Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/1 uku. 16
  • Jina la Mungu Ni Nani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jina la Mungu Ni Nani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jina la Mungu
    Amuka!—2017
  • Sababu Gani Tunapaswa Kulitumia Jina la Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Unajua Jina la Mungu na Unalitumia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Jina la Mungu—Je, Inafaa Tulitumie? Maana ya Jina Hilo Ni Nini
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/1 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Jina la Mungu Ni Nani?

Watu wote wa familia yetu wana majina ya pekee. Hata wanyama wa kufugwa wana majina. Je, hauone kama ni jambo lenye kupatana na akili kusema kama Mungu ana jina? Katika Biblia, Mungu ana majina mengi ya cheo, kama vile Mungu Mweza-Yote, Bwana Mutawala Mukubwa, na Muumbaji, lakini pia ana jina lake la pekee.​—Soma Isaya 42:8.

Tafsiri nyingi za Biblia zinaonyesha jina la Mungu la pekee katika Zaburi 83:18. Kwa mufano, katika Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, andiko hilo linasema hivi: “Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”

Sababu gani tunapaswa kutumia jina la Mungu?

[Picha katika ukurasa wa 16]

Tunatumia majina ya pekee tunapozungumuza na watu tunaowapenda, kwa mufano marafiki ambao tunapendana nao sana

Mungu anataka tutumie jina lake la pekee. Tunatumia majina ya pekee tunapozungumuza na watu tunaowapenda, kwa mufano marafiki ambao tunapendana nao sana, zaidi sana ikiwa wanatuomba tufanye hivyo. Je, hauone kama ni vizuri pia kutumia jina la pekee la Mungu tunapozungumuza naye? Zaidi ya hilo, Yesu Kristo alitutia moyo tutumie jina la pekee la Mungu.​—Soma Mathayo 6:9; Yohana 17:26.

Hata hivyo, ili tuwe marafiki wa Mungu, tunahitaji kujua mambo mengi juu yake kuliko tu kujua jina lake. Kwa mufano, Mungu ni mutu wa namna gani? Je, inawezekana kabisa kumukaribia? Unaweza kupata majibu ya maulizo hayo katika Biblia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine