Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lmd somo 12
  • Uhodari

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uhodari
  • Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Yenye Yesu Alifanya
  • Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?
  • Umuige Yesu
  • Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • “Kwa Hiyo, Muende, na Mufanye Wanafunzi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
lmd somo 12

KUFANYA WANAFUNZI

Yesu iko nazungumuza kwa uchangamufu na mwanaume mwenye anapiga magoti mbele yake na wanafunzi wake.

Mk. 10:17-22

SOMO YA 12

Uhodari

Kanuni: “Mafuta na uvumba vinafurahisha moyo, ni vile pia urafiki mutamu wenye unatokana na shauri la unyoofu.”​—Mez. 27:9.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

Yesu iko nazungumuza kwa uchangamufu na mwanaume mwenye anapiga magoti mbele yake na wanafunzi wake.

VIDEO: Yesu Anashauria Mutawala Mumoya Kijana Mwenye Alikuwa Tajiri

1. Angalia VIDEO, ao usome Marko 10: 17-22. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1. Pengine Yesu aliona sifa gani za muzuri kwa ule mutawala kijana?

  2. Juu ya nini iliomba Yesu akuwe na upendo na uhodari juu amushaurie ule kijana?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Juu mutu afanye maendeleo ya kiroho, ni kweli tunapaswa kuzungumuza naye kwa upendo; lakini tunapaswa pia kuzungumuza naye waziwazi, ikiwa inaomba afanye mabadiliko fulani.

Umuige Yesu

3. Saidia mwanafunzi ajiwekee miradi na kuitimiza.

  1. Tumikisha sehemu “Pima Kufanya Hivi” mu kila somo ya kitabu Furahia Maisha Milele!

  2. Saidia mwanafunzi wako ajue mambo yenye anapaswa kufanya juu atimize miradi ya wakati mufupi na ya wakati murefu.

  3. Kila mara umupongeze juu ya maendeleo yenye iko nafanya.

4. Tambua magumu yenye inazuia mwanafunzi wako kufanya maendeleo na umusaidie aipiganishe.

  1. Ujiulize hivi:

    • ‘Kama hafanye maendeleo juu afikie kubatizwa, pengine nini njo iko namuzuia?’

    • ‘Naweza kufanya nini juu ya kumusaidia?’

  2. Umuombe Yehova akupatie uhodari juu uzungumuze naye waziwazi na kwa upendo kuhusu mabadiliko yenye anapaswa kufanya.

5. Kama mwanafunzi hafanye maendeleo, musimamishe funzo.

  1. Unaweza kujua kama mwanafunzi hafanye maendeleo kwa kujiuliza hii maulizo:

    • ‘Huyu mwanafunzi anatumikishaka mambo yenye iko najifunza?’

    • ‘Anaendaka ku mikutano na kuambia watu wengine mambo yenye iko najifunza?’

    • ‘Kisha kujifunza naye kwa wakati fulani, anaonyesha kama anapenda kuwa Shahidi wa Yehova?’

  2. Kama mwanafunzi wa Biblia hapendi kufanya maendeleo ya kiroho:

    • Umuambie afikirie mambo yenye iko namuzuia.

    • Kwa heshima umuambie juu ya nini unapenda musimamishe funzo.

    • Umuambie maendeleo yenye anapaswa kufanya juu muanze tena kujifunza.

ONA PIA

Zb. 141:5; Mez. 25:12; 27:6; 1 Ko. 9:26; Kol. 4:5, 6

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine