Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/6 uku. 3-4
  • Chuki Ni Tatizo Linaloenea Katika Dunia Yote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Chuki Ni Tatizo Linaloenea Katika Dunia Yote
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • CHUKI NI TATIZO LA MUTU MWENYEWE
  • Dunia Isiyokuwa na Chuki Itakuwa Wakati Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Umeambukizwa na Tabia ya Ubaguzi?
    Amuka!—2020
  • Sisi Wote Tukuwe na Umoja Kama Vile Yehova na Yesu Wako na Umoja
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Mafundisho ya Mungu Yanamaliza Chuki
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/6 uku. 3-4
[Picha katika ukurasa wa 3]

KICHWA: DUNIA ISIYOKUWA NA CHUKI​—ITAKUWA WAKATI GANI?

Chuki Ni Tatizo Linaloenea Katika Dunia Yote

JONATHAN, Muamerika wa asili ya Korea, alichukiwa kwa sababu ya rangi yake ya ngozi alipokuwa mutoto. Alipokuwa akikomaa, alitafuta mahali ambapo watu hawangemuchukia kwa sababu ya sura yake ao rangi yake ya ngozi. Akawa muganga katika muji fulani kaskazini mwa Alaska, huko Amerika, ambako hali yake ya inje ilifanana sana na ile ya wagonjwa wengi aliokuwa akitunza. Alitumaini kwamba, labda huko, katikati ya upepo wenye baridi sana wa Arktiki, ataepuka matokeo mabaya zaidi ya chuki.

Tumaini lolote kama hilo lilivunjwa wakati alimutunza mwanamuke mumoja mwenye miaka 25. Mugonjwa huyo alipotoka katika hali yake ya kupoteza ufahamu, alimuangalia Jonathan kwenye uso na akamuambia maneno ya zarau, hivyo akafunua chuki kali aliyokuwa nayo moyoni kuelekea Wakorea. Jambo hilo lilimukumbusha Jonathan kwa huzuni nyingi kwamba bidii zote alizofanya ili kuhama na kukubaliwa na Waeskimo hazingemusaidia kuepuka chuki.

Jambo hilo ambalo lilimupata Jonathan linaonyesha ukweli wenye kuhuzunisha sana. Katika kila sehemu ya dunia, watu wana chuki. Inaonekana kwamba mahali popote ambako kuna watu, kuna chuki.

Hata hivyo, ijapokuwa chuki inaenea sana, watu wengi wanapinga chuki. Hilo ni jambo ambalo halieleweke. Inawezekana namna gani jambo ambalo watu hawapendi lienee katika dunia yote? Ni wazi kwamba watu wengi ambao wanapinga chuki wanashindwa kutambua kwamba wao wenyewe wana chuki ndani yao. Je, wewe pia una tatizo hilo? Unaweza kujibu ulizo hilo namna gani?

CHUKI NI NINI?

Watu wanaotafuta habari kuhusu mambo mbalimbali wanajikaza kueleza maana ya neno chuki. Wamoja wao wanasema kwamba chuki ni “maoni yasiyofaa ao namna mutu anajisikia moyoni kuelekea mutu fulani kwa sababu tu mutu huyo ni wa kikundi fulani cha watu.” Wengine wanasema kwamba maoni hayo yanategemea “kukosa habari za kutosha” juu ya kikundi fulani cha watu, na jambo hilo linafanya mutu “atangulie kuwa na maoni yasiyofaa juu ya watu wa kikundi hicho.” Kwa vyovyote vile, mutu anaweza kumuchukia mutu mwengine kwa sababu ya rangi yake ya ngozi, kimo chake, luga yake, dini yake, kwa sababu yeye ni mwanaume ao mwanamuke, ao kwa sababu ya jambo lingine lolote linalomufanya mutu huyo aonekane kuwa tofauti na wengine.

CHUKI NI TATIZO LA MUTU MWENYEWE

Iwe tunatambua hivyo ao hapana, ni vigumu kwetu kujua ikiwa mioyo yetu inajaa chuki. Biblia inaeleza sababu inaposema hivi: ‘Moyo ni mudanganyifu kuliko vitu vyote.’ (Yeremia 17:9) Kwa hiyo, tunaweza kujidanganya kwa kuamini kwamba tunawavumilia watu wa aina zote. Ao tunaweza kujitetea kwamba tuna sababu nzuri ya kuwa na mawazo mabaya juu watu wa makabila fulani.

[Picha katika ukurasa wa 4]

Utajisikia namna gani ikiwa unakutana na hali kama hii?

Ili kuonyesha kwamba ni vigumu kutambua ikiwa tuna chuki inayojificha ndani ya moyo wetu, wazia hali inayofuata: Unatembea katika barabara usiku wenye giza ukiwa peke yako. Vijana wanaume wawili ambao haujaona hata siku moja wanakuja mbele yako. Wanaonekana kuwa wenye nguvu, na mumoja wao anaonekana kuwa na kitu fulani katika mukono wake.

Je, utafikia uamuzi wa kwamba vijana hao ni watu hatari kwako? Kwa kweli, mambo yaliyokupata katika maisha yako yanaweza kukufanya uwe mwangalifu, lakini je, kwa kweli mambo hayo uliyojionea yanahakikisha kwamba vijana hao wawili ni hatari kwako? Labda unaweza kujiuliza ulizo hili la kujichunguza, Ninawazia vijana hao wanaume kuwa wa rangi ao kabila gani? Jibu lako kwa ulizo hilo linaweza kufunua mambo yaliyo ndani ya moyo wako. Linaweza kuonyesha kwamba, kwa kadiri fulani, tayari moyo wako umekwisha kuingiwa na chuki.

Ikiwa tunajijua vizuri kabisa, tunapaswa kukubali kabisa ndani ya moyo wetu kwamba sisi wote tuna kiasi fulani cha chuki katika njia moja ao nyingine. Hata Biblia inazungumuzia aina fulani ya chuki iliyo ya kawaida kwa watu wengi inaposema hivi: “Mwanadamu huona kile kinachoonekana kwa macho.” (1 Samweli 16:7) Kwa sababu sisi wote tuna mwelekeo huo wa kibinadamu, ambao mara nyingi unaleta matokeo mabaya, je, kuna tumaini lolote kwamba tunaweza kushinda ao kuondoa chuki katika maisha yetu? Na je, kutakuwa wakati ambapo chuki itaisha katika dunia yote?

CHUKI INAENEA KATIKA DUNIA YOTE

Kanada: “Ijapokuwa [inchi] hiyo imekuwa na imeanzisha mipango mbalimbali ya kisheria na kanuni ili kulinda haki za makabila mbalimbali, ubaguzi wa rangi linaendelea kuwa tatizo nzito kuhusiana na haki za wanadamu.”​—Maelezo juu ya Kanada ya mwaka wa 2012 ya Shirika la Kimataifa Linalotetea Haki za Wanadamu, Amnesty International.

Ulaya: “Wazungu wa Ulaya [makumi ine na munane] juu ya mia moja wanaamini kwamba ni bidii chache sana ndiyo inafanywa ili kumaliza ubaguzi katika inchi zao.”​—Ripoti ya Ulaya ya Mwaka wa 2011 Kuhusu Kukosa Kukubali ao Kuvumilia Watu Wengine, Chuki, na Ubaguzi.

Afrika: “Matendo ya jeuri na ubaguzi juu ya wanawake yanaenea katika inchi nyingi.”​—Ripoti ya Mwaka wa 2012 ya Shirika la Kimataifa Linalotetea Haki za Wanadamu, Amnesty International.

Nepal: “Wadali (“wahindu wa hali ya chini”) wanasumbuliwa kwa sababu ya ubaguzi mukali sana, hasa katika mambo ya kifeza, ya kijamii, na ya kiasili.”​—Ripoti ya Mwaka wa 2012 ya Shirika la Kimataifa Linalotetea Haki za Wanadamu.

Ulaya ya Mashariki: “Watu kusingiziwa katika inchi za kigeni, watu kutendewa kwa chuki nyumbani, na kubaguliwa kwa Waroma wa Ulaya ya Mashariki, yote hayo ni matatizo ambayo hakuna mwanasiasa anayetaka kuyatatua.”​—Gazeti The Economist, tarehe 4 Mwezi wa 9, 2010.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine