Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • th somo ya 19 uku. 22
  • Kujikaza Kugusa Moyo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kujikaza Kugusa Moyo
  • Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uchangamufu
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kuonyesha Wasikilizaji Namna ya Kutumikisha Habari
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kutia Watu Moyo
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kuzungumuza kwa Upole na kwa Upendo
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
Ona Habari Zaidi
Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
th somo ya 19 uku. 22

SOMO YA 19

Kujikaza Kugusa Moyo

Andiko

Mezali 3:1

JAMBO LA KUFANYA: Saidia wasikilizaji wako waone faida ya mambo yenye wamejifunza na watende kulingana nayo.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Saidia wasikilizaji wako wajichunguze. Tumia maulizo yenye haiombe wasikilizaji wajibie kwa sauti juu ya kuwasaidia wachunguze mawazo yao wenyewe.

  • Saidia wasikilizaji wakuwe na nia ya muzuri. Tia moyo wasikilizaji wako wachunguze juu ya nini wanafanyaka matendo ya muzuri. Uwasaidie wakuwe wanafanya mambo juu ya kuchochewa na nia ya muzuri, maana yake kupenda Yehova, kupenda wanadamu wenzao, na kupenda mafundisho ya Biblia. Fikiri na wasikilizaji wako; usiwaambie-ambie tu mambo yenye wanapaswa kufanya ao kuwachambua-chambua. Kuliko kuwapatisha haya ao kuwafanya wajisikie kuwa na kosa, uwaache wakiwa wametiwa moyo ku mwisho ya hotuba yako, wakiwa wamechochewa kufanya ile wanaweza.

  • Saidia wasikilizaji wako wakaze akili yao juu ya Yehova. Onyesha namna mafundisho ya Biblia, kanuni za Biblia, na amri za Biblia zinaonyesha sifa za Mungu na namna anatupenda. Saidia wasikilizaji wako wakuwe wanafikiria kwanza namna Yehova anaona mambo na wakuwe na tamaa ya kumufurahisha.

    Shauri

    Kumbuka kwamba Yehova njo anavutaka watu. Tumia Neno lake juu ya kugusa moyo wa wasikilizaji wako.

MU MAHUBIRI:

Wakati inawezekana, tumia maulizo juu ya kujua mambo yenye musikilizaji wako anaamini kabisa. Angalia sura yake na usikilize muzuri sauti yake juu ya kujua namna anajisikia kabisa. Lakini, ukuwe muvumilivu. Pengine itaomba akutumainie kwanza mbele ya kuanza kukuambia mambo yenye iko mu moyo wake.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine