Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lff somo 7
  • Yehova Ni Mutu wa Namna Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Ni Mutu wa Namna Gani?
  • Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
  • KWA KIFUPI
  • HABARI ZINGINE
  • Yesu Ni Mutu wa Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Endelea Kuvaa “Utu Mupya” Kisha Ubatizo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Kwa Nini Tujiache Kuongozwa na Roho ya Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mungu Ni Nani?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
Ona Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
lff somo 7
Somo ya 7. Mwanaume anasimama kwenye sehemu ya majiwe-majiwe na iko anaangalia bahari wakati wa mangaribi.

SOMO YA 07

Yehova Ni Mutu wa Namna Gani?

Maandishi
Maandishi
Maandishi

Unawazaka Yehova Mungu ni mutu wa namna gani? Unawazaka ni Mungu wa ajabu sana, lakini mwenye iko mbali sana na weye, sawa vile nyota zenye ziko mbali sana? Ao unawazaka kama Mungu haiko mutu wa kwelikweli, lakini ni nguvu fulani sawa vile upepo mukali? Kwa kweli, Yehova ni mutu wa namna gani? Kupitia Biblia, Yehova anatuambia sifa zake, na anatuambia kama anatuhangaikiaka.

1. Juu ya nini hatuwezi kumuona Mungu?

“Mungu ni Roho.” (Yohana 4:24) Yehova hana mwili sawa yetu. Yeye ni Roho na anaishi mbinguni, fasi kwenye hatuwezi kuona.

2. Yehova iko na sifa gani fulani?

Hatuwezi kumuona Yehova. Lakini wakati tunafikia kumujua muzuri, tunamupenda juu iko mutu wa kweli kabisa na iko na sifa za muzuri sana. Biblia inasema hivi: “Yehova anapenda haki, na hataacha washikamanifu wake.” (Zaburi 37:28) Tena, Yehova ni “mwenye upendo mwingi sana na mwenye rehema” kwa watu wote, zaidi sana kwa wale wenye kuteseka. (Yakobo 5:11) “Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo; anaokoa wale wenye kuvunjika moyo.” (Zaburi 34:18, maelezo ya chini) Unajuaka kama matendo yetu inaweza kumufurahisha Yehova ao kumuhuzunisha? Wakati mutu anafanya mambo ya mubaya, Yehova anahuzunikaka. (Zaburi 78:40, 41) Lakini wakati mutu anafanya mambo ya muzuri, Yehova anafurahiaka.​—Soma Mezali 27:11.

3. Namna gani Yehova anaonyesha kama anatupenda?

Sifa kubwa ya Yehova ni upendo. Biblia inasema kama “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Biblia na vitu vyenye Yehova aliumba vinaonyesha kama anatupenda. (Soma Matendo 14:17.) Kwa mufano, fikiria namna alituumba. Alitupatia uwezo wa kuona rangi za muzuri, kufurahia muziki, na kusikia butamu ya chakula. Anapenda tufurahie maisha.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone nini njo Yehova anatumiaka juu ya kufanya mambo ya ajabu. Kisha, tuone namna Yehova anatusaidiaka tujue sifa zake za muzuri na namna anazionyeshaka.

4. Roho takatifu ni nguvu ya Mungu

Picha: Mambo yenye roho takatifu ya Mungu ilifanya. 1. Planete mbalimbali na ulimwengu. 2. Muandikaji mumoja wa Biblia iko anaandika mawazo yenye roho ya Mungu inamuongoza aandike.

Sawa vile tu tunatumiaka mikono yetu juu ya kufanya kazi mbalimbali, Yehova naye anatumiaka roho yake takatifu juu ya kufanya kazi mbalimbali. Biblia inaonyesha kama roho takatifu haiko mutu, lakini ni nguvu yenye Mungu anatumiaka juu ya kufanya mambo mbalimbali. Musome Luka 11:13 na Matendo 2:17, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Mungu ‘atamwanga’ roho yake takatifu juu ya wale wenye wanaiomba. Sasa unawaza roho takatifu ni mutu, ao ni nguvu yenye Mungu anatumiaka juu ya kufanya mambo mbalimbali? Juu ya nini unasema vile?

Yehova anatumiaka roho yake takatifu juu ya kufanya mambo ya ajabu. Musome Zaburi 33:6 na 2 Petro 1:20, 21, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Yehova alitumia roho yake takatifu juu ya kufanya mambo gani?

Picha: Mambo yenye roho takatifu ya Mungu ilifanya. 1. Planete mbalimbali na ulimwengu. 2. Muandikaji mumoja wa Biblia iko anaandika mawazo yenye roho ya Mungu inamuongoza aandike.

5. Yehova iko na sifa za muzuri

Musa alikuwa mutumishi muaminifu wa Mungu, lakini alipenda kumujua Muumbaji wake muzuri zaidi. Njo maana, alimuambia Mungu hivi: “Nijulishe njia zako, ili nikujue wewe.” (Kutoka 33:13) Kisha, Yehova aliambia Musa sifa zake fulani. Musome Kutoka 34:4-6, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yehova alimuambia Musa kama yeye ni Mungu wa namna gani?

  • Ni sifa gani za Yehova zenye unafurahia sana?

6. Yehova anahangaikiaka watu

Mwanamuke iko anasali.

Waisraeli walikuwa watu wa Mungu na walikuwa watumwa kule Misri. Yehova alijisikia namna gani wakati aliona mateso yao? Musikilize USOMAJI WA BIBLIA, ao musome Kutoka 3:1-10. Kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

USOMAJI WA BIBLIA: Yehova Aliona Mateso Yao (2:45)

  • Hii habari inaonyesha kama Yehova anajisikiaka namna gani wakati anaona watu wako wanateseka?​—Ona mustari wa 7 na 8.

  • Unawaza kama Yehova anapenda kabisa kusaidia watu na kama iko na uwezo wa kufanya vile? Juu ya nini unawaza vile?

7. Vitu vyenye Yehova aliumba vinaonyesha sifa zake

Picha: Balene na mutoto wake, maua, na ndege mwenye kuitwa muvumaji.

Vitu vyenye Yehova aliumba vinatusaidia kujua sifa zake. Muangalie VIDEO. Kisha musome Waroma 1:20, na muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

VIDEO: Uumbaji Unaonyesha Upendo wa Yehova​—Mwili wa Mwanadamu (1:57)

  • Wakati unaangalia vitu vyenye Yehova aliumba, unaona kama iko na sifa gani?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Mungu haiko mutu, ni nguvu tu yenye iko fasi yote.”

  • Weye unawaza nini?

  • Juu ya nini unawaza vile?

KWA KIFUPI

Yehova ni Roho, na hatuwezi kumuona. Iko na sifa mingi za muzuri. Sifa yake kubwa ni upendo.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini hatuwezi kuona Yehova?

  • Roho takatifu ni nini?

  • Taya sifa fulani za Yehova.

Pima kufanya hivi:

HABARI ZINGINE

Ujifunze juu ya sifa ine kubwa za Yehova juu umujue muzuri zaidi.

“Mungu Ni Mutu wa Namna Gani?” (Munara wa Mulinzi Na. 1 2019)

Ona mambo yenye kuonyesha kama Yehova hakuwake fasi yote.

“Mungu Iko Fasi Yote?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona juu ya nini Biblia inaita roho takatifu mikono ya Mungu.

“Roho Takatifu Ni Nini?” (Inapatikana ku Enternete)

Haikukuwa mwepesi kwa mwanaume fulani kipofu kuamini kama Mungu anamupenda. Ona mambo yenye ilimusaidia abadilishe mawazo yake.

“Sasa Ninajisikia Kuwa Ninaweza Kusaidia Wengine” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 10, 2015)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine