Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lff somo 5
  • Biblia Ni Neno ya Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia Ni Neno ya Mungu
  • Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
  • KWA KIFUPI
  • HABARI ZINGINE
  • Habari Njema Yenye Iko mu Biblia Inatoka Kabisa kwa Mungu?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Jinsi Unaweza Kuvumbua Kile Mungu Anataka
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Bhayibele yi ko go Thušeng mo o ka fo yi Bala
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Unawaza Biblia Inaweza Kukusaidia?
    Furahia Maisha Milele!—Anza Kujifunza Biblia
Ona Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
lff somo 5
Somo ya 5. Mwanaume iko anasoma Biblia mu bisi.

SOMO YA 05

Biblia Ni Neno ya Mungu

Maandishi
Maandishi
Maandishi

Yehova ametupatia zawadi ya muzuri sana. Ile zawadi ni Biblia. Iko na vitabu vidogo-vidogo 66. Unaweza kujiuliza: ‘Biblia ilitoka wapi? Nani njo aliiandikishaka?’ Juu upate majibu, tuone Mungu alifanya nini juu tukuwe na Biblia.

1. Watu njo waliandikaka Biblia, sasa juu ya nini tunasema kama ni Neno ya Mungu?

Watu 40 hivi njo waliandikaka Biblia. Kazi ya kuiandika ilifanyaka miaka karibu 1 600, kuanzia mwaka wa 1513 M.K.Y. mupaka mwaka wa 98 hivi K.K.Y. Wenye waliiandikaka walikuwa watu wa hali mbalimbali. Kwa mufano, wamoja walikuwa wafalme, wachungaji, na wavuvi. Hata vile, Biblia yote inapatana. Juu ya nini? Juu Mungu njo aliiandikishaka. (Soma 1 Watesalonike 2:13.) Wenye waliandikaka Biblia, hawakuandikaka mawazo yao. “Walisema yenye yalitoka kwa Mungu wakiongozwa na roho takatifu.”a (2 Petro 1:21) Mungu alitumiaka roho yake takatifu juu ya kuwaongoza waandike mawazo yake.​—2 Timoteo 3:16.

2. Kila mutu anaweza kupata Biblia?

Mungu anapenda Biblia isaidie watu wa “kila taifa na kabila na luga.” (Soma Ufunuo 14:6.) Njo maana alifanya mipango juu Biblia itafsiriwe mu luga za mingi. Leo, hakuna kitabu ingine yenye iko mu luga za mingi sana sawa vile Biblia. Karibu kila mutu anaweza kusoma Biblia, ikuwe anaishi wapi ao anasemaka luga gani.

3. Namna gani Yehova amelinda Biblia?

Biblia iliandikwa ku vitu vyenye vilikuwa vinaharibika mbio, sawa vile ngozi na makaratasi fulani yenye ilitengenezwa na mumea wenye kuitwa papyrus. Ile ingefanya Biblia ipotee. Lakini, watu wenye walipenda Biblia walikuwa wanafanya kopi ya Biblia. Walikuwa wanafanya vile kwa mukono na kwa uangalifu. Watawala na viongozi fulani wa makanisa walifanya nguvu yao yote juu waharibu Biblia. Lakini, watu wengine walikubali kuteseka ao hata kufa juu tu ya kulinda Biblia. Yehova hayaruhusu mutu yeyote ao kitu yoyote imuzuie kuzungumuza na siye. Biblia inasema hivi: “Neno la Mungu wetu linadumu milele.”​—Isaya 40:8.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna Mungu aliongoza watu juu waandike Biblia, namna alilinda Biblia, na mambo yenye alifanya juu tukuwe nayo.

4. Biblia inatuambia ni nani njo aliiandikishaka

Muangalie VIDEO. Kisha musome 2 Timoteo 3:16, na muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

VIDEO: Ni Nani Aliandikisha Biblia?​—Sehemu (2:48)

  • Watu njo waliandikaka Biblia, sasa juu ya nini tunasema kama ni Neno ya Mungu?

  • Unaamini kabisa kama Mungu aliongoza watu juu waandike mawazo yake?

Mukubwa wa kazi iko anaambia sekretere wake mawazo ya kuandika, na ule sekretere iko anaiandika mu barua.

Mutu anaweza kumuambia sekretere wake amuandikie barua. Mawazo yenye iko mu ile barua haiko ya sekretere, ni ya ule mutu. Vilevile, watu wenye waliandika Biblia hawakuandikaka mawazo yao, waliandikaka njo mawazo ya Mungu

5. Biblia iliokoka, hata kama watu walitafuta kuiharibu

Kama Biblia ni Neno ya Mungu, anapaswa kuilinda. Tangu zamani, wenye mamlaka wamefanya nguvu yao yote juu waharibu Biblia. Viongozi wa makanisa hawakupenda watu wasome Biblia. Lakini, watu wengine walikubali kuteswa ao hata kufa juu tu ya kulinda Biblia. Juu ya kujua mutu fulani mwenye alifanyaka vile, muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

VIDEO: Waliona Biblia Kuwa ya Maana​—Sehemu (William Tyndale) (6:17)

  • Kujua kama watu walikubali kuteswa ao hata kufa juu tu ya kulinda Biblia, kunakufanya upende kuisoma? Juu ya nini unasema vile?

Musome Zaburi 119:97, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Nini njo ilifanya watu wengi wakubali kuteswa ao hata kufa juu tu ya kutafsiri Biblia na kuigawia watu?

6. Biblia ni kitabu ya watu wote

Biblia njo kitabu yenye imetafsiriwa mu luga za mingi sana na njo kitabu yenye watu wengi sana wako nayo. Musome Matendo 10:34, 35, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini Mungu anapenda Biblia itafsiriwe mu luga za mingi sana na watu wengi wakuwe nayo?

  • Nini njo inafanya ufurahie Biblia?

Watu wa rangi na inchi mbalimbali wako wanasoma Biblia mu luga yao.

Karibu

watu wote

mu dunia

wanaweza kusoma Biblia mu luga yenye wanaelewa

Inapatikana

ya muzima ao sehemu

mu luga zaidi ya

3 000

Biblia zenye zimechapishwa zinakadiriwa kuwa

5 000 000 000

hakuna kitabu yenye imechapishwa sana vile

WATU FULANI WANASEMAKA: “Biblia ni kitabu tu ya zamani yenye watu waliandikaka.”

  • Na weye unawaza nini?

  • Nini njo inaonyesha kama Biblia ni Neno ya Mungu?

KWA KIFUPI

Biblia ni Neno ya Mungu, na amefanya mipango juu watu wote wakuwe na Biblia.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Wakati tunasema kama Mungu aliongoza wale wenye waliandika Biblia, ile iko na maana gani?

  • Ni mambo gani yenye tumezungumuzia mu hii somo juu ya Biblia yenye inakushangaza sana?

  • Kujua kama Mungu amefanya ile mambo yote juu ya kuzungumuza na weye, kunakufanya ujisikie namna gani?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Soma historia ya Biblia juu uone namna kopi za Biblia zilichungwa, na namna Biblia ilifikia kutafsiriwa mu luga za mingi.

“Namna Tulifikia Kupata Biblia” (Amuka!, Mwezi wa 11, 2007)

Ona namna Biblia iliokoka hatari tatu.

“Biblia Iliokoka Namna Gani” (Munara wa Mulinzi Na. 4 2016)

Ona namna watu walikubali kuteswa ao hata kufa juu tu ya kutafsiri Biblia.

Waliona Biblia Kuwa ya Maana(14:26)

Watu wamefanya kopi ya maandishi ya Biblia na wameitafsiri mara mingi. Nini njo inaonyesha kama mawazo ya Biblia haikubadilishwa?

“Biblia Imebadilishwa ao Kugeuzwa?” (Inapatikana ku Enternete)

a Kama vile Somo ya 07 inaonyesha, roho takatifu ni nguvu yenye Mungu anatumiaka juu ya kufanya mambo mbalimbali.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine