Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/7 uku. 3
  • Je, Kuna Yule Anayesikiliza Sala?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Kuna Yule Anayesikiliza Sala?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Watu Fulani Hawaamini Kama Mungu Iko?
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Kumukaribia Mungu Karibu Katika Sala
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Utangulizi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/7 uku. 3

Je, Kuna Yule Anayesikiliza Sala?

“Zamani, sikuamini kama Mungu iko. Hata hivyo, wakati fulani nilikuwa nikisali. Sikuwa na uhakika kama kuna yule anayesikiliza sala zangu, lakini ndani yangu nilijisikia kuwa kuna yule anayesikiliza. Sikuwa na furaha na sikuwa na kusudi lolote katika maisha. Sikutaka kuamini kama Mungu iko kwa sababu nilikuwa nawaza kama ni watu wa hali ya chini tu ndio waliamini kama Mungu iko.”​—PATRICIA,a WA HUKO IRLANDE.

JE, UMEKWISHA kuwaza na kujisikia kama Patricia? Je, unasali hata ikiwa hauamini kama Mungu iko? Kama ni hivyo, ujue kama hauko peke yako. Ona mifano miwili inayofuata.

◼ Uchunguzi fulani uliofanywa juu ya wanainchi 2200 wa Angleterre ulionyesha kama kati ya watu hao, watu 484 tu ndio walioamini kama kuna Mungu ambaye ni roho aliyeumba dunia na anayesikiliza sala zetu. Lakini, kati ya watu hao waliochunguzwa, watu 1210 wanasali wakati fulani.

◼ Uchunguzi mwengine ulifanywa juu ya watu 10 000 kutoka kontinenti ine. Karibu 30% ya watu waliosema hawaamini kama Mungu iko, walikuwa wanasali.

Sababu Gani Watu Fulani Hawaamini Kama Mungu Iko?

Mutu mumoja wa Angleterre anayeitwa Allan anasema hivi: “Sikuamini kama Mungu iko kwa sababu niliwaza kama dini iliundwa ili kutawala watu na kuwaiba feza zao. Tena niliwaza hivi, ikiwa Mungu iko, hakungepaswa kuwa mambo mengi ya ukosefu wa haki kama ilivyo. Lakini, wakati fulani nilikuwa nikikaa kimya na kuanza kuzungumuza tu na kitu ao mutu fulani. Na nilikuwa nikijiuliza hivi, ‘Sababu gani niko hapa duniani?’”

Haishangaze ikiwa mutu aliye na mawazo kama hayo anasema kama haamini kwamba sala zinajibiwa. Watu wengi hawaamini kama Mungu iko kwa sababu wanakosa majibu kwa maulizo kama haya:

◼ Je, kuna Muumbaji?

◼ Sababu gani mara nyingi dini inachochea watu wafanye mambo mabaya?

◼ Sababu gani Mungu anawaacha watu wateseke?

Ikiwa unapata majibu kwa maulizo hayo, je, utaamini kama kuna yule anayesikiliza sala?

[Maelezo ya chini]

a Majina fulani yamebadilishwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine