Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/9 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Viumbe wa Kiroho: Ni Marafiki ao Maadui Wetu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kweli Juu ya Malaika
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ukweli Kuhusu Malaika
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Namna Gani Malaika Wanaweza Kukusaidia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/9 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Malaika wanaweza kutusaidia?

Malaika anamulinda Danieli katika shimo la simba

Kama walivyomusaidia Danieli, mutumishi muaminifu wa Mungu wa zamani, leo malaika wanasaidia watu wenye mioyo mizuri wafaidike na habari njema

Yehova Mungu aliumba mamilioni ya malaika zamani sana mbele ya kuumba watu. (Ayubu 38:4, 7) Malaika hao ni viumbe wa kiroho wenye nguvu wanaofanya kazi ya Mungu, wakati fulani Mungu anawatuma ili kuongoza na kulinda watumishi wake duniani. (Zaburi 91:10, 11) Leo, malaika wanasaidia watu ili wafaidike na habari njema ambayo wafuasi wa Yesu wanahubiri.—Soma Ufunuo 14:6, 7.

Tunapaswa kuomba malaika watusaidie? Hapana. Sala ni tendo la ibada, linalostahili Mungu tu. (Ufunuo 19:10) Kwa sababu malaika ni watumishi wa Mungu, wanakubali maagizo ya Mungu lakini hawakubali maagizo ya watu. Kwa hiyo, sikuzote tunapaswa kusali kwa Mungu tu kupitia Yesu.—Soma Zaburi 103:20, 21; Mathayo 26:53.

Kuna malaika wabaya?

Kama wanadamu, malaika waliumbwa wakiwa na uhuru wa kuchagua na wanaweza kuchagua kufanya mambo mazuri ao mabaya. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba malaika wengi walimuasi Mungu. (2 Petro 2:4) Wa kwanza kati ya malaika hao ni Shetani; wengine walimufuata na wakakuwa mashetani. Katika miaka ya hivi karibuni, Shetani na mashetani wake walifukuzwa mbinguni na wakatupwa duniani.—Soma Ufunuo 12:7-9.

Kuongezeka sana kwa uovu na jeuri tangu mwaka wa 1914 kunaonyesha kwamba hivi karibuni Mungu atazuia Shetani na mashetani wake wasidanganye tena watu. Kisha Mungu atarudisha dunia katika hali yake nzuri.—Soma Ufunuo 12:12; 21:3, 4.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 10 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine