Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/12 uku. 8-10
  • Timgad—Muji Uliozikwa Unafunua Siri Zake

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Timgad—Muji Uliozikwa Unafunua Siri Zake
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUSUDI LA KISIASA LILILOFICHWA
  • NAMNA WAROMA WALIVUTA MIOYO YA WATU
  • MUJI MUZURI UNASAHAULIKA
  • “HAYO NDIYO MAISHA!”
  • Je, Unakumbuka?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Namna “Fundisho la Yehova” Lilifikia Mataifa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/12 uku. 8-10
Mabomoko ya muji wa zamani wa Thamugadi, unaoitwa leo Timgad

Timgad—Muji Uliozikwa Unafunua Siri Zake

MUVUMBUZI asiye na woga hakuamini jambo aliona. Aliona monima ya ushindi ya Waroma iliyokuwa yenye kuzikwa kwa sehemu katika muchanga wa jangwa la Aljeria! Wakati Scotsman James Bruce alifanya uvumbuzi huo katika mwaka wa 1765, hakujua kuwa alikuwa anasimama juu ya makao makubwa zaidi yenye Waroma walijenga katika Afrika ya Kaskazini, ni kusema, muji wa zamani wa Thamugadi, unaoitwa leo Timgad.

Monima ya ushindi ya Waroma katika Timgad

Zaidi ya miaka mia moja kisha hapo, katika mwaka wa 1881, wavumbuzi Wafaransa walianza kuvumbua sehemu zilizobaki za muji wa Timgad zenye zilibaki bila kuharibiwa. Waliamua kuwa hata ikiwa eneo hilo halikuwa na mbolea na lilikuwa katika hali mbaya, wakaaji wake walikuwa na maisha ya muzuri na ya starehe. Ni nini iliwachochea Waroma wajenge muji wenye utajiri katika nafasi kama hiyo? Na tunaweza kujifunza nini kutokana na muji huo wa zamani na wakaaji wake?

KUSUDI LA KISIASA LILILOFICHWA

Wakati Waroma walipanua utawala wao mupaka Afrika ya Kaskazini kati ya mwaka wa 1 na 100 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, walipingwa sana na makabila yanayohama-hama. Namna gani Waroma walifanya amani na watu wa eneo hilo? Kwanza, askari wa Augusto wa Lejioni ya Tatu walijenga kambi nyingi na nyumba nyingi za walinzi katika eneo kubwa la milima la sehemu inayojulikana leo kuwa Algeria ya kaskazini. Kisha, walijenga muji unaoitwa Timgad, lakini wakiwa na kusudi lingine.

Kusudi la Waroma la kujenga muji wa Timgad lililojulikana waziwazi lilikuwa kwa ajili ya maaskari wa zamani, lakini walijenga muji huo wakiwa na kusudi la kuregeza ushambulizi wa makabila ya eneo hilo. Mupango wao ulikuwa na matokeo ya muzuri. Bila kukawia, hali ya muzuri ya maisha katika muji wa Timgad ilianza kuvutia watu wa eneo hilo waliokuwa wanakuja katika muji ili kuuzisha vitu vyao. Wakitumainia kukubaliwa katika muji wa Timgad, ambamo raia Waroma tu ndio waliruhusiwa kuishi, wazaliwa wengi wa eneo hilo walijiunga bila kulazimishwa na Jeshi la Waroma kwa kipindi cha miaka 25 ili wao na watoto wao wanaume wakubaliwe kuwa raia wa Roma.

Kwa kuwa hawakutosheka tu na kuwa raia wa Roma, kisha wakati kupita, Waafrika fulani walijikaza hata kupata vyeo katika muji wa Timgad na katika miji mingine iliyotawaliwa na Waroma. Mupango wa ujanja wa Waroma wa kuchangamana na wakaaji wa eneo hilo ulikuwa na matokeo mazuri. Miaka 50 tu kisha kuundwa kwa muji wa Timgad, wakaaji wengi wa muji huo walikuwa watu wa Afrika ya Kaskazini.

NAMNA WAROMA WALIVUTA MIOYO YA WATU

Mabomoko ya nafasi ya soko yenye kuwa na nguzo zenye kuvutia na meza za kuuzishia katika Timgad

Nafasi ya soko yenye kuwa na nguzo zenye kuvutia na meza za kuuzishia

Namna gani Waroma waliweza kuvuta haraka mioyo ya watu wa eneo hilo? Kwanza, waliunda kanuni ya kuwaona raia wote kuwa sawa, iliyofundishwa na Cicero, ofisa Muroma. Muji uligawanywa sawasawa kati ya Askari wa zamani wa Roma na watu wa Afrika waliogeuka kuwa raia wa Roma. Muji ulijengwa kwa uangalifu, ulikuwa na nyumba za metre 20 za muraba na zilitenganishwa na njia nyembamba. Mupango huo wa kuwa na nyumba zenye ukubwa moja na utaratibu katika muji huo vilivutia sana wakaaji.

Kama ilivyokuwa katika miji ya Roma, wakaaji walikutana kwenye baraza siku za soko zenye watu wengi ili kusikiliza habari za mupya ao kucheza michezo. Wazaliwa wa maeneo ya karibu-karibu ya milima isiyokuwa na maji bila shaka walifurahia kutembea chini ya nguzo zenye kivuli katika siku ya joto na isiyokuwa na mvua. Walipenda pia kujifurahisha katika vyumba vingi vya kuogea vya watu wote wakisikia sauti ya maji yanayotiririka. Wangeweza kufurahia kukaa karibu na visima vyenye maji yenye kuburudisha, wakizungumuza na marafiki. Mambo hayo yote yanapaswa kuwa yalionekana kama ndoto kwao.

Jiwe lililowekwa kwenye kaburi lililokuwa na michoro ya miungu mitatu, ni kusema, miungu ya wazaliwa wa eneo hilo na miungu ya Waroma

Jiwe la kuweka kwenye kaburi lenye miungu mitatu

Jumba la maonyesho lisilofunikwa lilikuwa pia na kazi ya maana katika kuvuta mioyo ya watu. Jumba hilo lililokuwa na nafasi za kukaa za watu zaidi ya 3500, lilipokea watu wengi sana wenye kelele waliotoka katika muji wa Timgad na miji ya karibu-karibu. Kwenye jukwaa, wachezaji walionyesha watu mambo machafu ya kujifurahisha ya Waroma kupitia michezo iliyoonyesha mara nyingi mambo ya uasherati na ya kupigana na kuuana.

Dini ilifanya pia watu wapende desturi za Waroma. Kwenye sehemu ya chini na kwenye kuta za nyumba zilizokuwa na vyumba vya kuogea, kulikuwa michoro yenye kufanywa kwa majiwe ya rangi mbalimbali iliyoonyesha mambo ya hadisi za kutungwa za kipagani. Kwa kuwa kuoga lilikuwa jambo la maana katika maisha ya kila siku, wakaaji wa muji huo walijua polepole miungu na dini ya Waroma. Nia ya kujaribu kuchanga desturi za Waafrika pamoja na za Waroma ilikuwa na matokeo mazuri hivi kwamba mara nyingi majiwe yaliyowekwa kwenye makaburi yalikuwa na michoro ya miungu mitatu ya sehemu zote mbili, ni kusema, miungu ya wazaliwa wa eneo hilo na miungu ya Waroma.

MUJI MUZURI UNASAHAULIKA

Kisha Mutawala Trajan kuunda muji huo katika mwaka wa 100 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Waroma walitia watu moyo walime mbegu, watengeneze mafuta ya zeituni, na divai katika eneo lote la Afrika ya Kaskazini. Bila kukawia eneo hilo likakuwa depo ya Waroma, liliwatolea vitu hivyo vya lazima. Kama vile miji mingine iliyotawaliwa na Roma, muji wa Timgad uliendelea muzuri chini ya utawala wa Roma. Kisha wakati kupita, wakaaji wa muji wa Timgad waliongezeka, na muji ukaendelea kupanuka mupaka inje ya mipaka yake.

Wakaaji wa muji na watu wenye mashamba walipata utajiri kwa kufanya biashara na Roma, lakini wenye mashamba walipata faida kidogo tu. Kati ya mwaka wa 201 na 300 kisha kuzaliwa kwa Yesu, ukosefu wa haki na kodi zenye kupita kiasi zilifanya wenye mashamba wa hali ya chini waasi Waroma. Wamoja kati yao, waliokuwa Wakatoliki, walijiunga na Wadonati, ni kusema, kikundi cha watu waliojiita kuwa Wakristo kilichoanzishwa ili kupinga rushwa iliyokuwa katika Kanisa Katoliki.—Soma kisanduku “Wadonati—Si ‘Kanisa Safi.’”

Kisha kufanya mamia ya miaka katika ugomvi wa kidini, vita vya watu wenyewe kwa wenyewe, na mashambulizi ya watu wabaya, utawala wa Roma ulipoteza nguvu zake katika Afrika ya Kaskazini. Kuanzia mwaka kati ya 501 na 600 kisha kuzaliwa kwa Yesu, muji wa Timgad uliharibiwa na makabila ya Waarabu wa eneo hilo na muji ukasahauliwa polepole kwa miaka zaidi ya 1000.

“HAYO NDIYO MAISHA!”

Maandishi ya Kilatini yaliyokuwa kwenye baraza katika Timgad

Maandishi ya Kilatini kwenye baraza yanayosema hivi: “Kuwinda, kuoga, kucheza, kucheka, hayo ndiyo maisha!”

Wavumbuzi wa vitu vya zamani waliovumbua sehemu zilizobaki za muji wa Timgad walifurahi kuona maandishi ya kilatini yaliyokuwa kwenye baraza. Maandishi hayo yanasomekana hivi: “Kuwinda, kuoga, kucheza, kucheka, hayo ndiyo maisha!” Mwanahistoria mumoja Mufaransa anasema kuwa maneno hayo “yanaonyesha wazo la kwamba pengine watu hawakukuwa na tamaa ya kutafuta mambo makubwa, lakini watu fulani wanaona wazo hilo kuwa siri ya kupata hekima.”

Kwa kweli, Waroma waliishi maisha ya namna hiyo kwa wakati fulani. Mutume Mukristo Paulo aliyeishi kati ya mwaka wa 1 na 100 alisema juu ya watu waliokuwa na mawazo haya katika maisha: ‘Tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.’ Hata ikiwa Waroma walipenda dini, waliishi tu kwa furaha ya palepale, hawakuwa wanafikiria maana na kusudi la maisha la wakati unaokuja. Paulo alishauria Wakristo wenzake wajiepushe na watu kama hao. Alisema hivi: ‘Musipotoshwe [ao musidanganyike]. Mashirika [ao marafiki] mabaya yanaharibu tabia nzuri.’—1 Wakorintho 15:32, 33.

Hata ikiwa watu wa muji wa Timgad waliishi kumepita miaka 1500 hivi, mawazo ya watu juu ya maisha hayajabadilika sana. Watu wengi leo wanaishi wakifikiria tu wakati wa sasa. Watu hao wanaona mawazo ya Waroma juu ya maisha kuwa ya muzuri sana, bila kufikiria matokeo. Lakini, Biblia inatoa mawazo haya mafupi na yenye kufaa: “Mambo ya dunia hii yanapita.” Kwa sababu hiyo inatuomba ‘tusitumie dunia hii kabisa.’—1 Wakorintho 7:31, La sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo.

Mabomoko ya muji wa Timgad yanatoa ushahidi kuwa siri ya kupata maisha yenye furaha na yenye maana haitegemee kufuata maneno ya maandishi yaliyozikwa katika muchanga wa eneo la Afrika ya Kaskazini kumepita miaka mingi. Lakini, inategemea kukazia akili maneno haya ya Biblia: “Ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”—1 Yohana 2:17.

Wadonati—Si ‘Kanisa Safi’

Mabomoko ya mahali pa kubatizia katika Timgad

Mahali pa kubatizia katika Timgad, panaonyesha uriti wa “Kikristo” wa muji huo

Katika eneo la mangaribi la Timgad kuna mabomoko ya Kanisa kubwa lililokuwa na mahali ao kisima cha kubatizia. Hilo linaonyesha kuwa kuanzia kati ya mwaka wa 301 na 400 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, muji huo ulikuwa ngome ya Wadonati, ni kusema, kikundi cha “Wakristo” waliojitenga na kanisa Katoliki.

Wadonati hawakuitika watawala wa Roma wajiingize katika mambo ya kanisa. Walijiona kuwa ‘kanisa safi,’ lililojitenga na ulimwengu. Jambo la kuhuzunisha ni hili: matendo yao hayakuonyesha hivyo. Wadonati walianza kujiingiza katika vita vya watu wenyewe kwa wenyewe na vya kisiasa na waliunga mukono wakulima wa hali ya chini katika uasi wao mukali kuelekea wenye mashamba na Waroma wa kulipisha kodi. Matendo hayo yalifanya wasikubaliwe na serikali. Hata ikiwa walikuwa wanajitapa, Wadonati hawakujionyesha kuwa ‘kanisa safi.’—Yohana 15:19.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine