SOMO YA 56
Usaidie Kutaniko Iendelee Kuwa na Umoja
Wakati tuko na Wakristo wenzetu, tunajisikiaka sawa vile Mufalme Daudi alijisikiaka. Alisema hivi: “Ni muzuri sana na inapendeza sana ndugu kukaa pamoja kwa umoja!” (Zaburi 133:1) Umoja wenye uko kati yetu, haukuye hivi-hivi tu. Siye wote tunajikazaka juu tuendelee kuwa na umoja.
1. Juu ya nini watu wa Mungu wanakuwaka familia ya pekee sana?
Kama unaenda ku mukutano mu inchi ingine, pengine hautaelewa luga yenye wako nazungumuza. Lakini utajisikia sawa uko mu familia yako kabisa. Juu ya nini? Juu vichapo vyenye tunatumikishaka vinakuwaka sawasawa. Na tunajikazaka kuonyeshana upendo. Ikuwe tunaishi wapi, siye wote ‘tunaitia jina la Yehova, tunamuabudu kwa umoja.’—Sefania 3:9, maelezo ya chini.
2. Unaweza kufanya nini juu ya kuendelesha umoja?
“Mupendane sana kutoka katika moyo.” (1 Petro 1:22) Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama unafuata ile shauri? Usikuwe tu unaangalia makosa ya wengine, lakini ukuwe unatafuta sifa zao za muzuri. Usikuwe tu unapitisha wakati na watu wenye wanafurahiaka mambo yenye na weye unafurahiaka, lakini ujikaze kujua ndugu na dada wenye kuwa tofauti na weye. Tunapaswa pia kujikaza kuachana kabisa na mawazo yoyote ya ubaguzi yenye pengine tuko nayo.—Soma 1 Petro 2:17.a
3. Utafanya nini kama unakosana na Mukristo mwenzako?
Ni kweli kama tuko na umoja, lakini hatuko wakamilifu. Wakati fulani tunakwazaka wengine ao hata kuwaumiza. Biblia inatuambia hivi: “Muendelee . . . kusameheana.” Inasema tena hivi: “Kama vile Yehova aliwasamehe ninyi kwa kupenda, ninyi pia munapaswa kufanya vilevile.” (Soma Wakolosai 3:13.) Tulishakakosea Yehova mara mingi sana. Lakini, anakuwaka tayari kutusamehe. Njo maana anapenda na siye tukuwe nasamehe ndugu na dada zetu. Kama unatambua kuwa ulishakwaza mutu fulani, uone namna unaweza kufanya juu muelewane tena.—Soma Matayo 5:23, 24.b
TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
Tuone mambo yenye na weye unaweza kufanya juu ya kuendelesha amani na umoja mu kutaniko.
Utafanya nini juu ya kuendelesha amani?
4. Achana na ubaguzi
Tunajua kama tunapaswa kupenda ndugu zetu wote. Lakini, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kupenda mutu mwenye anaonekana kuwa tofauti na siye. Nini njo inaweza kutusaidia? Musome Matendo 10:34, 35, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Yehova anakubali watu wa namna zote wakuwe Mashahidi wake. Kujua vile kunapaswa kukuchochea ukuwe na mawazo gani juu ya watu wenye wako tofauti na weye?
Fasi kwenye unaishi, watu wanazoea kubagua watu wa namna gani?
Musome 2 Wakorinto 6:11-13, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Unaweza kufanya nini juu ufikie kupenda ndugu na dada wote?
5. Ukuwe tayari kusamehe na kufanya amani
Yehova anakuwaka tayari kutusamehe, hata kama hakuna siku yenye atatukoseaka juu na siye tumusamehe. Musome Zaburi 86:5, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Nini njo inaonyesha kama Yehova anapenda kutusamehe?
Juu ya nini unafurahi kujua kama Yehova anakuwaka tayari kusamehe?
Ni mambo gani inaweza kufanya ikuwe nguvu kusikilizana na wengine?
Namna gani tunaweza kumuiga Yehova na kuendelea kuishi kwa umoja na ndugu na dada zetu? Musome Mezali 19:11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Kama mutu anakukwaza ao anakukasirisha, unaweza kufanya nini juu hali ikuwe muzuri?
Wakati fulani tunakwazaka wengine. Kama ile jambo inatokea, tunapaswa kufanya nini? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.
Vile uliona mu video, ule dada alifanya nini juu asikilizane tena na dada mwenzake?
6. Tafuta sifa za muzuri za ndugu na dada
Kadiri tunapitisha wakati mingi pamoja na ndugu na dada zetu, tunafikia kujua sifa zao na uzaifu wao. Nini njo inaweza kutusaidia tukaze akili yetu juu ya sifa zao za muzuri? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.
Nini njo inaweza kukusaidia uone sifa za muzuri za ndugu na dada?
Yehova anaangaliaka zaidi sana sifa zetu za muzuri. Musome 2 Mambo ya Nyakati 16:9a, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Yehova anaangaliaka zaidi sana sifa zetu za muzuri. Ile inakufanya ujisikie namna gani?
Hata diama ya kupendeza inakuwaka na kasoro, lakini ile haipunguzake bei yake. Vilevile, ndugu na dada zetu wako na uzaifu mbalimbali, lakini Yehova anawaona kuwa wa maana sana
WATU FULANI WANASEMAKA: “Juu nisamehe mutu, anapaswa kwanza kunilomba huruma.”
Juu ya nini tunapaswa kuwa tayari kusamehe wengine?
KWA KIFUPI
Unaweza kusaidia kuendelesha umoja mu kutaniko kama unajikaza kusamehe na kupenda ndugu na dada zako wote.
Maulizo ya kujikumbusha
Unaweza kufanya nini juu ya kuachana kabisa na ubaguzi?
Utafanya nini kama hauelewane na Mukristo mwenzako?
Juu ya nini unapenda kusamehe wengine sawa vile Yehova anafanyaka?
HABARI ZINGINE
Ona namna mufano fulani wenye Yesu alitoa unaweza kutusaidia kuepuka kuhukumu wengine.
Ni lazima tuombe musamaha hata kama tunawaza kuwa hatukufanya kosa yoyote?
“Kuomba Musamaha Kunasaidiaka Kufanya Amani” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 11, 2002)
Ona namna watu fulani wamejifunza kutendea wengine bila ubaguzi.
a Mafasirio Ingine ya 6 inaonyesha namna upendo unachochea Wakristo waepuke kuambukiza wengine magonjwa ya kuambukiza.
b Mafasirio Ingine ya 7 inaonyesha namna tunaweza kushugulikia matatizo ya kukosa kuelewana mu mambo ya biashara na mu mambo ya sheria.