SOMO YA 11
Unaweza Kufanya Nini Juu Upate Faida Wakati Uko Nasoma Biblia?
Kuko siku ulianzaka kufanya kazi fulani kubwa lakini ukaona kama iko nguvu sana? Juu uweze, pengine ulianzaka kuifanya kidogo-kidogo. Biblia nayo ni vile. Unaweza kujiuliza, ‘Nitaanzia wapi?’ Mu hii somo, tutazungumuzia mambo fulani yenye unaweza kufanya juu ufurahie kusoma na kujifunza Biblia.
1. Juu ya nini tunapaswa kusoma Biblia kila siku?
Mutu mwenye anasomaka Biblia, ao “sheria ya Yehova” kila siku, anakuwaka na furaha na maisha ya muzuri. (Soma Zaburi 1:1-3.) Na weye upime kwanza. Ukuwe nasoma Biblia kila siku mu dakika kidogo tu. Wakati utaendelea kujua Biblia muzuri, ni vile utafurahia zaidi kuisoma.
2. Unapaswa kufanya nini juu upate faida wakati uko nasoma Biblia?
Juu upate faida wakati uko nasoma Biblia, usiende mbio-mbio. Ukuwe unasimama kidogo na kufikiri juu ya mambo yenye uko nasoma. Tunapaswa kusoma Biblia na “kufikiri sana juu yake.” (Yoshua 1:8, maelezo ya chini) Wakati uko nasoma, ukuwe najiuliza hii maulizo: ‘Hii mambo, inanifundisha nini juu ya Yehova? Ninaweza kuitumikisha namna gani mu maisha yangu? Ninaweza kuitumikisha namna gani juu ya kusaidia wengine?’
3. Unaweza kufanya nini juu upate wakati ya kusoma Biblia?
Unakosaka wakati ya kusoma Biblia? Hauko weye peke. Ujikaze ‘kutumia muzuri zaidi wakati wako.’ (Waefeso 5:16) Unaweza kufanya vile namna gani? Upange wakati ya kusoma Biblia kila siku. Watu fulani wanasomaka Biblia asubui sana. Wengine wanasomaka Biblia muchana, wakati ya kupumuzika. Na wengine wanasomaka Biblia usiku, mbele ya kulala. Na weye, unaweza kuwa nasoma Biblia saa gani?
TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
Tuone mambo yenye unaweza kufanya juu ufurahie zaidi kusoma Biblia, na namna unaweza kujitayarisha juu uelewe muzuri mambo yenye tuko najifunza.
Tunaweza kujifunza kufurahia chakula mbalimbali, vilevile tunaweza kujifunza kufurahia kusoma Biblia
4. Furahia kusoma Biblia
Inaweza kuwa nguvu kuanza kusoma Biblia. Lakini, unaweza ‘kukomalisha tamaa’ ya kuisoma, sawa vile mutu anafikiaka kufurahia chakula yenye hazoee. Musome 1 Petro 2:2, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Kama unakuwa nasoma Biblia kila siku, unawaza utaifurahia na utakuwa na hamu ya kuendelea kuisoma?
Muangalie VIDEO juu muone nini njo ilisaidiaka watu fulani waanze kufurahia kusoma Biblia. Kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.
Vile uliona mu video, nini njo ilifanya ikuwe nguvu kwa wale vijana kusoma Biblia?
Nini njo iliwasaidia wakuwe nasoma Biblia kila siku?
Walifanya nini juu wafurahie zaidi kusoma Biblia?
Mashauri ya kukusaidia uanze kusoma Biblia:
Tumia tafsiri yenye haina makosa, yenye inatumia luga ya sasa. Pima kusoma Tafsiri ya Ulimwengu Mupya kama iko mu luga yako.
Usome kwanza sehemu zenye unafurahia sana. Juu ya kupata mawazo ya kukusaidia, ona muchoro “Anza Kusoma Biblia.”
Andika sehemu zenye ulishasoma. Tumia muchoro “Sura za Biblia Zenye Nilishasoma” yenye iko mu hii kitabu.
Tumia JW Library®. Kama uko nayo mu telefone, tablete ao chombo ingine ya kielektronike, unaweza kuitumia juu ya kusoma na kusikiliza usomaji wa Biblia hata ukuwe wapi.
Tumia nyongeza zenye kuwa mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Mule utapata karte, michoro, na maana ya maneno fulani. Ile yote itakusaidia ufurahie zaidi kusoma Biblia.
5. Ukuwe natayarisha habari yenye tutajifunza
Musome Zaburi 119:34, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Juu ya nini ni muzuri kusali mbele ya kusoma Biblia, ao mbele ya kutayarisha habari yenye tutajifunza?
Unaweza kufanya nini juu upate faida kabisa wakati tuko najifunza? Wakati uko natayarisha kila somo, pima kufanya hivi:
Usome mafungu ya kwanza-kwanza yenye kuwa mu somo.
Ujikaze kuona namna inapatana na mambo yenye somo inazungumuzia.
Utie alama ku maneno ao misemwa yenye inajibia kila ulizo; ile itakusaidia wakati tutajifunza.
Unajua?
Mashahidi wa Yehova wametumia tafsiri mbalimbali za Biblia. Lakini, wanafurahiaka sana Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya juu haina makosa, iko wazi, na inatumia jina ya Mungu.—Ona habari yenye inapatikana ku Enternete yenye kichwa “Mashahidi wa Yehova Wanakuwaka na Biblia Yao?”
WATU FULANI WANASEMAKA: “Ni nguvu kujifunza Biblia, sina wakati na sina nguvu ya kujifunza.”
Na weye unawaza nini?
KWA KIFUPI
Juu Biblia ikuletee faida, upange wakati ya kuisoma, uombe Mungu akusaidie uelewe mambo yenye uko nasoma, na ukuwe natayarisha habari yenye tutajifunza.
Maulizo ya kujikumbusha
Unaweza kufanya nini juu upate faida wakati uko nasoma Biblia?
Saa gani njo unaweza kuwa nasoma na kujifunza Biblia?
Juu ya nini ni muzuri ukuwe natayarisha habari yenye tutajifunza?
HABARI ZINGINE
Ona mawazo fulani yenye inaweza kukusaidia upate faida wakati uko nasoma Biblia.
“Namna ya Kupata Faida Wakati Unasoma Biblia” (Munara wa Mulinzi Na. 1 2017)
Ona njia tatu za kusoma Biblia.
Ona mambo ya kufanya juu ufurahie kusoma Biblia.
Watu fulani wamesoma Biblia kwa miaka mingi, ona mambo yenye imewasaidia.