Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/10 uku. 4-5
  • Sababu Gani Rushwa Haiishe?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Rushwa Haiishe?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Rushwa Itaisha!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Shetani
    Amuka!—2013
  • Rushwa Yenye Kuwa mu Serikali Itaishaka?
    Habari Zingine
  • Ufalme wa Mungu—Serikali Yenye Haina Rushwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/10 uku. 4-5

Sababu Gani Rushwa Haiishe?

‘Mwanadamu amemutawala mwanadamu kwa kumuumiza.’​—MHUBIRI 8:9.

MANENO hayo yanaeleza vizuri historia ya utawala wa watu. Utawala wa watu umeleta mateso na huzuni nyingi. Sikuzote, watu wenye nia nzuri ambao wamejaribu kusaidia wengine wafuatie haki wamezuiwa na watu wenye tamaa na wenye kupenda rushwa. Sababu gani hivyo? Sababu gani rushwa haiishe? Kwa sababu ya vishawishi vitatu vinavyofuata:

1. Zambi.

Biblia inasema waziwazi kama sisi ‘wote tuko chini ya zambi.’ (Waroma 3:9) Zambi ‘inakaa’ ndani yetu kama vile ugonjwa ulioritiwa usioweza kupona. Kwa maelfu ya miaka, zambi ‘imetawala’ kama mufalme juu ya watu. “Sheria” ya zambi inaendelea kutenda ndani yetu. Mielekeo ya zambi inawasukuma watu wengi watafute faida zao wenyewe ao kufuatilia sana utajiri ao mamlaka bila kuhangaikia wengine.​—Waroma 5:21; 7:17, 20, 23, 25.

2. Ulimwengu muovu ambamo tunaishi.

Ulimwengu huu unajaa tamaa na kujipendelea sana. Katika hali hiyo, watu fulani wanaona kama ni vigumu kuwa tofauti na watu wengine. Kwa sababu ya kutaka mambo makubwa, wanatamani sana mamlaka. Tena, wanatamani kuwa na feza nyingi na vitu vya kimwili kupita vile wanavyohitaji kabisa. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba wanatenda kwa njia isiyofaa ili kutimiza miradi yao. Kuliko kuzuia tamaa mbaya, watu hao ‘wanafuata umati kwa ajili ya makusudio maovu.’​—Kutoka 23:2.

3. Shetani Ibilisi.

Shetani, kiumbe wa roho muasi, ‘anaipotosha dunia nzima inayokaliwa.’ (Ufunuo 12:9) Anafanya yote awezayo ili kudanganya watu. Anaweza kutumia kwa mayele tamaa ya kawaida ya mutu ya kuwa na vitu vya kimwili ao feza ili kumusukuma atende kwa udanganyifu.

Je, hilo linamaanisha kama sisi ni kama vyombo katika mikono ya Shetani ambavyo anaweza kutumia namna anavyopenda? Tutaona jibu katika habari inayofuata.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine