Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w11 1/12 uku. 3
  • Je, Mungu Anatuadhibu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Mungu Anatuadhibu?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Biblia Inasema Nini Juu ya Misiba ya Asili?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Misiba ya Asili—Kwa Nini Imeongezeka Sana?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Kukabiliana na Misiba ya Asili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 1/12 uku. 3

Je, Mungu Anatuadhibu?

“Nafikiri hii ni tembatsu (adhabu kutoka kwa Mungu), ingawa ninawasikitikia watu walioathiriwa na msiba huo,” akasema kiongozi mmoja wa kisiasa nchini Japani baada ya nchi hiyo kukumbwa na tsunami na tetemeko la ardhi la kipimo cha 9.0 mwezi wa Machi 2011.

Baada ya watu zaidi ya 220,000 kufa katika tetemeko la ardhi nchini Haiti mwezi wa Januari 2010, kasisi fulani maarufu, anayehubiri kwenye televisheni, alidai kwamba watu hao walikufa kwa sababu “walikuwa wamefanya mkataba na ibilisi” na walihitaji “kumrudia mungu.”

“Mungu anataka kuamsha dhamiri zetu zilizokufa ganzi,” akatangaza kasisi mmoja Mkatoliki wakati watu 79 walipokufa katika msongamano wa watu huko Manila, Ufilipino. Gazeti moja nchini humo lilisema kwamba “asilimia 21 ya watu wazima wanaamini kwamba Mungu anaonyesha hasira yake kupitia maporomoko ya ardhi, vimbunga na misiba mingine” inayotokea mara kwa mara katika nchi hiyo.

WAZO la kwamba Mungu anatumia misiba kuwaadhibu watu wabaya si jipya. Mwaka wa 1755, baada ya watu 60,000 hivi kuangamizwa na tetemeko la ardhi, moto, na tsunami iliyokumba jiji la Lisbon, Ureno, mwanafalsafa maarufu Voltaire aliuliza: “Je, uovu ulikuwa umejaa Lisbon, kuliko Paris, ambako watu wanajifurahisha sana kwa anasa zilizopotoka?” Kwa kweli, mamilioni ya watu wamejiuliza kama Mungu anatumia misiba ya asili kuwaadhibu watu. Katika nchi nyingi, misiba hiyo inaitwa kazi ya Mungu.

Kwa kuzingatia hali hizo, tunahitaji kujiuliza: Je, kweli Mungu amekuwa akitumia misiba ya asili kuwaadhibu watu? Je, kuongezeka kwa misiba katika nyakati za hivi karibuni ni adhabu kutoka kwa Mungu?

Wanapokimbilia kumlaumu Mungu, wengine wanataja masimulizi ya Biblia yanayoonyesha jinsi Mungu alivyoleta uharibifu akitumia nguvu za asili. (Mwanzo 7:17-22; 18:20; 19:24, 25; Hesabu 16:31-35) Hata hivyo, tunapochunguza kila tukio katika masimulizi hayo ya Biblia, tunaona mambo matatu ya pekee. Kwanza, onyo lilitolewa mapema. Pili, tofauti na misiba ya asili inayotokea leo, ambayo inasababisha vifo vya watu wazuri kwa wabaya, uharibifu uliosababishwa na Mungu ulitenganisha wazuri na wabaya. Watu waovu kabisa au wale waliokataa kusikiliza maonyo ndio tu walioangamizwa. Tatu, Mungu aliandaa njia ili watu wasio na hatia waponyoke.—Mwanzo 7:1, 23; 19:15-17; Hesabu 16:23-27.

Katika misiba mingi sana ambayo imesababisha vifo vya mamilioni ya watu leo, hakuna uthibitisho wowote unaoonyesha kwamba Mungu ndiye anayeisababisha. Basi, kwa nini misiba hiyo imeongezeka sana? Tunawezaje kukabiliana nayo? Na je, kuna wakati ambapo misiba haitakuwapo tena? Utapata majibu katika makala zinazofuata.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine