Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lmd somo 4
  • Unyenyekevu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unyenyekevu
  • Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Yenye Paulo Alifanya
  • Mufano wa Paulo Unatufundisha Nini?
  • Umuige Paulo
  • Yehova Anaona Watumishi Wake Wanyenyekevu Kuwa wa Maana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Yesu Alituachia Mufano Wa Unyenyekevu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Tuonyeshe Sifa Zenye Kumupendeza Mungu—Unyenyekevu
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Usijifikirie Mwenyewe Sana Kuliko Vile Inaomba Kufikiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
lmd somo 4

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

Mutume Paulo iko mwenye kufungwa munyororo. Kwa heshima anaongea na Mufalme Agripa, Gavana Festo, na Bernike.

Mdo. 26:2, 3

SOMO YA 4

Unyenyekevu

Kanuni: “Kwa unyenyekevu muone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko ninyi.”​—Flp. 2:3.

Mambo Yenye Paulo Alifanya

Mutume Paulo iko mwenye kufungwa munyororo. Kwa heshima anaongea na Mufalme Agripa, Gavana Festo, na Bernike.

VIDEO: Paulo Anahubiria Mufalme Agripa

1. Angalia VIDEO, ao usome Matendo 26:2, 3. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1. Namna gani Paulo alionyesha unyenyekevu wakati alikuwa nazungumuza na Mufalme Agripa?

  2. Namna gani Paulo alimusaidia afikirie zaidi Yehova na Maandiko kuliko kumufikiria yeye?​—Ona Matendo 26:22.

Mufano wa Paulo Unatufundisha Nini?

2. Wakati tunazungumuza na watu kwa unyenyekevu na heshima, watafurahia zaidi ujumbe wetu.

Umuige Paulo

3. Uepuke kujionyesha. Wakati uko nazungumuza na mutu, usifanye ionekane sawa vile weye njo unajua kila kitu na kama ule mwenye uko naongea naye hajue kitu. Zungumuza naye kwa heshima.

4. Onyesha kabisa kama kweli zenye uko nafundisha zinatoka njo mu Biblia. Mu Neno ya Mungu muko mawazo yenye inaweza kugusa mioyo ya watu. Wakati tunaitumikisha, tutawasaidia wakuwe na imani ya kweli yenye inategemea Neno ya Mungu.

5. Ukuwe mupole. Usikaze mutu aitike mambo yenye unasema. Hatupende kubishana. Onyesha unyenyekevu kwa kubakia kimya ao kuondoka kama inafaa. (Mez. 17:14; Tit. 3:2) Tendo ya upole inaweza kufanya ule mutu akubali kuzungumuza na siye hata wakati ingine.

ONA PIA

Ro. 12:16-18; 1 Ko. 8:1; 2 Ko. 3:5

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine