Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 15/3 uku. 18
  • Unafarijiwa ili Uwafariji Wengine

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unafarijiwa ili Uwafariji Wengine
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • HANGAIKIA SANA WALE WANAOTESEKA
  • ‘Wafariji Wote Wanaoomboleza’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mtegemee Yehova, “Mungu wa Faraja Yote”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Namna Mungu Anatolea Watu Kitulizo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Namna ya Kufariji Wale Wenye Wametendewa Mubaya Kingono
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 15/3 uku. 18

Unafarijiwa ili Uwafariji Wengine

Kwa kuwa sisi wote ni wanadamu wasio wakamilifu, tunagonjwa, na wengine hata kati yetu wana magonjwa ya hatari sana. Tunapopatwa na matatizo kama hayo, ni jambo gani linaloweza kutusaidia tusikate tumaini?

Jambo moja linaloweza kutusaidia sana ni faraja ambayo watu wa familia yetu, marafiki wetu, na Mashahidi wenzetu wanatutolea.

Maneno yenye fazili na upendo ya rafiki fulani yanaweza kuwa kama mafuta yenye kutuliza na kuburudisha. (Met. 16:24; 18:24; 25:11) Lakini Mukristo wa kweli hafikiri kwamba yeye tu ndiye ana lazima ya kufarijiwa. Mukristo wa kweli anajikaza pia ‘kuwafariji wale walio katika namna yoyote ya ziki kupitia faraja ambayo yeye mwenyewe anafarijiwa na Mungu.’ (2 Kor. 1:4; Lu. 6:31) Ndugu Antonio, mwangalizi wa wilaya katika Mexique, alijionea jambo hilo.

Walipomupata na ugonjwa unaoitwa lymphome, aina ya kansere ya damu, alihangaika sana. Hata hivyo, yeye alijikaza kuzuia mawazo mabaya yasivuruge akili yake. Alifanya nini? Alijaribu kukumbuka nyimbo za Ufalme, aliziimba na kutafakari juu ya maneno ya nyimbo hizo. Jambo lingine lililomufariji sana ni hili: alikuwa anasali na kusoma Biblia kwa sauti.

Hata hivyo, ndugu Antonio anatambua kama musaada mukubwa kabisa ulitoka kwa Mashahidi wenzake. Anasema hivi: “Bibi yangu nami tulipohangaishwa na jambo hilo, tulimuita mutu mumoja wa jamaa yetu ambaye ni muzee wa kutaniko ili aje kusali pamoja nasi. Hilo lilitufariji na kufanya tutulie. Kwa kweli, kwa sababu ya kutegemezwa na watu wa familia yetu na Mashahidi wenzetu, katika muda mufupi, tuliweza kushinda mawazo mabaya yaliyokuwa yanavuruga akili zetu.” Alishukuru sana kuwa na marafiki hao wenye kuwapenda na kuwahangaikia!

Musaada mwengine wakati wa taabu ni roho takatifu ambayo Mungu ametuahidi. Mutume Petro alisema kama roho takatifu ya Mungu ni “zawadi ya bure” ao ya bila malipo. (Mdo. 2:38) Maneno yake yalionekana kuwa ya kweli wakati wa Pentekoste ya mwaka wa 33, wakati wengi walitiwa mafuta kwa roho. Zaidi ya watiwa-mafuta, sisi wote tunaweza kufaidika na zawadi hiyo. Zawadi hiyo inaendelea kutolewa bila mwisho, kwa hiyo, tunakutia moyo uendelee kuiomba kwa uwingi.​—Isa. 40:28-31.

HANGAIKIA SANA WALE WANAOTESEKA

Mutume Paulo alivumilia taabu nyingi, na wakati fulani alipambana hata na kifo. (2 Kor. 1:8-10) Hata hivyo, mutume Paulo hakuogopea uzima wake kupita kiasi. Wazo la kwamba Mungu alimutegemeza, lilimufariji. Aliandika hivi: ‘Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, Baba ya rehema nyororo na Mungu wa faraja yote, ambaye anatufariji katika ziki yetu yote.’ (2 Kor. 1:3, 4) Mutume Paulo hakuruhusu magumu yake yamulemee. Tofauti na hilo, majaribu aliyovumilia yalimusaidia akomalishe sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine, kwa hiyo aliweza kuwafariji wengine wakati walikuwa na lazima ya kufarijiwa.

Ndugu Antonio, alipona na akarudilia kazi yake ya mwangalizi mwenye kusafiri. Ni kweli kwamba alikuwa anawahangaikia ndugu na dada kwa ukawaida, lakini kuanzia wakati huo, yeye na bibi yake wamejikaza kwa njia ya pekee kutembelea na kutia moyo wagonjwa. Kwa mufano, kisha kumutembelea Mukristo mumoja aliyekuwa mugonjwa sana, Antonio alisikia kwamba ndugu huyo hakupenda kuenda kwenye mikutano. Antonio anaeleza hivi: “Si kwamba hakuwa anapenda Yehova na ndugu na dada, lakini ugonjwa wake ulimuvunja moyo hivi kwamba alijiona kuwa wa bure.”

Jambo moja ambalo ndugu Antonio alifanya ili kumutia ndugu huyo moyo, alimualika kwenye karamu ndogo ya kirafiki waliofanya hivi karibuni na akamujulisha kwamba ni yeye atatoa sala. Ijapokuwa ndugu huyo aliona kwamba hastahili, alikubali mualiko huo. Antonio anaeleza hivi: “Ndugu huyo alitoa sala nzuri kabisa, na kisha hapo, akabadilika kabisa, akajisikia tena kuwa wa maana.”

Kwa kweli, sisi wote tumekuwa na wakati wa taabu kwa kiasi kikubwa ao kidogo. Lakini kama vile mutume Paulo alivyosema, kupitia hali hiyo kunaweza kutusaidia tujue namna ya kuwafariji wengine wakati wana taabu. Kwa hiyo, tuwe tayari kuwafariji Wakristo wenzetu na tumuige Yehova Mungu kwa kuwa chanzo cha faraja kwa wengine.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine