SOMO YA 15
Yesu Ni Nani?
Yesu iko kati ya watu wenye wanajulikana sana. Watu wengi wanajua jina ya Yesu, lakini hawamujue muzuri. Na ukiuliza watu kama Yesu ni nani, utaona kama kila mutu iko na yake jibu. Biblia inafundisha mambo gani juu ya Yesu?
1. Yesu ni nani?
Yesu ni malaika mwenye nguvu mwenye anaishi mbinguni. Mbele Yehova aumbe vitu vingine vyote, aliumbaka kwanza Yesu. Njo maana Biblia inamuita “muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.” (Wakolosai 1:15) Tena Biblia inaita Yesu ‘Mwana muzaliwa-pekee’ juu yeye tu njo Yehova aliumbaka moja kwa moja. (Yohana 3:16) Yesu alitumika sana na Baba yake, Yehova, juu ya kumusaidia kuumba vitu vingine vyote. (Soma Mezali 8:30.) Yesu angali anatumika sana na Yehova. Yeye ni “Neno” ao musemaji wa Mungu. Mungu anamutumaka aende kuambia viumbe wake habari fulani na mambo yenye anapenda wafanye.—Yohana 1:14.
2. Juu ya nini Yesu alikuya ku dunia?
Miaka 2000 hivi yenye imepita, Yehova alifanyaka muujiza. Alitumiaka roho yake takatifu juu ya kutosha uzima wa Yesu mbinguni na kuuhamishia mu tumbo ya mwanamuke bikira mwenye aliitwa Maria. Vile njo Yesu alizaliwaka sawa mwanadamu. (Soma Luka 1:34, 35.) Yesu njo Masiya ao Kristo mwenye Mungu alitumaka ku dunia juu aokoe wanadamu.a Maunabii yote ya Biblia juu ya Masiya mu maisha ya Yesu. Ile ilisaidia watu watambue kama Yesu njo “Kristo, Mwana wa Mungu mwenye kuishi.”—Matayo 16:16.
3. Yesu iko wapi leo?
Kisha Yesu kufa, Mungu alimufufuaka, akakuwa tena malaika, na akarudia mbinguni. Kule mbinguni, “Mungu alimuinua kwenye cheo cha juu zaidi.” (Wafilipi 2:9) Sasa, Yesu iko malaika mwenye nguvu sana. Yehova tu njo iko na nguvu zaidi kumupita.
TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
Tuone Yesu ni nani kabisa na tuone juu ya nini ni jambo ya maana tujifunze juu yake.
4. Yesu haiko Mungu Mweza-Yote
Yesu ni malaika mwenye nguvu sana. Lakini, anakuwaka anatii Yehova Mungu. Juu ya nini tunasema vile? Muangalie VIDEO juu muone namna Biblia inafundisha kama Yesu haiko sawasawa na Mungu Mweza-Yote.
Maandiko yenyeufuata.
Musome Luka 1:30-32.
Malaika alisema nini yenye inaonyesha kama Yesu haiko sawasawa na Yehova, Mungu “Mwenye Kuwa Juu Zaidi”?
Musome Matayo 3:16, 17.
Sauti kutoka mbinguni ilisema nini wakati Yesu alibatizwa?
Unawaza ilikuwa sauti ya nani?
Musome Yohana 14:28.
Nani njo mukubwa zaidi na nani njo iko na mamlaka zaidi? Baba ao mwana?
Yesu aliita Yehova kuwa Baba yake. Ile inaonyesha nini?
Musome Yohana 12:49.
Yesu anawazaka kama yeye na Baba yake ni mutu mumoja? Na weye unawaza nini?
5. Mambo yenye inaonyesha kama Yesu njo Masiya
Mu Biblia muko maunabii ya mingi yenye inazungumuzia Masiya, mwenye Mungu alichagula juu atuokoe. Ile maunabii ilisaidia watu watambue Masiya. Muangalie VIDEO juu muone maunabii fulani yenye Yesu alitimiza wakati alikuya ku dunia.
Musome maunabii ya Biblia na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata:
Musome Mika 5:2 juu mujue kwenye Masiya alipaswa kuzaliwa.b
Hii unabii ilitimia wakati Yesu alizaliwa?—Matayo 2:1.
Musome Zaburi 34:20 na Zekaria 12:10 juu muone mambo yenye Biblia ilikuwaka ilishasema juu ya kifo ya Masiya.
Ile maunabii ilitimiaka?—Yohana 19:33-37.
Unawaza Yesu alipangaka mambo juu ile maunabii itimie vile?
Ile inakuonyesha kama Yesu ni nani?
6. Utapata faida kama unajifunza juu ya Yesu
Biblia inaonyesha kama ni jambo ya maana sana kujifunza juu ya Yesu na juu ya kazi yenye Yehova alimupatia. Musome Yohana 14:6 na 17:3, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Juu ya nini ni jambo ya maana kujifunza juu ya Yesu?
Yesu alitufungulia njia ya kuwa marafiki wa Mungu. Alifundisha kweli juu ya Yehova. Na kupitia yeye tunaweza kupata uzima wa milele
WATU FULANI WANASEMAKA: “Mashahidi wa Yehova hawaamini Yesu.”
Unaweza kuwajibia namna gani?
KWA KIFUPI
Yesu ni malaika mwenye nguvu. Yeye ni Mwana wa Mungu na ni Masiya.
Maulizo ya kujikumbusha
Juu ya nini Biblia inaita Yesu kuwa “muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote”?
Yesu alifanyaka kazi gani mbele akuye hapa ku dunia?
Nini njo inaonyesha kama Yesu ni Masiya?
HABARI ZINGINE
Ona mambo yenye kuonyesha kama Yesu ni Masiya.
“Maunabii Juu ya Masiya Inaonyesha Kabisa Kama Yesu Alikuwa Masiya?” (Inapatikana ku Enternete)
Tafuta kujua ikiwa Biblia inafundisha kama Mungu alizalaka Yesu, sawa vile tu baba mwanadamu anazalaka watoto.
“Juu ya Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?” (Inapatikana ku Enternete)
Ona juu ya nini fundisho ya Utatu haipatane na Biblia.
“Yesu Ni Mungu?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 4, 2009)
Ona namna maisha ya mwanamuke fulani ilibadilika wakati alivumbula mambo yenye Biblia inafundisha juu ya Yesu.
a Somo ya 26 na 27 itaonyesha juu ya nini wanadamu walikuwa na lazima ya kukombolewa na namna Yesu anatukomboa.
b Ona Mafasirio Ingine ya 2 yenye inazungumuzia unabii wenye ulionyesha ni wakati gani Masiya angetokea ku dunia.