Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/12 uku. 3
  • Unajisikia Kuwa Rafiki ya Mungu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unajisikia Kuwa Rafiki ya Mungu?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • INAWEZEKANA KUWA RAFIKI YA MUNGU
  • Kuwa Rafiki ya Mungu Ndiyo Njia ya Muzuri Zaidi ya Maisha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Unazoea Kuzungumuza na Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mungu Ndiye Rafiki Bora Unayeweza Kuwa Naye
    Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/12 uku. 3
Mwanaume anayewaza juu ya Mungu

KICHWA | UNAWEZA KUWA RAFIKI YA MUNGU

Unajisikia Kuwa Rafiki ya Mungu?

“Kuwa na urafiki na Mungu kunakufanya ujisikie kuwa salama, muzima, na mwenye kutulia. Kunakufanya ujisikie kuwa Mungu anakutafutia mema sikuzote.”—CHRISTOPHER, KIJANA ANAYEISHI KATIKA INCHI YA GHANA.

“Mungu anaona magumu yako yote, na anakuonyesha upendo zaidi na kukuhangaikia zaidi kuliko vile ungeweza kumuomba.”—HANNAH ALIYE NA MIAKA 13, ANAYEISHI KATIKA ALASKA, AMERIKA.

“Kujua kama uko rafiki wa sana wa Mungu ni jambo la muzuri zaidi na linakufanya ujisikie kuwa mwenye kutulia!”—GINA, MWANAMUKE WA JAMAIKA MWENYE MIAKA KATI YA 41 NA 50.

Kuna watu wengine wanaojisikia kama Christopher, Hannah, na Gina. Watu wengi duniani wako hakika kuwa Mungu anawaona kuwa marafiki wake. Wewe pia unaona vile? Unajisikia kuwa rafiki wa sana wa Mungu? Ao ungependa kuwa rafiki yake ao rafiki yake wa sana? Labda unajiuliza: ‘Inawezekana kabisa mutu afanye urafiki wa sana na Mungu Mweza-Yote? Ikiwa ndiyo, namna gani?’

INAWEZEKANA KUWA RAFIKI YA MUNGU

Biblia inaonyesha kama inawezekana kufanya urafiki wa sana na wa pekee na Mungu. Inaonyesha kama Mungu alimuita Abrahamu muzee wa ukoo Muebrania “rafiki yangu.” (Isaya 41:8) Tena, ona mwaliko wenye upendo unaopatikana katika andiko la Yakobo 4:8: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’ Kwa hiyo, ni wazi kuwa inawezekana kufanya uhusiano ao urafiki na Mungu. Lakini kwa kuwa Mungu haonekane, namna gani unaweza ‘kumukaribia’ na kufanya urafiki muzuri naye?

Ili kujibia ulizo hilo, fikiria namna watu wawili wanafanya urafiki. Mara nyingi watu wawili wanaanza urafiki kwa kuambiana kwanza majina. Kisha, wanapozungumuza mara kwa mara, kwa kubadilishana mawazo na kuambiana namna wanajisikia moyoni, urafiki wao unakomaa. Na wakati wanajikaza kusaidiana, urafiki wao unakuwa nguvu zaidi. Ni vile pia mutu anafanya urafiki na Mungu. Acha tuone namna gani mutu anaweza kufanya vile.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine