubaya mwenye anatawala mu miezi tatu na kisha anajitia mu mikono ya Nebukadneza
617-607: Sedekia, mufalme muovu, muoga, anafanywa kuwa mutawala mudogo na Nebukadneza
609: Sedekia anaasi Nebukadneza, mwenye anafikia kuvamia Yuda kwa mara ya tatu
607: Nebukadneza anaharibu Yerusalemu, anakamata Sedekia, anamufanya kuwa kipofu, na anamupeleka Babiloni