Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 15/1 uku. 17-21
  • Kijana, Chukua Maamuzi Yenye Hekima

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kijana, Chukua Maamuzi Yenye Hekima
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UAMUZI WA MAANA SANA KATIKA MAISHA YAKO
  • UTAFANYA NINI KATIKA UJANA WAKO?
  • KANUNI TATU ZA KUKUONGOZA
  • TUMIA KANUNI ZA BIBLIA ILI KUCHUKUA MAAMUZI YENYE HEKIMA
  • FURAHIA KUWA KIJANA MUKRISTO
  • Watoto Wako Watamutumikia Yehova Wakati Watakomaa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Na Atimize Mipango Yako Yote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Onyesha Imani—kwa Kukamata Maamuzi Yenye Hekima!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Wapi njo Tunaweza Kupata Muongozo Wenye Kutumainika Leo?
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 15/1 uku. 17-21
Mutume Paulo na Timotheo katika mashua

Kijana, Chukua Maamuzi Yenye Hekima

‘Enyi vijana nanyi mabikira pia . . . mulisifu jina la Yehova.’​—ZAB. 148:12, 13.

UNAWEZA KUELEZA?

  • Vijana wanapaswa kuchukua maamuzi gani sasa yatakayowaongoza kwenye mapendeleo mengine katika kazi ya Yehova wakati ujao?

  • Vijana fulani wamemutumikia Yehova namna gani?

  • Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kukusaidia uchukue maamuzi mazuri zaidi katika maisha?

1. Ni mambo gani yenye kufurahisha ambayo vijana wengi Wakristo wanafanya leo?

TUNAISHI katika kipindi cha maana sana. Kuliko wakati mwingine wowote, leo mamilioni ya watu wa mataifa yote wanajiunga na ibada ya kweli. (Ufu. 7:9, 10) Vijana wengi wanaendelea kupata matokeo yenye kufurahisha wanapowasaidia wengine waelewe mafundisho ya Biblia yenye kuokoa maisha. (Ufu. 22:17) Vijana fulani wanaongoza mafunzo ya Biblia na kusaidia watu wawe na maisha yenye kumupendeza Mungu. Wengine wanahubiri kwa bidii habari njema katika maeneo ya luga za kigeni. (Zab. 110:3; Isa. 52:7) Namna gani unaweza kufanya mengi zaidi katika kazi ya Yehova?

2. Namna gani mufano wa Timotheo unaonyesha kwamba Yehova iko tayari kuwatolea vijana mapendeleo ya utumishi? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

2 Kijana, unaweza kuchukua maamuzi fulani ambayo yanaweza kukuongoza baadaye kwenye mapendeleo mengine katika kazi ya Mungu. Kwa mufano, Timotheo aliyeishi Listra alichukua maamuzi yenye hekima; kwa hiyo alistahili kupewa mugawo wa kuwa misionere alipokuwa na miaka 20 hivi. (Mdo. 16:1-3) Inaonekana kwamba miezi fulani tu hapo mbele, kisha Paulo kulazimishwa kuacha kutaniko mupya la Thesalonike kwa sababu ya upinzani mukali, alimupatia Timotheo mugawo wa kurudi Thesalonike ili kuwatia ndugu moyo. (Mdo. 17:5-15; 1 Thes. 3:1, 2, 6) Unafikiri Timotheo alijisikia namna gani alipopokea mugawo huo?

UAMUZI WA MAANA SANA KATIKA MAISHA YAKO

3. Ni uamuzi gani ulio wa maana sana katika maisha yako, na ni wakati gani unaofaa zaidi ili kuchukua uamuzi huo?

3 Kipindi cha ujana ndio wakati muzuri wa kuchukua maamuzi ya maana. Lakini uamuzi wako wa kumutumikia Mungu ndio uamuzi mumoja tu ulio wa maana zaidi kuliko maamuzi yote. Ni wakati gani unaofaa zaidi ili kuchukua uamuzi huo? Yehova anasema hivi: ‘Mukumbuke . . . Muumba wako Mukubwa katika siku za ujana wako.’ (Mhu. 12:1) Njia moja tu ya ‘kumukumbuka’ Yehova ni kumutumikia kwa moyo wako wote. (Kum. 10:12) Uamuzi wako wa kumutumikia Mungu kwa moyo wako wote ndio uamuzi wa maana sana kuliko maamuzi yote unayoweza kufanya. Uamuzi huo unaweza kubadili maisha yako ya wakati ujao.​—Zab. 71:5.

4. Ni maamuzi gani mengine ya maana yatakayokuwa na matokeo juu ya namna yako ya kumutumikia Mungu?

4 Bila shaka, zaidi ya uamuzi wako wa kumutumikia Yehova, kuna maamuzi mengine yanayoweza kubadili maisha yako ya wakati ujao. Kwa mufano, unaweza kujiuliza ikiwa siku moja utaoa ao kuolewa, utaoa ao kuolewa na nani, na utafanya kazi gani ili kutosheleza mahitaji yako. Hayo ni maamuzi ya maana, lakini mbele ya kuamua kuhusu mambo hayo, ni vizuri uamue kwanza kumutumikia Yehova kwa moyo wako wote. (Kum. 30:19, 20) Sababu gani? Kwa sababu maamuzi hayo yote yanahusiana sana. Maamuzi utakayofanya kuhusu ndoa na kazi yanaweza kuwa na matokeo juu ya namna yako ya kumutumikia Mungu. (Linganisha na Lu. 14:16-20.) Kwa upande mwingine, tamaa yako ya kumutumikia Mungu inaweza kukusaidia uchukue maamuzi mazuri kuhusu ndoa na kazi. Kwa hiyo ni vizuri uamue kwanza ni mambo gani yaliyo ya maana zaidi katika maisha yako.​—Flp. 1:10.

UTAFANYA NINI KATIKA UJANA WAKO?

5, 6. Eleza namna gani kuchukua maamuzi mazuri kunaweza kumuongoza mutu kwenye mapendeleo mengine katika kazi ya Yehova. (Soma habari “Uamuzi Niliochukua Nilipokuwa Kijana Mudogo” katika gazeti hili.)

5 Kisha kuamua kumutumikia Mungu, unaweza sasa kufikiria yale ambayo Mungu anataka ufanye, na namna ya kumutumikia. Ndugu mumoja Mujapani anayeitwa Yuichiro anasema hivi: “Nilipokuwa na miaka 14, siku moja nilikuwa katika mahubiri pamoja na muzee wa kutaniko letu. Muzee huyo alitambua kwamba sifurahie mahubiri. Kisha aliniambia hivi kwa upole: ‘Yuichiro, rudia nyumbani. Utakapofika nyumbani, kaa kwenye kiti na ufikiri sana kuhusu mambo ambayo Yehova amekufanyia.’ Nilifanya kama alivyoniambia. Kwa hiyo, niliendelea kufikiri na kusali kwa muda wa siku fulani. Pole kwa pole, mutazamo wangu ulianza kubadilika. Kisha, nilianza kufurahia mahubiri. Nilifurahia kusoma habari kuhusu wamisionere, na nilianza kufikiria namna ambavyo ningefanya mengi zaidi katika kazi ya Mungu.”

6 Yuichiro anaendelea kusema hivi: “Niliamua kuanza kufanya mambo fulani ambayo yangeniwezesha siku moja kumutumikia Yehova katika inchi za kigeni. Kwa mufano, niliamua kujifunza Kiingereza. Nilipomaliza masomo ya segondere, niliamua kuanza kufundisha Kiingereza. Kazi hiyo haikunichukua muda mwingi na iliniwezesha kufanya upainia. Nilipokuwa na miaka 20, nilianza kujifunza Kimongolia na nilitembelea kikundi kimoja cha wahubiri wanaozungumuza Kimongolia. Miaka miwili baadaye, ni kusema katika mwaka wa 2007, nilitembelea Mongolia. Nilipoenda kuhubiri pamoja na mapainia fulani na kuona namna watu wengi walivyokuwa na hamu ya ukweli, nilitamani kuhamia huko ili kuwasaidia. Kisha, nilirudi Japani ili kufanya mipango ya kuhama. Nimefanya kazi ya upainia hapa Mongolia kuanzia Mwezi wa 4, 2008. Maisha si rahisi hapa. Lakini watu wanakubali habari njema, na ninaweza kuwasaidia wamukaribie Yehova. Ninafikiri kwamba nilichukua uamuzi muzuri sana.”

7. Ni mambo gani ambayo tunapaswa kujiamulia, na Musa alituachia mufano gani?

7 Kila mutu anapaswa kujiamulia namna atakavyomutumikia Yehova. (Yos. 24:15) Hakuna mutu anayeweza kukuambia kwamba unapaswa kuoa ao kuolewa, uoe nani ao uolewe na nani, ao ufanye kazi ya namna gani. Unapaswa pia kujiamulia ikiwa utachagua kazi inayoomba mazoezi kidogo ao hapana. Vijana fulani Wakristo wanaishi katika vijiji maskini; wengine wanaishi katika miji tajiri. Kila kijana ana sifa, uwezo, uzoefu, mapendezi, na imani isiyolingana na ya mwengine. Hali zenu zinatofautiana kama vile hali za vijana Waebrania zilivyotofautiana na zile za kijana Musa. Aliishi katika makao ya mufalme, lakini vijana wengine Waebrania walikuwa watumwa. (Kut. 1:13, 14; Mdo. 7:21, 22) Vijana hao waliishi katika kipindi cha maana kama ninyi. (Kut. 19:4-6) Kila mumoja wao alipaswa kuamua kile atakachofanya katika maisha yake. Musa alichukua uamuzi muzuri.​—Soma Waebrania 11:24-27.

8. Ni nini inayoweza kusaidia vijana wachukue maamuzi yenye hekima kuhusu wakati ujao?

8 Yehova anakutolea mashauri yanayoweza kukusaidia uchukue maamuzi yenye hekima. Anakutolea kanuni za Biblia unazoweza kutumia katika hali yoyote ya maisha yako. (Zab. 32:8) Zaidi ya hilo, wazazi wako ambao ni Wakristo na vilevile wazee katika kutaniko wanaweza kukusaidia kufikiri kuhusu namna ya kutumia kanuni hizo. (Met. 1:8, 9) Tuzungumuzie sasa kanuni tatu za Biblia zinazoweza kukusaidia uchukue maamuzi yenye hekima yatakayokusaidia uwe na maisha mazuri wakati ujao.

KANUNI TATU ZA KUKUONGOZA

9. (a) Namna gani Yehova anaonyesha kwamba anakuheshimu? (b) ‘Kutafuta kwanza Ufalme’ kunatutolea nafasi gani?

9 Tafuta kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake. (Soma Mathayo 6:19-21, 24-26, 31-34.) Yehova anakuheshimu kwa kukutolea uhuru wa kuchagua. Hakuambie utumie wakati wote katika mahubiri. Lakini Yesu anakuambia utafute kwanza Ufalme. Kutii maneno ya Yesu kunakutolea nafasi ya kuonyesha ikiwa unamupenda Mungu na majirani wako, na ikiwa unasamini tumaini la uzima wa milele. Unapofikiria ndoa ao kazi, chunguza ikiwa maamuzi yako yatakufanya uhangaikie sana mambo ya kimwili ao yatakufanya uonyeshe bidii kwa ajili ya Ufalme wa Mungu na haki yake.

10. Ni nini iliyomuletea Yesu furaha, na unapaswa kufanya nini ili uwe na furaha?

10 Pata furaha kwa kuwatumikia wengine. (Soma Matendo 20:20, 21, 24, 35.) Yesu alifundisha kanuni hiyo ya maana katika maisha. Alikuwa mutu mwenye furaha nyingi kwa sababu alifanya mapenzi ya Baba yake wala si mapenzi yake mwenyewe. Yesu alifurahia kuona namna watu wanyenyekevu walivyokubali habari njema. (Lu. 10:21; Yoh. 4:34) Pengine umekwisha kupata furaha inayotokana na kuwatumikia wengine. Ikiwa unategemea kanuni ambazo Yesu alifundisha unapochukua maamuzi ya maana sana katika maisha, bila shaka utapata furaha na utamufurahisha Yehova.​—Met. 27:11.

11. Sababu gani Baruku alipoteza furaha yake, na Yehova alimutolea shauri gani?

11 Furaha kubwa zaidi inatokana na kumutumikia Yehova. (Met. 16:20) Inaonekana kwamba Baruku, aliyekuwa mwandishi wa Yeremia, alisahau jambo hilo. Wakati fulani, hakufurahia tena kumutumikia Yehova. Yehova alimuambia hivi: ‘Unaendelea kujitafutia mambo makubwa. Usiendelee kuyatafuta. Kwa maana karibuni nitaleta musiba juu ya wote wenye mwili, . . . na nitakupa uzima wako kuwa nyara mahali popote utakapoenda.’ (Yer. 45:3, 5) Unawaza ni jambo gani ambalo lingemuletea Baruku furaha: Kutafuta mambo makubwa ao kumutumikia Yehova kwa uaminifu ili kuokoka uharibifu wa Yerusalemu?​—Yak. 1:12.

12. Ni uamuzi gani uliomusaidia ndugu Ramiro awe na maisha yenye furaha?

12 Ndugu Ramiro alipata furaha kwa kuwatumikia wengine. Anasema hivi: “Nilikomalia katika kijiji kinachopatikana kwenye Milima ya Andes. Familia yangu ilikuwa maskini. Kwa hiyo wakati kaka yangu aliahidi kunilipia masomo ya juu, hiyo ilikuwa bahati kabisa. Lakini nilikuwa nimebatizwa hivi karibuni, na painia mumoja alikuwa amenialika ili nihubiri naye katika muji fulani mudogo. Nilienda huko, nilijifunza kukata nywele, na nilifungua chumba cha kukatia nywele ili nipate feza kwa ajili ya mahitaji yangu. Watu wengi ambao tulihubiria walikubali kujifunza Biblia. Baadaye, nilijiunga na kutaniko mupya ambalo lilikuwa limeanzishwa katika luga ya eneo hilo. Sasa nimefanya upainia kwa miaka kumi katika eneo hilo. Hakuna kazi ambayo ingeweza kuniletea furaha ninayopata kwa kuwasaidia watu wajifunze Biblia katika luga yao.”

Maamuzi ambayo Ramiro alifanya ili kumutumikia Yehova kuanzia umri mudogo na kuendelea

Ndugu Ramiro amekuwa mwenye furaha kwa kumutumikia Yehova tangu ujana wake (Ona fungu la 12)

13. Sababu gani wakati mutu angali kijana ndio wakati muzuri wa kufanya mengi katika kazi ya Yehova?

13 Mutumikie Yehova wakati ungali kijana. (Soma Mhubiri 12:1.) Usifikiri kwamba inafaa kwanza kuwa na kazi nzuri mbele ya kuanza kumutumikia Yehova. Huu ndio wakati wa kufanya mengi katika kazi ya Yehova. Vijana wengi hawajakuwa na madaraka ya familia na wana afya nzuri na nguvu ambayo wanaweza kutumia ili kushugulikia migawo migumu. Unapenda umufanyie Yehova nini wakati ungali kijana? Pengine unataka kuwa painia ao unataka kutumikia katika eneo la luga ya kigeni. Ao pengine unaona kwamba unaweza kufanya mengi katika kutaniko lako. Iwe unataka kufanya nini katika kazi ya Mungu, utahitaji kazi itakayokusaidia kupata mahitaji ya kila siku. Utachagua kazi gani? Na utajifunza kazi hiyo kwa muda gani?

TUMIA KANUNI ZA BIBLIA ILI KUCHUKUA MAAMUZI YENYE HEKIMA

14. Kijana anapaswa kuwa mwangalifu kuhusu mambo gani anapochukua maamuzi kuhusu kazi?

14 Kanuni tatu za Biblia ambazo tumezungumuzia zinaweza kukusaidia uchukue maamuzi mazuri kuhusu kazi. Bila shaka, waalimu wako wanajua kazi zinazopatikana katika eneo lako. Ao pengine shirika la serikali linaweza kukuambia kazi zinazohitajiwa katika eneo lako na mahali ambapo unaweza kupata kazi. Watu hao wanaweza kukutolea mashauri mazuri, lakini unapaswa kuwa mwangalifu. Watu ambao hawamupendi Yehova wanaweza kupanda upendo wa ulimwengu katika moyo wako. (1 Yoh. 2:15-17) Unapofikiria mambo ambayo unaweza kupata katika ulimwengu huu, moyo wako unaweza kukudanganya kwa urahisi.​—Soma Methali 14:15; Yer. 17:9.

15, 16. Ni nani anayeweza kukutolea mashauri mazuri kuhusu kazi?

15 Kisha kujua kazi zinazopatikana, unahitaji mashauri mazuri. (Met. 1:5) Ni nani anayeweza kukusaidia kuchunguza ikiwa kazi fulani haipingane na kanuni za Biblia? Sikiliza mashauri ya wale wanaomupenda Yehova, wanaokupenda, na wanaokujua vizuri. Watakusaidia kuchunguza uwezo wako mbalimbali na nia yako. Pengine mashauri yao yatakusaidia ufikirie tena miradi yako. Wewe ni mwenye kubarikiwa hata zaidi ikiwa wazazi wako ni Mashahidi wa Yehova! Pia, wazee katika kutaniko lako ni wanaume wenye kukomaa kiroho wanaoweza kukutolea mashauri mazuri. Zaidi ya hilo, unaweza kuzungumuza na mapainia na waangalizi wanaosafiri. Unaweza kuwauliza hivi: Sababu gani waliamua kufanya utumishi wa wakati wote? Namna gani walianza kazi ya upainia, na wanapata mahitaji ya kimwili namna gani? Ni furaha gani wanayopata katika utumishi wao?​—Met. 15:22.

16 Wale wanaokujua vizuri ndio wanaweza kukutolea mashauri mazuri. Kwa mufano, pengine unataka kuacha masomo ya segondere ili uwe painia kwa sababu tu unaona kama masomo yanakuchokesha. Mutu anayekupenda anaweza kuvumbua nia yako na anaweza kukusaidia uelewe kwamba masomo yanaweza kukusaidia uwe muvumilivu, asiyevunjika moyo haraka. Sifa hiyo itakusaidia ufanye mengi katika kazi ya Yehova.​—Zab. 141:5; Met. 6:6-10.

17. Ni maamuzi gani ambayo tunapaswa kuepuka?

17 Kila mutu anayemutumikia Yehova anaweza kupambana na majaribu ambayo yanaweza kuharibu uhusiano wake na Yehova. (1 Kor. 15:33; Kol. 2:8) Lakini kazi fulani zinaweza kukuingiza katika majaribu zaidi kuliko zingine. Je, kuna watu fulani mahali unapoishi ambao ‘imani yao ilivunjika’ kisha kuchagua kazi fulani? (1 Tim. 1:19) Ni jambo la hekima uepuke maamuzi yanayoweza kuhatarisha uhusiano wako na Mungu.​—Met. 22:3.

FURAHIA KUWA KIJANA MUKRISTO

18, 19. Ikiwa haujakuwa na nia ya kumutumikia Yehova, unapaswa kufanya nini?

18 Ikiwa nia yako ni kumutumikia Yehova, tumia nafasi anazokutolea za kumutumikia wakati ungali kijana. Chukua maamuzi yatakayokusaidia umutumikie katika kipindi hiki cha maana.​—Zab. 148:12, 13.

19 Lakini, unapaswa kufanya nini ikiwa haujakuwa na nia ya kumutumikia Yehova? Endelea kutia nguvu imani yako. Kisha kueleza jitihada alizofanya ili kuishi maisha yenye kumupendeza Mungu, mutume Paulo aliandika hivi: ‘Ikiwa muna muelekeo wa akili ulio tofauti na huo kwa jambo lolote, Mungu atawafunulia ninyi mutazamo huo ulio hapo juu. Kwa vyovyote, kwa kadiri ambavyo tumefanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu katika kawaida hiyohiyo.’ (Flp. 3:15, 16) Usisahau kwamba Yehova anakupenda. Endelea kufuata mashauri yake yenye hekima. Yehova pekee anaweza kukusaidia kuchukua maamuzi yenye hekima wakati ungali kijana.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine